Thursday 12 October 2017

MCHEZAJI WA ZAMANI WA CHELSEA NA AC MILAN GEORGE WEAH ASHINDA URAIS LIBERIA




Aliyekuwa mchezaji wa zamani wa Chelsea akitokea Ac Milani George Weah amefanikiwa kushinda nafasi  ya urais iliyoachwa wazi na aliyekuwa rais Mstaafu Eileen nchini Liberia kwa kuwabwanga washindani wenzake 19 waliokuwa wakiwania kiti hicho cha urais.

George Weah aliwahi kuchezea Monaco chini ya Kocha wa arsenal kwa sasa Arsene wenger mnamo mwaka 1988 , akajiunga na PSG mwaka 1992 baadae akajiunga na AC MILLAN mwaka 1995 baada ya hapo alijiunga na Chelsea na Man city kabla ya kwenda Klabu ya Marsel ya nchini Ufaransa , George weah alistaafu kucheza soka akiwa katika klabu ya Al-Jazira mnamo mwaka 2003, Mafanikio makubwa aliyoyapata akicheza soka katika vilabu hivi ni pamoja kubeba tuzo kubwa duniani ya Ballon d'Or na kuwa Mwafrika wa kwanza kubeba tuzo hiyo
Pia alifanikiwa kuchezea Timu ya taifa ya Liberia kwa mechi 70 , Mwaka  1989, 1994 na 1995, alitajwa kama Mchezaji bora wa mwaka wa Afrika (African Footballer of the Year), na mnamo mwaka 1996, alitatwa kuwa mchezaji bora wa karne wa Afrika ( African Player of the Century).
George Weah alijiingiza kwenye siasa na kufanikiwa kugombania nafasi kubwa ya kisiasa ( nafasi ya urais) kwa mara ya kwanza mwaka 2005 ambapo alibwagwa  na Ellen Johnson Sirleaf katika duru ya pili ya uchaguzi. Mwaka 2011 aligombania kama mgombea mwenza ( makamu wa rais) wa Winston Tubman's lakini hakufanikiwa , 2014 alifanikiwa kuchaguliwa kuwa seneta kupitia chama cha Congress for Democratic Change (CDC).

BOFYA HAPA KUONA GEORGE WEAH AKISAKATA KABUMBU

No comments: