Tuesday 4 April 2017

Shahidi wa kesi ya scorpion anusurika kutupwa jela

Mkazi wa Buguruni jijini hapa, Deus Johakim Magosa (45) ambaye ni shahidi wa nane upande wa Jamhuri katika kesi namba 303 ya mwaka 2016 ya kumjeruhi, kumtoboa macho na kumfanyia unyang’anyi wa kutumia silaha, Saidi Mrisho inayomkabili Salum Njwete ‘Scorpion’ katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala jijini, leo alinusurika kutupwa lupango baada ya Wakili Mwandamizi wa Serikali, Nassoro Katuga kumtuhumu kutoa ushahidi wa uongo.
Wakili Katuga alimtuhumu shahidi huyo  kutokana na kutoa majibu tofauti wakati akimuongoza kutoa ushahidi wake na maelezo aliyoyatoa awali Kituo cha Polisi cha Buguruni.
Awali shahidi huyo alisema mahakamani hapo kuwa hakuwahi kusikia popote kuwa Scorpion amehusishwa katika tukio la kumshambulia Said, lakini baadaye alipobanwa alisema ni kweli alisikia tetesi hizo kuwa mtuhumiwa huyo ndiye aliyefanya tukio hilo. Pamoja na mambo mengine aliyomhoji na kumbaini kuwa anatoa ushahidi wa uongo wakili Katuga
alipomgeukia hakimu aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo, Flora Haule  na kumwambia shahidi anazidi kuidanganya mahakama hiyo na kuitaka mahakama hiyo imchukulie hatua kwa mujibu wa kifungu cha 164 cha ushahidi hapa nchini (Tanzania Evidence Act).
Shahidi huyo alionekana kuwa katika wakati mgumu baada ya wakili huyo kuwaita askari polisi na kuwataka wakae tayari kumchukua shahidi huyo.
Hata hivyo kutokana na ufinyu wa muda hakimu Flora aliahirisha kesi hiyo mpaka Aprili 18 mwaka huu na kumuacha shahidi huyo aondoke na kumtaka kufika tena mahakamani hapo tarehe iliyopangwa bila kukosa ambapo Scorpion naye alirudishwa mahabusu mpaka tarehe hiyo.
Mwandishi wetu alizungumza na mmoja wa wanasheria mahakamani hapo kuhusu ushahidi wa uongo ambapo, mwanasheria huyo alisema unapobainika kutoa ushahidi wa uongo ukiwa ndani ya kiapo unaweza kufungwa jela kati ya miezi sita mpaka mwaka mmoja.

Mchekeshaji kutoka ufaransa aamua kuatamia mayai kwa siku 21

Msanii kutoka Ufaransa Abraham Poincheval anaendelea kuatamia mayai ya kuku akiwa na matumaini kwamba mwishowe yataangua vifaranga.
Msanii huyo anatumia joto kutoka kwa mwili wake kutamia mayao hayo 10.
Poincheval ambaye hufanya uigizaji wa kuigiza mambo ya ucheshi lakini ya hatari tayari ameishi wiki mbili ndani ya dubu, miongoni mwa mambo mengine ya kushangaza.
Atakuwa katika chumba maalum ambacho anatamia mayai, ambapo watalii wanaweza kumtazama katka makumbusho ya Palais de Tokyo mjini Paris.
Anatarajia kutamia mayai hayo kwa siku 21 hadi 26.

Saturday 1 April 2017

Vilabu vya Ujerumani vya gombania saini ya Samatta

Image result for mbwana samatta kukipiga bundesliga
Vilabu vitatu vya Ligi ya Ujerumani, maarufu kama Bundesliga vinamfuatilia kwa ukaribu mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta.

Kwa mujibu wa wakala anayeishi Ubelgiji makachero wa timu za  Wolfsburg, Hamburger SV na  Borussia Mönchengladbach  wamekuwa wakimfuatilia Samatta anayetajwa kuwekewa thamani ya euro milioni 10.

Klabu ya Genk inasemekana iko tayari kumuachi Samatta mwenye mkataba hadi mwaka 2020 kwa dau lisilopungua euro milioni 10 licha ya kumnunua kwa Euro 800,000 kutoka klabu ya TP Mazembe mwanzoni mwa mwaka jana.

Liuakali aeleza alivyoteseka gerezani

Mbunge  Mhe Lijualikali: Nimepata mateso makali Ukonga.

Kuishi gerezani unapaswa kuwa mvumilivu na mwenye busara. Kuna mateso ya kikatili ambayo ambayo wafungwa wanafanyiwa. Kuna wakati niliumwa malaria daktari akashauri nipumzike. Lakini nilifanyishwa kazi ngumu na kuhatarisha afya yangu.”
Askari Magereza saikolojia yao bado ipo kikoloni. Nimeshuhudia mtu anapigwa hadi anatambaa. Kuna harassment ambazo nilikuwa nafanyiwa. Nilipigwa sana.
“Gerazani kuna madaraja matatu, daraja la kwanza, la kati na la tatu. Kwa nafasi yangu ya ubunge nilipaswa kuwekwa daraja la kwanza. Ningekufa taifa lingepata hasara kubwa. Lingepoteza zaidi ya bilioni tano kurudia uchaguzi.
“Wakati haya yanafanywa kwa wafungwa wa kawaida, wezi wa meno ya tembo wakiwemo raia wa China wenyewe wanapewa huduma maalum ambazo ni nzuri, tena daraja la kwanza,” amesema Lijualikali.

TAARIFA TOKA MAHAKAMA KUU KANDA YA DAR ES SALAAM

JAJI DYANSOBELA AMZUIA MSAJILI JAJI FRANCIS MUTUNGI KUTOA FEDHA ZA UMMA (RUZUKU YA CUF) KWA LIPUMBA NA KUNDI LAKE:
THE CIVIC UNITED FRONT
(CUF–Chama Cha Wananchi)
THE DIRECTORATE OF INFORMATION, PUBLICITY AND PUBLIC RELATION
P.O.BOX 10979 DAR ES SALAAM
TAARIFA KWA UMMA
Imetolewa leo Tarehe 31/3/2017
Na. Kurugenzi ya Habari, Uenezi Na Mahusiano Na Umma-CUF Taifa
JAJI DYANSOBELA AMZUIA MSAJILI KUTOA FEDHA ZA UMMA (RUZUKU) KWA LIPUMBA NA KUNDI LAKE:
MAHAKAMA KUU KANDA YA DAR ES SALAAM MBELE YA MHESHIMIWA JAJI DYANSOBELA katika Shauri No.  28/2017 leo Tarehe 31/03/2017 IMETOA AMRI DHIDI YA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA NCHINI JAJI FRANCIS MUTUNGI KUMZUIA KUTOTOA FEDHA ZA RUZUKU YA THE CIVIC UNITED FRONT (CUF-CHAMA CHA WANANCHI) MPAKA SHAURI NAMBA 21/2017 DHIDI YA MSAJILI NA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI KUHUSU KUTOA FEDHA ZA RUZUKU SHILINGI MILIONI 369 KWA NJIA ZA WIZI NA UDANGANYIFU LITAKAPOSIKILIZWA NA KUTOLEWA MAAMUZI.
Amri hiyo ya Mahakama Kuu imekuja baada ya Jopo la Mawakili wasomi wa Chama wanaoiwakilisha Bodi ya Wadhamini ya CUF (THE REGISTERED TRUSTEES OF THE CIVIC UNITED FRON (CUF-CHAMA CHA WANANCHI) Mhe. Juma Nassor, Mhe Daimu Halfani na Hashim Mziray kuwasilisha maombi hayo mbele ya Mahakama Kuu kuiomba Mahakama Kuu kutoa Amri hiyo kwa kuwa fedha zilizotolewa awali Milioni 369 hazijulikani zimetumika vipi, na hazikuwa katika mikono salama wala hakuna udhibiti wowote wa Chama –CUF juu ya fedha hizo ikizingatiwa kuwa Lipumba alishavuliwa Uanachama. Wakili Msomi Juma Nassor aliyewasilisha maombi hayo aliweka mkazo na kusisitiza kuwa kwa mazingira yaliyopo ni vyema na Busara kwa fedha za umma zilizopaswa kutolewa kama Ruzuku kwa Chama Cha CUF kwa sasa ZIENDELEE KUBAKIA SERIKALINI.  Aidha, Mawakili wasomi wameiomba Mahakama Kuu amri hiyo pia ifungamane na Kesi ya Msingi namba 23/2016 ya kuhoji maamuzi ya Msajili kumtambua Lipumba kwa Nafasi ya Uenyekiti iliyopo mbele ya Jaji Kihijo ambayo kwa sasa imekatiwa Rufaa/maombi ya kufanyiwa Marejeo-REVISION mbele ya Mahakama ya Rufaa-Tanzania.
Mhe Jaji Dyansobela amekubaliana na Hoja zote hizo zilizowasilishwa kwa HATI YA DHARURA(UNDER CERTIFICATE OF URGENCY)  NA KUTOA AMRI YA KUZUIA FEDHA ZA SERIKALI KUTOLEWA KWA MASLAHI YA UMMA MPAKA HAPO MASHAURI YOTE YATAKAPOSIKILIZWA NA KUAMULIWA IPASAVYO.
Katika Hatua nyingine ili kuhakikisha kuwa masuala ya kesi yote yanasimamiwa na kushughulikiwa na kumalizwa kwa haraka Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad ameshakamilisha mazungumzo ya kuongeza nguvu zaidi za utetezi wa kisheria kwa kuwapata Mawakili Wasomi Maarufu sana nchini watano (5) ambao wataungana na kutengeneza jopo la Mawakili 9 watakaosimamia Kesi zote dhidi ya Lipumba na kundi lake.
CUF NI TAASISI IMARA, YENYE VIONGOZI MAKINI.
HAKI SAWA KWA WOTE
----------------------------------------------
MBARALA MAHARAGANDE
NAIBU MKURUGENZI WA HABARI, UENEZI
NA MAHUSIANO NA UMMA- CUF TAIFA
MAWASILIANO: 0784 001 408/0715 062577

MADIWANI DODOMA WAMFUNGIA MKURUGENZI OFISINI

KAMATI ya Uongozi, Mipango na Fedha ya Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Mpwapwa mkoani Dodoma, ilifunga Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Mohamed Maje ikidai ameshiNdwa kutekeleza maelekezo ya madiwani. 
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Dornart Nghwezi alisema Mkurugenzi huyo na timu yake wamekuwa hawatekelezi kwa wakati maelekezo ya Baraza hali inayosababisha kuwapo malumbano ya mara kwa mara yanayokwamisha maendeleo.