Monday 27 April 2015

Nigeria wafunga ubalozi wa Afrika kusini nchini mwao

Maandamano ya kupiga chuki dhidi ya wageni Afrika Kusini
Nchi ya Nigeria imewaita mabalozi wake waishio nchini Afrika Kusini warejee nyumbani kufuatia mashambulizi ya kibaguzi dhidi ya wenyeji .
Mpaka sasa watu saba wameshapoteza uhai kufuatia mashambulizi hayo, yaliyoanza wiki tatu zilizo pita.mali zimeharibiwa vibaya na mashambulizi hayo yamizusha hofu kubwa miongoni mwa raia wa kigeni .
Balozi wa Nigeria mjini Pretoria,mji wa kibiashara na kwingineko wanatarajiwa kurejea Nigeria kwa ushauri zaidi .
Taarifa hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki ilieleza wazi baadhi ya waafrika kusini walia andaa maandamano ya Amani na shutuma za Jacob Zuma kulaani mashambulio hayo na kama ambavyo alifanya mfalme Zulu King Goodwill Zwelithini, ambaye anashutumiwa kuwa maoni yake ndiyo chanzo cha vurugu hizo.
Wabunge nchini Nigeria wameitaka serikali ya Afrika Kusini kulipa uharibifu uliotokea na kikundi cha kutetea haki cha Nigeria kimesha peleka malalamiko yake katika mahakama ya uhalifu wa kivita ICC.
Mwishoni kwa wiki iliyopita,katika taarifa iliyotolewa nchini Afrika Kusini,kutoka katika kitengo kinachoshughulikia mahusiano ya kimataifa na ushirika kimerusha lawama zake kwa serikali ya Nigeria kwa hatua waliyoichukua na kuielezea kama isiyo bahati na ya kusikitisha
Katika utetezi wake serikali ya Afrika Kusini imesema kwamba hatua ya mashirika ya kiraia kulaani na kukemea mashambulizi hayo na kutoa wito wa kusitishw akwa mashambulio dhidi ya wageni kutokana na hayo utekelezaji, utulivu wa kijamaa na utaratibu na amri ilitolewa .
Kipekee,wizara ya mambo ya mambo ya nje ya Liberia katika taarifa iliyotolewa Jumapili pamoja na mambo mengine, imeipongeza Afrika Kusini kwa kuadhimisha miaka kadhaa leo April 27 tangu kuondolewa kwa ubaguzi wa rangi nchini humo na uchaguzi wa kidemokrasia uliofanyika nchini humo mnamo mwaka 1994,wizara hiyo imezungumzia hali ngumu nchi hiyo iliyokuwa inapitia ,katika taarifa hiyo Rais Ellen Johnson Sirleaf, mshindi wa tuzo ya Amani,alisema kwamba alikuwa akiiombea nchi hiyo kupata ujasiri na nguvu ya pamoja kwa umuhimu mkubwa iweze kuongoza watu wake katika maamuzi sahihi katika harakati za kutaka kuufunga ukurasa wa kiza uliokuwa ukiiandama nchi hiyo dhidi ya raia wa kigeni.

No comments: