Monday 27 April 2015

Eden Michael Hazard atangazwa kuwa mchezaji bora wa mwaka England

Image for the news resultBaada ya kusubiri kwa misimu miwili hatimae Eden Hazard wa Chelsea ameibuka mchezaji bora wa mwaka wa England na kutwaa tuzo ya PFA.
Hazard mwenye umri wa miaka 24 amefunga mabao 13 na na kusaidia wafungaji (assists) 8 katika michezo 33 ya ligi kuu ya nchi hiyo na kuisaidia timu yake kushika ususkani katika msimamo wa ligi.
Naye Harry Kane mwenye umri wa miaka 21 ameibuka kidedea kwa kunyakua tuzo ya mchezaji bora chipukizi huku naye Ji So-Yun wa Chelsea akiibuka mshindi kwa upande wa wanawake.
Hazard ambaye msimu uliopita aliibuka mshindi kwa upande wa chipukizi alikabidhiwa tuzo yake katika hoteli ya Grosvenor jijini London jana Jumapili. " ninafuraha sana. Nataka siku moja niwe mjichezaji bora kabisa na na nilichofanya msimu huu ni kucheza vizuri na timu yangu imecheza vizuri sana" alisema Hazard baada ya kupokea tuzo hiyo. "sijui kama nastahili kushinda lakini jambo hili ni zuri kwangu. Ni jambo zuri kupigiwa kura na wachezaji kwasababu wanajua kila kitu kuhusu mpira" aliongeza mchezajia huyo.

No comments: