Saturday 26 July 2014

Meli ya zama na abiria 21 huko malaysia

Wahamiaji haramu kutoka Indonesia wanaendelea kufariki kutokana na ajali za majini kwenye mwambao wa Malacca.

Wahamiaji haramu kutoka Indonesia wanaendelea kufariki kutokana na ajali za majini kwenye mwambao wa Malacca.
Watu watatu wamefariki na wengine wanane hawajulikanai waliko baada ya meli waliyo kuwemo kuzama maji karibu na mwambao wa Malaysia, ambako meli tatu zilizama maji hivi karibuni.

Meli hiyo ilikua imesafirisha wahamiaji haramu kutoka indonesia, Shirika la habari linalomilikiwa na polisi ya majini ya Malaysia limearifu
“Miili ya watu watatu imeondolea ndani ya maji, watu 10 wameokolewa na wengine wanane hawajulikani waliko, baada ya meli hiyo kuzama, ajali ambayo ilitokea mapema alhamisi aubuhi wiki hii”, amesema Iskandar Ishak msimamizi wa shirika hilo la habari.
Meli hiyo iliyokua imesafirisha wahamiaji haramu 21, ambao walikua wakirejea nchini Indonesia kusheherekea Al Aïd el-Fitr, siku kuu ya kislamu ya kuhitimisha mfungo wa mwezi wa ramadhan, imezama maji katika bahari katika jimbo la Johor (kusini).
Iskandar Ishak, amesema kwamba uchunguzi wa kina umeanzishwa katika bahari hiyo, katikamwambao wa Malacca kulikotokea ajali hiyo ya meli.
Takribani watu 20 kutoka Indonesia wamefariki kutokana na ajali tatu mfululizo ziliyotokea katika bahari hiyo tangu mwishoni mwa mwezi Juni, na wengine zaidi ya ishirini wamepotea, kwa mujibu wa viongozi wa taifa hilo la kusini mashariki mwa Asia.

No comments: