Sunday 28 May 2017

Tetesi za Usajili Uingereza leo



Mshambuliaji wa Atletical Madrid aliyehusishwa kwa mda mrefu kuhamia Klabu ya Manchester United Antoine Griezman amewakatisha tamaa mashabiki wa man u baada ya kuandika katika akaunti yake ya twitter kuwa bado anafurahia kubaki A.Madrid na taarifa zinazomhusisha na kutaka kuhama ni za uongo zipuuzwe.

Mshambuliaji wa Chelsea na nchezaji wa timu ya taifa ya Ghana Christin Atsu aliyekwa akikipiga kwa Mkopo katika club ya Newcastle inayofundishwa na kocha wa zaman wa Mabingwa wa Uingereza kwa sasa Chelsea Rafael Benitez amekamilisha uhamisho wake wa moja kwa moja utakaombakisha katika kla
bu hiyo kwa ada ya uhamisho wa £6 million.

Manchester city wamewapiku jirani zao Manchester United kwa kumfanikisha kupata saini ya mchezaji wa Monaco Bernardo Silva kwa kiwango cha £43million . Huku klabu ya napoli ikifanikiwa kumbakiza mchezaji wake mahiri Dries Mertens ambaye mkataba wake ulikuwa unakaribia kufika kikomo , Dries Mertens ameingia mkataba mpya na klabu yake hadi 2022.
Mshambuliaji hatari wa Borussia Dortmund Aubameyang ameweka wazi kuwa anatamani kubadili mazingira na anatamani kufana kazi na klabu nyingine tofauti na Borussia Dortmund hata hivyo timu za ligi kuu nchini uingereza kama vile Chelsea zinamvizia mshambuliaji huyo hatari , chelsea chini ya meneja wake Conte inamwinda kinda huyo ili kuziba nafasi ya Diego Costa anaetimkia China msimu ujao na kuungana na wachezaji wenzake wa zaman kama Oscar , Ramirez na Dembaba.
Klabu ya Monaco ya nchini Ufaransa imeingia kwenye vita kali na klub ya newcastal katika kuwania saini   ya mshambuliaji wa Chelsea Michy Batshuayi.

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp anamtolea macho mchezaji wa kimataifa wa Ujermani na klabu ya Borussia Dortmund Mario Gotze ili kuziba pengo la mshambuliaji wake Philippe Coutinho
anaetazamiwa kujiunga na miamba wa soka nchini Uhispania Barcelona.

Katika hali ya sintofahamu wamiliki wa Arsenal juzi walikuwa wamemwahidi kocha wa Arsenal arsen wenger kuwa atapatiwa mkataba wa miaka miwili endapo watapata matokeo mazuri dhidi ya chelsea katika fainali ya kombe la FA , hata hivyo Wenger haku chezea bahati hiyo alifanikiwa kutwaa kombe la FA kwa kuwachapa Chelsea 2-1 , hivyo inatazamiwa wenger akaongezewa mkataba wa miaka miwili

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUKANUSHA TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI LILILOSAMBAA MITANDAONI.

Katika siku za hivi karibuni kumekuwepo na Tangazo la nafasi za kazi linalosambaa katika baadhi ya mitandao ya kijamii ikiwemo ''Facebook na WhatsApp'' likionyesha kwamba Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma imetoa tangazo la kazi lenye jumla ya nafasi wazi 188 kwa niaba ya waajiri mbalimbali Serikalini.

Watu hao mwenye nia ovu kwa makusudi wameamua kusambaza taarifa za uongo zenye kichwa cha Habari Tangazo la Nafasi za Kazi likiwataka watanzania wenye sifa na uwezo kutuma maombi ya kazi kwenye portal ya ajira kwa ajili ya kujaza nafasi hizo huku wakijua kuwa tangazo hilo sio la kweli kwa kuwa Serikali haijatangaza nafasi hizo hali ambayo imeleta usumbufu kwa jamii na wadau mbalimbali.

Saturday 27 May 2017

Njiwa ashikwa na mfuko wa 'uliojaa madawa ya kulevya'

Maafisa wa forodha nchini Kuwait wamemkamata njiwa aliyekuwa amebeba madawa ya kulevya katika mkoba mdogo mgongoni, gazeti la Kuwait, la al-Rai limeripoti.
Jumla ya tembe 178 ziliipatikana katika mfukop huo uliokuwa umepachikwa mgongoni mwake, gazezi hilo lilisema.
Ndege huyo alinaswa karibu na jumba la forodha jijini Abdali, karibu na mpaka wa nchi hiyo na Iraq.
Mwanahabari wa Al-Rai alisema kuwa madawa hayo ya kulevya yalikuwa aina ya ketamine, nusukaputi ambayo pia hutumiwa kama dawa haramu katika sherehe.
Abdullah Fahmi aliiambia BBC kwamba maafisa wa forodha walijua mbeleni kuwa njiwa walitumiwa kusafirisha madawa ya kulevya, lakini hii ilikuwa mara ya kwanza kunasa njiwa katika harakati hizo.

Thursday 18 May 2017

Kikwete ateuliwa kuwa mwenyekiti mwenza wa baraza la wakimbizi duniani

Aliyekuwa rais wa Tanzania Mh. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete ameteuliwa kuhudumu katika baraza kuu la wakimbizi duniani WRC, ambalo ni kundi huru la viongozi na wavumbuzi wanaolenga kubuni mbinu mpya za kutatua mizozo ya wakimbizi.
Kulingana na gazeti la The Citizen nchini Tanzania, taarifa kwa vyombo vya habari ilimtaja Bwana Kikwete kuwa mwenyekiti mwenza wa baraza hilo lililopo chini ya uenyekiti wa waziri wa maswala ya kigeni nchini Canada Lloyd Axworthy.

Wednesday 17 May 2017

Malima afikishwa kortini kwa kumshambulia askari

Aliyekuwa Naibu Waziri wa fedha na mbunge wa Mkuranga, Adam Kigoma Malima amefikishwa
mahakamani kujibu tuhuma za kumshambulia askari polisi. Malima anashtakiwa pamoja na dereva wake Ramadhani Mohamed Kigwande anayekabiliwa na tuhuma za kujeruhi. Washtakiwa wamesomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Respicious Mwijage wa
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.  Wakili wa serikali, Mwanaamina Kombakono amedai, Mei 15 mwaka huu huko Masaki katika wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam mshtakiwa Malima alitenda kosa.