Friday 31 July 2015

Mabaki ya ndege yaliyopatikana kweye ufukwe wa kisiwa cha Reunion katika Bahari ya Hind

Sehemu ya bawa ya ndege iliyopatikana ReunionMabaki ya ndege yaliyopatikana kweye ufukwe wa kisiwa cha Reunion katika Bahari ya Hindi siku ya Jumatano huwenda yakawa ni shemu ya bawa la ndege ya shirika la ndege la Malaysia Airlines iliyotoweka mwaka mmoja uliyopita kulingana na maafisa wa Malaysia na Australia.
Kugunduliwa kwa chombo hicho, ambacho kimethibitishwa na waatalamu kua ni kutoka ndege ya aina ya Boieng 777, imesababisha kuanzishwa uchunguzi mpya kutafuta ndege ya shirika la Malaysia MH370 iliyotoweka Marchi 8 2014, ilipokuwa safarini kutoka Kulalumpar kuelekea Bejing.

Thursday 30 July 2015

Wafuasi 3 wa CCM wajeruhiwa katika ugomvi wa kisiasa wilayani Rorya.

Watu watatu wamelazwa katika hospitali teule ya Shirati wilayani Rorya baada ya kujeruhiwa vibaya katika ugomvi ambao unadaiwa kuhusishwa na kampeni za kisiasa za wagombea wa ubunge wa chama cha mapindizikatika jimbo la Rorya mkoani Mara.
Mmoja wa majeruhi wa tukio hilo, amesema walishambuliwa na chupa huku wakitishiwa kukatwa mapanga muda mfupi baada ya kumalizika mkutano wa kampeni za CCM katika eneo hilo. 

Wasomi wa mpongeza Lowasa Kuhamia Chadema

Siku moja baada ya mbunge wa Monduli Edward Lowassa kujiunga na Chadema baadhi ya wasomi nchini wamempongeza kwa ujasili aliouonyesha.
Kabla ya kujiunga na Chadema, wadadi wa masuala ya siasa za Afrika wanasema ni Tanzania na Zimbabwe pekee ndizo zilizokuwa bado hazijatikishwa kisiasa, lakini kwa Tanzania Julai 28 bado itakumbukwa.

Azam yaigaragaza Yanga kwa mikwaju ya penati

AZAM FC jana ilimaliza ubabe wa Yanga katika michuano ya Kombe la Kagame baada ya kuibuka na ushindi wa penalti 5-4 katika mchezo wa robo fainali uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Timu hizo zilifikia hatua ya kupigiana penalti baada ya kutoka suluhu katika dakika 90 za kawaida za mchezo huo, uliokuwa wa vuta nikuvute katika kipindi chote.
Haji Mwinyi ndiye aliyeitia Yanga doa baada ya kukosa penalti ya tatu, huku Azam FC ikipata penalti zote tano. Waliofunga kwa upande wa Azam FC ni Kipre Tchetche, John Bocco, Humid Mao, Pascal Wawa na Aggrey Morris wakati walioifungia Yanga ni Salum Telela, Nadir Haroub na Godfrey Mwashiuya.
Haroub alikosa penalti katika mchezo dhidi ya Gor Mahia ya Kenya wakati Yanga ikilala 2-1, huku Simon Msuva na Amis Tambwe wakikosa penalti zao katika mchezo dhidi ya Telecom ya Djibouti, licha ya timu yao kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 katika hatua ya makundi.
Kwa ushindi huo, Azam FC sasa watakutana na KCCA katika mchezo wa nusu fainali utakaofanyika kwenye Uwanja wa Taifa kesho, huku Gor Mahia ikicheza dhidi ya Khartoum ya Sudan katika mchezo utakaotangulia wa nusu fainali.

Maradona amshtumiu Mkewe kumwibia

Diego Maradona aibiwa fedha
Nguli wa soka Duniani ,Diego Maradona amemtuhumu mke wake wa zamani Claudia Villafañe kwamba kumuibia kiasi cha fedha zipatazo dola milioni tisa, katika akaunti yake ya benki.
Akizungumza katika matangazo ya moja kwa moja ya Luninga,Maradonna amesema Villafañe ambaye alikuwa mpenzi wake wa zamani ni mwizi. Hata hivyo Villafañe amepinga vikali madai na kudai kuwa yeye si mwizi na hakuiba fedha hizo.

Wednesday 29 July 2015

Video Lowassa Akijibu kuhusu RICHMOND baada ya Kujiunga na UKAWA

Dakika chache baada ya kutangaza kutangaza kujiunga rasmi na UKAWA kupitia Chadema, waandishi wakamuuliza kuhusu Sakata la RICHMOND.... Sikia alivyojibu hapa kwenye hii Video:

Rais wa Nigeria akiri wakatayari kukabiliana na Boko Haram

Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari

Msemaji wa rais wa Nigeria,Muhammadu Buhari,amesema amejipanga kupambana na kundi la kigaidi la Boko Haram kama litaendesha mashambulizi yake katika mipaka ya kimataifa.
Msemaji huyo , Garba Shehu , aliiambia BBC kuwa tangu rais Buharia chaguliwe mwezi Mei amejipanga kutatua migogoro inayoikabili nchi hiyo tangu wananchi wa Nigeria wampa dhamana ya kuwaongoza.

Mapadri watatu na mtawa mmoja wafariki dunia katika ajali mbaya Missenyi

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Susan Kaganda.MAPADRI watatu na mtawa mmoja wa Kanisa Katoliki Jimbo la Rulenge wilayani Ngara walifariki dunia jana papo hapo huku watu 13 wakijeruhiwa katika ajali ya barabarani wakiwahi Karagwe kwenye misa ya shukrani ya mwenzao aliyepata daraja hilo hivi karibuni.
Tukio lingine ni la juzi ambapo watu saba walikufa na wengine 44 kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha basi na treni ya mizigo mkoani Tabora. Ajali hiyo ya juzi watu wanne walikufa papo hapo huku wengine wakifia njiani wakipelekwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tabora, Kitete.
Katika tukio la kwanza la Ngara, kwa mujibu wa mmoja wa mapadri waliokuwa katika msafara huo, Erasto Nakule, ajali hiyo ilitokea jana saa 2:00 asubuhi katika barabara iendayo nchi jirani ya Uganda katika eneo la Bugorora wilayani Missenyi mkoani Kagera.
Alisema gari aina ya Land Cruser lenye namba ya usajili T.650 BY1 la Jimbo Katoliki la Rulenge lililokuwa likiendeshwa na Padri Florian Tuombe ambaye pia amefia katika Hospitali ya Mkoa Kagera liligongana uso kwa uso na basi la Kampuni ya Sabuni lenye namna ya usajili T.166 AGU.

Tuesday 28 July 2015

Ajali ya Treni yaua wa 4 Tabora

Watu wanne wamefariki papo hapo na wengine zaidi ya arobaini kujeruhiwa baada ya Treini ya mizigo,kuligonga basi kampuni ya Don’t Worry lililokuwa likitokea mjiniTabora kuelekea ufuruma  uyui mkoani humo  lilipofika eneo la kuvuko cha reli eneo loa malolo manispaa ya Tabora katika kile kilichodaiwa kuwa ni uzembe wa dereva.
Mashuhuda wa ajali hiyo  wamesema kuwa, dereva aliyekuwa katika mwendo wa kasi alitaka kukatiza haraka bila kuzingatia eneo hilo inapopita Treini hata kama aliiona Treini hiyo, na ndipo alipokata kona ya ghafla na basi hilo kuanguka kwenye reli na Treini kuigonga na kukutoa paa lote la juu la gari.

Tatizo la mashine kutotambua alama za vidole limejitokeza katika baadhi ya vituo jijini DSM

Tatizo la mashine kutokutambua alama za vidole limejitokeza kwa baadhi ya vituo wakati zoezi la uandikishaji likiendelea jijini Dar es Salaam na kusababisha mashine kuzima zaidi ya mara sita huku tatizo la ubovu wa mashine na waandikishaji wasiokuwa na uzoefu likiendelea kulalamikiwa.
Licha ya kuwepo kwa malalamiko tangu siku ya kwanza ya zoezi hili kuanza hapa jijini lakini mamlaka husika zimeonekana kushindwa kuyatatua kwa wakati hali inayopelekea msongamano kwa baadhi ya vituo kutokupungua na watu kulazimika kuamka usiku wa manane kuwahi namba za uandikishwaji siku moja kabla.
 
TanzaniaOne blog imetembelea vituo mbalimbali na kushuhudia wananchi wakiwa wamejipumzisha vivulini na wengine wakichapa usingizi wakisubiri kuitwa majina huku kina mama wenye watoto wakilalamikia kutokupewa kipaumbele.
 
Baadhi ya waandikishaji waliozungumza na Ukomboz Blog wamedai kuwa tatizo la vidole vya baadhi ya wananchi kutokusoma kwenye mashine limekuwa likijitokeza mara kwa mara na kulazimika kutumia muda mwingi kuhudumia mtu mmoja hali inayozua kelele kwa watu waliopo kwenye foleni.
 
Kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi Temeke akizungumzia zoezi hilo amesema changamoto ambayo wamekuwa wakikabiliana nayo mara kwa mara ni watu kupiga simu vituoni hasa wanapoona wenzao hawafuati utaratibu na kuongeza kuwa hakuna aliyeshikiliwa kutokana na vurugu zinazojitokeza katika vituo hivyo.

Mbunge wa Viti maalumu Chadema atimkia ACT

Wakati vuguvugu la uchaguzi mkuu wa rais,wabunge na madiwani likiendelea kwa kasi mbunge wa viti maalum kwa tiketi ya chama cha demokrasi na mendeleo chadema Bi.Chiku Abwao amejitoa katika chama hicho na kujiunga rasmi na  chama cha ACT wazalendo.
Bi.Abwao amesema ameridhishwa na uongozi wa ACT-wazalendo, katiba na ilani ya uchaguzi wa chama hicho hadi kumpelekea kuamua kujiunga kwa vile kinalenga kumkomboa mtanzania masikini pamoja na kuweka msingi imara ya maadili ya viongozi.

Lowasa Kuzungumzia Swala la kuhamia ukawa Leo

Lowassa rasmi UkawaSASA ni rasmi kuwa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa anajiunga katika Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) na leo anatarajiwa kuzungumzia suala hilo, lililotanda katika siasa za Tanzania tangu baada ya kutopata nafasi ya kuteuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa mgombea wake wa urais.
Msemaji wake, Aboubakary Liongo alithibitisha jana jioni kuwa mbunge huyo wa Monduli, atazungumza saa 10 kamili jioni leo Dar es Salaam, kutoa kauli yake kuhusu mwaliko wa Ukawa, umoja ulioasisiwa wakati wa mchakato wa Bunge Maalumu la Katiba mwaka jana, ukimwalika ajiunge nao.
Liongo alieleza kuhusu mkutano huo wa leo, baada ya wakuu wa vyama vinavyounda Ukawa kuzungumza na waandishi wa habari kwenye Ofisi Kuu za Chama cha Wananchi (CUF), Buguruni, Dar es Salaam na kuchukua fursa hiyo kumwalika Lowassa kujiunga nao na kumsafishia njia ya kuwa mgombea wao wa urais.
“Tunachukua fursa hii kipekee kumwalika Waziri Mkuu mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mheshimiwa Edward Lowassa ajiunge na Ukawa na tuko tayari kushirikiana naye katika kuhakikisha tunaiondoa CCM madarakani katika Uchaguzi Mkuu ujao. “Tunaamini Mheshimiwa Lowassa ana uwezo wa kuhamasisha umma kuikataa CCM yenye kusimamia mifumo isiyotenda haki. Ni mchapakazi makini na mfuatiliaji wa karibu wa utendaji katika majukumu anayokabidhiwa,” alisema Mwenyekiti wa Taifa wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia ambaye pia ni Mwenyekiti mwenza wa Ukawa wakati akisoma taarifa ya Ukawa.

Watu Saba wanusurika kifo baada ya kula chakula chenye sumu mkoani Dodoma.

Watu saba wamenusurika kifo baada ya kula chakula kinachodaiwa kuwa na sumu kwenye tafrija ya maulidi ya kumtoa mtoto nje katika eneo la Nkuhungu manispaa ya Dodoma.
Watu hao mara baada ya kula chakula hicho ambacho kilikuwa ni kitoweo cha nyama ya mbuzi mikate na asali walianza kutapika mfululizo kabla ya wasamaria wema kuwakimbiza hosipitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma ambapo muuguzi mfawizi wa hosipitali hiyo Rehema Mghina akithibitisha kupokea watu hao huku akisema kuwa bado wako kwenye utafiti wa kitabibu ili kugundua wagonjwa hao wanasumbuliwa na tatizo gani.

Monday 27 July 2015

Kilichojiri Ukawa leo katika Mkutano wa waandishi wa Habari

UKAWA

Viongozi wa Vyama vinavyunda Umoja wa vyama vya Upinzani Tanzania (UKAWA) wakiwa katika Ofisi za Makao makuu ya Chama cha CUF, katika Mkutano na waandishi wa Habari mapema leo.


Na. Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Mwenyekiti mwenza, ndugu James Mbatia ndie alikuwa wa kwanza kuongea. Ni rai ya UKAWA kwa kila mtanzania ambae yuko tayari kuondoa mfumo kandamizi wa CCM kuungana nasi. Tunachukua fursa hii kumualika waziri mkuu mstaafu na mbunge wa Monduli kujiunga na UKAWA. Ni mchapakazi makini na mtekelezaji wa majukumu, UKAWA ndio tumaini la Tanzania, tusikubali kunyamaza pale ambapo sauti zetu zinazimwa kwa lazima. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki UKAWA, UKAWA ndio tumaini letu.

Lowasa ahamia Rasmi Ukawa, Sikiliza Audio akikaribishwa Ukawa

Waziri Mkuu Mstaafu wa JMT Mh. Edward Ngoyai Lowassa, akisalimiana na viongozi na wanachama wa CHADEMA

Waziri Mkuu Mstaafu wa JMT Mh. Edward Ngoyai Lowassa akiwa Meza Kuu na viogozi wa CHADEMA
http://www.audiomack.com/embed4/millardayocom/james-mbatia-kuhusu-ishu-ya-lowassa#embed

Siri nzito Ukawa , Vikao vya kaliwa hadi usiku wa manane

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe (kulia)
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe (kulia) akifurahia jambo na wajumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho walipohudhuria kikao cha dharura katika Hoteli ya Bahari Beach, jijini Dar es Salaam jana. kuanzia kushoto ni Ezekia Wenje, Mchungaji Peter Msigwa na Naibu Katibu wa chama hicho (Zanzibar), Salum Mwalimu.
Licha ya Baraza Kuu la Uongozi la Chama cha Wananchi (CUF) kupokea taarifa ya Ukawa na kuamua chama hicho kiendelee kushiriki katika umoja huo, bado suala la mgombea urais wa vyama vinavyounda umoja huo limeendelea kuwa siri nzito.
Taarifa zilizopatikana kutoka ndani ya CUF jana, zilisema kuwa katika kikao chake kilichoketi juzi na jana mjini Zanzibar, baraza hilo lilipokea taarifa ya Ukawa, kuithibitisha na kuamua chama hicho kiendelee na ushirikiano huo.
Mkutano wa waandishi wafutwa
Pamoja na hayo, jana kutwa nzima viongozi wa Ukawa walikuwa kwenye vikao mfululizo na hakukuwa na taarifa rasmi zilizopatikana na hata mkutano na waandishi wa habari ulioitishwa jana jioni uliahirishwa bila kueleza utaitishwa tena lini.
Ingawa taarifa ya mkutano wa Ukawa na wanahabari haikutaja ajenda, habari zilizoenea katika mitandao ya kijamii zilibainisha kuwa walikuwa wanakusudia ama kutangaza chama kilichopitishwa na Ukawa kusimamisha mgombea urais au kutangaza jina la mgombea mwenyewe pamoja na mgombea mwenza.
Vyanzo mbalimbali ndani ya Ukawa, vilieleza kuwa ufunguo wa hatua hiyo ulikuwa unashikiliwa na CUF, ambayo hivi karibuni ilijitenga na umoja huo ili masuala yake yajadiliwe kwanza na vikao vyake vya maamuzi kabla ya kurejea kwenye meza ya majadiliano.
Taarifa za uhakika kutoka katika kikao hicho kilichoketi Zanzibar kwa siku mbili, zilibainisha kuwa wajumbe waliafikiana kinyume na ilivyotarajiwa kuwa wangevurugana.
Miongoni mwa mambo ambayo inadaiwa wameafikiana ni kuwa mgombea urais atoke Chadema na chama hicho kitoe mgombea mwenza.
Jussa: Watanzania mtafurahi
Hata hivyo, mmoja wa wajumbe wa baraza hilo, Jussa Ismail Ladhu alipoulizwa alisema ikiwa itaamuliwa mgombea mwenza wa Ukawa atoke CUF, hakutakuwa na shida kwa kuwa chama hicho kina wanasiasa wazuri, safi na makini na kwamba kitatoa mtu ambaye Watanzania wote watafurahi.
“Ikiamuliwa kuwa mgombea mwenza atoke CUF, wananchi msiwe na wasiwasi, CUF ina hazina nyingi, itatoa mtu bora, itawapa chaguo ambalo Watanzania wote wataridhika nalo,” alisema Jussa.
Pamoja na kuthibitisha kuwa Baraza hilo limeamua CUF iendelee kushiriki katika umoja huo, Jussa alisema kwenye mjadala matatizo kidogo yalikuwapo katika mgawanyo wa majimbo.
Hata hivyo alisema baada ya kuweka vigezo vya kuwa na mgombea wa Ukawa, sasa hakuna shida kwa kuwa majimbo machache yaliyosalia utaratibu wake utatangazwa hivi karibuni.
Kuhusu mgombea mwenza, Jussa alisema CUF ina nafasi kubwa ya kutoa mgombea huyo kwa sababu ndicho chama chenye nguvu Zanzibar na kina wanasiasa mahiri na makini.
Wagombea wetu tunataka wawe ni wale watakaohakikisha kuwa Katiba Mpya inapatikana mara baada ya uchaguzi ili kuyaweka sawa mambo yanayohitaji kuwekwa sawa.
Hata hivyo, kwa mujibu wa Katiba, mgombea urais na mgombea mwenza wanapaswa kutoka chama kimoja, hivyo kama Chadema itamtoa mgombea urais inabidi pia mgombea mwenza atoke chama hicho.
Habari ambazo bado si rasmi zinasema kuwa mmoja wa viongozi wa CUF anaweza kuhamia Chadema ili kukidhi matakwa hayo ya Katiba.
Mkurugenzi wa Haki za Binadamu, Habari, Uenezi na Mawasiliano ya Umma wa CUF, Salim Bimani alisema kuwa mambo katika Ukawa ni mazuri, wapo waliofikiri kuwa watavurugana, lakini wamekubaliana na sasa Watanzania wasubiri kupata wagombea safi katika ngazi zote.
Bimani alisema CUF kitaendelea kushirikiana na vyama vingine vya upinzani nchini ili kuhakikisha demokrasia inazidi kukua.

Yanga yaongeza nguvu kumsajili Michael Olunga

Yanga yaongeza nguvu kumsajili Michael OlungaMbali na Olunga Yanga pia wanamwania kiungo wa mabingwa hao wa Kenya Khalid Auch, ili kuimarisha safu yao ya kiungo mkabaji
KLABU ya Yanga imeongeza nguvu za kumsajili mshambuliaji wa Gor Mahia ya Kenya Michael Olunga, ili kuziba nafasi ya Mliberia Kpah Sherman, anayetarajiwa kujiunga na timu ya Mpumalanga Black Aces inayoshiriki Ligi Kuu nchini Afrika Kusini.
Uongozi wa Yanga kupitia kwa katibu wake Mkuu Dr Joans Tiboroha amesema wanatarajia kuanza mazungumzo na viongozi wa Gor kuangalia uwezekano wa kumpata mshambuliaji huyo ambaye ameonyesha uwezo mkubwa kwnenye michuano ya Kgame inayoendelea Dar es Salaam Tanzania.
“Olunga ni mchezaji mzuri kila mtu analijua hilo na kwakua Sherman wakati wowote ataondoka tumeona yeye ndiyo mtu sahihi wa kuziba nafasi yake kwenye kikosi chetu kusaidiana na Donald Ngoma Amissi Tambwe na Malimi Busungu,”amesema Tiboroha.
Mbali na Olunga Yanga pia wanamwania kiungo wa mabingwa hao wa Kenya Khalid Auch, ili kuimarisha safu yao ya kiungo mkabaji baada ya Mbuyu Twite kuonekana kuchoka kutokana na umri mkubwa aliokuwa nao huku pia klabu yake ya zamani FC Lupopo kuonekana kuisumbua Yanga kutokana na usajili wake.

Obama Awasili Ethiopia

Rais Obama akishuka kutoka ndani ya ndege ya Rais
Rais Barack Obama wa Marekani hatimaye amefika nchini Ethiopia katika ziara yake ya pili ya nchi za Afrika.
Ni mara yake ya kwanza tangu aongoze taifa la Marekani akiwa raisi kuhutubia wanachama hamsini na mbili wa umoja wa Afrika katika makao makuu yake yaliyoko Addis ababa.Mazungumzo yao yakiwa yamelenga kutafuta suluhu ya kutokomeza migogoro ya vita za wenyewe kwa wenyewe sudan ya kusini.
Raisi Obama,aliwasili nchini Ethiopia akiwa anatokea mjini Nairobi ambako aliwaambia wakenya kuwa amna kikomo cha kile wanachokihitaji na kusisitiza kwa kutoa angalizo katika athari za ukabila na rushwa. Tamaduni mbaya kama unyanyasaji wa kijinsia,ndoa za kulazimishwa ,tohara kwa watoto wa kike na kutopeleka watoto shuleni.

Sunday 26 July 2015

Wiki ya mtikisiko

Mwenekiti wa Chadema Freeman Mbowe akiwahutubiaNi wiki ya mtikisiko. Hivi ndiyo unavyoweza kuelezea hali itakavyokuwa nchini kutokana na matukio makubwa ya kisiasa yanayotazamiwa kutokea ndani ya wiki inayoanza leo ambayo yanaweza kubadili mwelekeo wa siasa za Tanzania.
Hali hiyo inatokana na vuguvugu la kisiasa linalohusisha viongozi wenye ushawishi kuhama vyama vyao vya siasa na kutimkia kwenye vyama vingine, ikiwa ni siku chache kabla ya kufanyika Uchaguzi Mkuu Oktoba 25, mwaka huu.
Ni wiki ambayo itapambwa na matokeo ya kikao cha Baraza Kuu la Uongozi wa CUF kilichofanyika jana mjini Zanzibar kuhusu mustakabali wake ndani ya Ukawa, ikizingatiwa kuwa hivi karibuni chama hicho kiliamua kujiweka kando ya vikao vya umoja huo hadi vikao vya juu viamue.
Hata hivyo, habari ambazo gazeti hili limezipata zinasema kuwa uwezekano wa chama hicho kujitoa ndani ya Ukawa ulikuwa mdogo kutokana na kuogopa hasira za wananchi wenye matumaini na umoja huo.
Aidha, kulikuwa na taarifa kuwa kikao cha jana kilikuwa kinaangalia jinsi watakavyoshiriki katika umoja huo na kwamba kulikuwa na matumaini makubwa.

Azam ngoma inogile watoa dozi kwa Adama City

Wachezaji wa Azam FC wakipongezana baada ya Kipre Tchetche kuipatia timu yao bao la pili
Wachezaji wa Azam FC wakipongezana baada ya Kipre Tchetche kuipatia timu yao bao la pili

Timu ya Azam FC ‘wanalambalamba’ leo wametoa dozi ya magoli 5-0 kwa Adama City FC ya Ethiopia kwenye mashindano ya Kagame Cup ambayo yanazidi kuchanja mbuga jijini Dar es Samaa mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Taifa.

Simba ina wakali watano wapya

wachezaji wa Simba wakiwa kwenye mazoezi
SIMBA ina malengo mengi ya kuyatekeleza katka msimu mpya wa Ligi Kuu Bara, lakini kubwa zaidi ni usajili hasa wachezaji wa kigeni ambapo imeweka majina ya wachezaji watano mezani ambao wapo kwenye mpango huku ikiwa na nafasi tatu za wazi kwa wachezaji wa aina hiyo.
Simba ina wachezaji wageni wanne ambao wana uhakika nao tayari, hao ni  Simon Sserunkuma, Hamisi Kiiza na Juuko Murshid ambao wote ni raia wa Uganda.Pia inatarajia kumalizana na Laudit Mavugo raia wa Burundi.

Rais Kikwete ateua Mkurugenzi mpya wa Uchaguzi

Rais Jakaya Kikwete akimwapisha Mkurugenzi wa Uchaguzi, Kailima Ramadhani Kombwey (kulia) Ikulu Dar es Salaam jana. Mwingine ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue
RAIS Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko ya utendaji katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kwa kumteua aliyekuwa Mkurugenzi wa Utawala wa Tume hiyo, Kailima Kombwey kuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi.
Kwa mujibu wa taarifa ya Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, Kombwey ambaye aliapishwa jana jioni, anachukua nafasi ya aliyekuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi, Julius Mallaba, ambaye ameteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania.
Rais Kikwete pia amemteua Jaji Richard Mziray, kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na majaji wengine wapya 13 wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

Vigogo wa CCM wang'olewa Ubunge wa Viti maalum

BAADHI ya vigogo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Serikali, waliokuwa wakiwania nafasi ya kuteuliwa kuwa wabunge wa viti maalumu baada ya kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu ujao, wamejikuta wakishindwa katika kura za maoni.
Kura hizo zilizopigwa juzi na wajumbe wa mkutano wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) ngazi za mikoa yote nchini, isipokuwa Mkoa wa Dar es Salaam, mbali na kuangusha baadhi ya vigogo, pia zimeibua majina mapya na kuwapa nafasi za juu, zitakazowapa fursa ya kuteuliwa kuwa wabunge wa Viti Maalumu na hata pengine uwaziri. Washindi wawili wa juu katika kura hizo katika kila mkoa, ndio walio na nafasi ya kuteuliwa kuwa wabunge wa viti maalumu, huku wa kwanza akiwa na nafasi nzuri zaidi, baada ya kupatikana kwa kura za mgombea urais wa CCM.
Miongoni mwa vigogo walioangushwa, yupo Waziri wa zamani wa Maliasili na Utalii, Shamsha Mwangunga, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, Dk Pindi Chana na viongozi wa mikoa wa UWT, wakuu wa wilaya na wabunge kadhaa wa Viti Maalumu wanaomaliza muda wao.
Mkoa wa Njombe

Saturday 25 July 2015

Marekani yakosoa Uchaguzi wa Burundi

Nkurunziza
Waziri wa masuala ya Nje wa Marekani John Kerry amekashifu matokeo ya uchaguzi ya Burundi yaliyotolewa hapo jana ambapo rais Pierre Nkurunziza alitangazwa kusajili ushindi mkubwa.
Kerry ametaja uchaguzi huo kuwa ukiukaji mkubwa wa katiba na kejeli kwa mfumo wa haki huku akimlaumu rais Pierre Nkurunziza kwa ghasia zilizotokea nchini humo wiki chache kabla ya kufanyika uchaguzi.

Obama kuhutubia kongamano la wajasiria mali kenya leo

Rais Barack Obama alipowasili Kenya hapo jana
Rais wa marekani Barack anatarajiwa kuhutubia kongamano la wajasiriamali akianza rasmi ziara yake katika eneo la afrika masharaki.
Anatarajiwa kuzungumzia suala la ufisadi ambapo atataka kuwepo kwa jitihada kubwa za kupambana na ufisadi na pia kuwahutubia wafanyibiahara vijana nchini Kenya.

Yanga kwa raha zao watinga robo fainali kagame Cup

Deus Kaseke akiwatoka wachezaji wa KMKM
YANGA jana ilitinga robo fainali ya Kombe la Kagame baada ya kupata ushindi wa pili mfululizo kwa kuizamisha KMKM ya Zanzibar kwa mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Ushindi huo umewafanya mabingwa hao wa Tanzania Bara kufikisha pointi sita, pointi moja nyuma ya timu mbili za Al Khartoum ya Jamhuri ya Sudan na Gor Mahia ya Kenya zinazoongoza Kundi A.
Yanga ilianza kwa kufungwa mabao 2-1 na Gor Mahia wiki moja iliyopita, lakini Jumatano wiki hii ilizinduka na kuichapa Telecom ya Djibouti mabao 3-0, na hivyo kufufua matumaini ya kusonga mbele.
Kwa matokeo ya jana, Al Khartoum na Gor Mahia ambazo zilitoka sare ya bao 1-1 katika mechi ya kwanza jana kwenye uwanja huo, zinaungana na Yanga kucheza robo fainali wakati KMKM imetupwa nje sawa na Telecom.

Obama awasili Kenya kwa Kishindo kikubwa

Rais wa Marekani, Barack Obama amewasili nchini Kenya, huku kukiwa na ulinzi mkali sana, ikiwa ni mwanzo wa ziara ya siku mbili nchini humo.
Rais Obama alilakiwa na mwenyeji wake Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya. Rais wa Marekani aliepeana mikoni na viongozi wengine wa Kenya na kutia sain kitabu maalum cha wageni kabla ya kupanda kwenye gari yake.
Mitaa ya Nairobi ilikuwa imepakawa rangi na kusafishwa,  mji ulitumia kila ilichokuwa nacho kwa ajili ya kumkaribisha  Obama kwa kile ambacho wakenya wamekiita “kurejea nyumbani.”

Wadau wataka tume ya uchaguzi kuongeza mudawauandikishaji wapiga kura Dar es Salaam

Kutokana na zoezi la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa kutumia mfumo wa BVR mkoa wa Dar es Salaam kugubikwa na matatizo lukuki vyama vya siasa na wadau wa siasa wameitaka tume kuongeza mida pamoka na kuhakikisha kila kituo kina kuwa na mtaalamu wa komputa.
Zoezi hili likiwa limeingia siku ya tatatu jijini hapa huku idadi kubwa ya watu wakiwa hawajaandikishwa kwa madai ya ubovu wa mashine na waandikishaji ambao siyo wataalamu kumepelekea vyama hivyo vya siasa na wadau kuzungunzia hali hiyo kama wanavyoelezea.

Friday 24 July 2015

10 wafariki, 55 wajeruhiwa kwenye ajali ya basi iliyotokea Dodoma

Ajali ya basi yatokea nchini Tanzania10 wafariki, 55 wajeruhiwa kwenye ajali ya basi iliyotokea karibu na mji mkuu wa Tanzania

Watu 10 wameripotiwa kupoteza maisha na wengine 55 kujeruhiwa baada ya basi moja kupoteza mwelekeo na kugonga mti katika eneo la Chamwino lililoko karibu na mji mkuu wa Dodoma nchini Tanzania.
Kamanda wa polisi wa eneo la Dodoma David Mnyambugha, alitoa maelezo na kusema kwamba ajali hiyo ilitokea nyakati za jioni wakati basi hilo lilipokuwa likisafiri kutoka Shinyanga kuelekea Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa maelezo ya Mnyambugha, basi hilo lilipoteza mwelekeo na kugonga mti na kusababisha abiria 8 kupoteza maisha papo hapo.

Atletico Madrid yamsajili Mghana

Atletico Madrid yamsajili nyota wa GhanaBernard Mensah atia saini mkataba wa miaka 6 na kilabu ya Atletico Madrid

Kilabu ya Atletico Madrid kutoka Uhispania imemsajili kiungo wa kati wa Ghana Bernard Mensah kutoka kilabu ya Vitoria Guimaraes.
Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa mtandaoni kupitia tovuti rasmi ya Atletico Madrid, Mensah alitia saini mkataba wa miaka 6 baada ya makubaliano ya usajili.

SZCZESNY kuondoka Arsenal


huyooo Roma....
huyooo Roma….
Golikipa wa Arsenal, Wojciech Szczesny, 25, anaondoka klabuni hapo kujiunga na Roma kwa mkataba wa mkopo wa mwaka mmoja.
Szczesny aliruhusiwa na Arsenal kufanya mazungumzo na Roma juu ya maslahi yake, kwani tayari wanaye Petr Cech aliyesajiliwa kutoka Chelsea na David Ospina aliyempoka Szczesny namba yake katikati ya msimu uliopita.

Man City kuvunja benki kumsajili Kevin de Bruyne

Manchester City wanajiandaa ‘kuvunja benki’ kumnasa kiungo mshambuliaji wa Wolfsburg, Kevin de Bruyne, 24.
Mchezaji huyo ameshawaambia klabuni kwamba anataka kuondoka kwenda kucheza Etihad. Matajiri hao wa England wanaingiza dau hilo kubwa baada ya wiki jana tu kumnasa mshambuliaji wa Liverpool, Raheem Sterling kwa pauni milioni 49.
City wanaaminika kuanza na ofa ya pauni milioni 40 lakini inavyoonekana watapanda hadi pauni milioni 60 kumnasa mchezaji ambaye Chelsea waliachana naye wakisema hana kiwango, wakamuuza kwa pauni milioni 18.

Bulaya: Niliukataa Uwaziri ili kutetea maslahi ya watanzania

Mchuano mwingine mkali unatarajiwa kuwapo
Mchuano mwingine mkali unatarajiwa kuwapo katika Jimbo la Bunda Mjini ambako Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira atavaana na Mbunge wa Viti Maalumu, Ester Bulaya
Mbunge wa Viti Maalum alihama juzi CCM na kujiunga Chadema, Ester Bulaya amesema licha ya kuahidiwa vyeo vingi ukiwamo uwaziri na ukuu wa wilaya ili asihame CCM, aliamua kuviacha ili aweze kuwasaidia Watanzania wa chini ambao wameonewa na serikali ya chama hicho kwa miaka 50 iliyopita.
Akihutubia katika mkutano wa hadhara uliofanyikia katika Viwanja vya Stendi ya zamani mjini Bunda jana, Bulaya alisema wakati chama chake cha zamani kilipogundua mikakati yake ya kuhamia Chadema, makada wake walimwendea wakimsihi asitoke, bali abakie ili apatiwe ukuu wa wilaya au uwaziri.

Auawa na wananchi wenye hasira kali baada ya kuwachoma kisu abiria kwenye daladala

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, CamiliusMtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Mosha Mahona ameuawa na wananchi baada ya kuwachoma kwa kisu abiria watano waliokuwa kwenye daladala linalofanya safari zake kati ya Posta na Ubungo Simu 2000.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camilius Wambura alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea juzi saa moja usiku katika eneo la Magomeni Usalama na Mahona aliuawa kwa kushambuliwa na wananchi baada ya kudhuru abiria wenzake.

January Makamba afunguka baada ya kukatwa Jina lake

ALIYEKUWA mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) January Makamba, amefunguka na kuwataka wananchi wasife moyo kwa yeye kuishia nafasi ya tano kwa vile muda bado upo na kwamba hivi sasa wafanye kampeni za kufa mtu ili John Magufuli aliyechaguliwa na chama hicho aweze kushinda na kuingia Ikulu.

Akizungumza kwenye mkutano maalum wa Umoja wa Wanawake wa CCM wilayani hapa, ulioitishwa kwa ajili ya kuchagua madiwani wa viti maalum, Makamba aliyeomba tena kuchaguliwa kuwa mbunge katika jimbo la Bumbuli, alisema kwamba anawashukuru wote waliokuwa wakimuunga mkono hadi kufikia nafasi hiyo ambayo haikuwa yake, bali ni ya wananchi wa Lushoto waliomlea na Watanzania wote.

Vidal kutua Bayern Munich ya Ujerumani


Vidal kuelekea Bayern MunichBayern Munich yatangaza kuafikiana na Juventus kwa ajili ya usajili wa Vidal

Kiongozi wa kilabu ya Bayern Munich nchini Ujerumani Karl-Heinz Rummenigge, ametangaza kufanya makubaliano na kilabu ya Juventus kwa ajili ya usajili wa kiungo wa kati Arturo Vidal.
Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa mtandaoni kupitia tovuti rasmi ya Bayern Munich, Rummenigge alithibitisha kuafikiana na Juventus pamoja na Vidal kuhusu usajili wake

Chupi za zua kizaazaa bungeni

Chupi zazua kihoha Bungeni
Mbunge mmoja nchini Zimbabwe alizua kizaazaa bungeni pale alitumia chupi za kina mama kusisitiza hatma ya raia masikini wa nchini hiyo ambao hawana uwezo wa kununua chupi mpya.
Katika kikao kilichokua kikipeperusha moja kwa moja kwenye runinga ya taifa, Priscilla Misihairabwi-Mushonga, wa chama cha upinzani cha Movement for Democratic Change (MDC), alitoa karatasi ya plastiki iliyokuwa na chupi hiyo. Kisha akamuuliza waziri wa fedha na sera za serikali kuhusiana na uagizwaji wa chupi kukuu ambayo anasema ni ya bei nafuu na zinasababisha madhara makubwa kwa afya ya kina mama.
''Bwana spika hebu tazama hizi chupi ninazo hapa, hizi ni mpya na hugharimu dola mbili kila moja.''

Mbunge huyo Misihairabwi-Mushonga baadaye alitimuliwa bungeni baada ya kumkabili vikali mbunge wa chama tawala cha ZANU-PF
''Hizi zilizoko mkono wangu wa kushoto ni mitumba na hugharimu dola moja kwa chupi mbili. alisema mbunge huyo
Akijibu swali hilo waziri wa fedha Patrick Chinamasa alimtania mbunge huyo Misihairabwi-Mushonga kutokana na uamuzi wake wa kubeba chupi hizo bungeni lakini amesema wizara yake inachunguza suala hilo. ''Bwana Spika, kabla sijajibu swahili hilo, naamini mheshimiwa mbunge hangelifanya kitendo kama hicho kusisitiza hoja yake'' alisema waziri huyo wa fedha.

Uchumi wa Zimbabwe umedorora kwa miaka kadhaa iliyopita
Chinamasa amesema atalishughulikia suala hilo wiki ijayo wakati atakapotoa taarifa rasmi ya serikali kuhusuiana na sera zake za kiuchumi.

Thursday 23 July 2015

Yanga yaona mwanga Katika Michuano ya Kagame

MABINGWA wa Tanzania Bara Yanga, jana walizinduka katika michuano ya Kombe la Kagame baada ya kuifunga Telecom ya Djibout kwa mabao 3-0 katika mchezo wa Kundi A uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Yanga iliyoanza vibaya mechi za Kundi A kwa kufungwa 2-1 na Gor Mahia ya Kenya, sasa inaweza kwenda robo fainali iwapo itashinda mechi zijazo dhidi ya KMKM na Khartoum N ya Sudan.
Katika mchezo huo, uliochezeshwa na mwamuzi Issa Kagabo wa Rwanda aliyesaidiwa na Lee Okello wa Uganda na Yeatyew Belachew wa Ethiopia, mabao ya Yanga yalifungwa na wachezaji waliosajiliwa mwaka huu na hadi mapumziko walikuwa mbele kwa bao 1-0.

Bunge la Ugiriki lapitisha awamu ya pili ya mageuzi

Waziri mkuu Alexis Tsipras hakuwa na njia nyingje ispokua kuwashawishi wabunge wa Ugiriki kupigia kura mfuko wa pili wa hatua kali za malipo ziliyotolewa na wakopeshaji.
Waziri mkuu Alexis Tsipras hakuwa na njia nyingje ispokua kuwashawishi wabunge wa Ugiriki kupigia kura mfuko wa pili wa hatua kali za malipo ziliyotolewa na wakopeshaji.
Usiku wa Jumatano kuamkia Alhamisi wiki hii, Bunge la Ugiriki limepitisha mfuko awamu ya pili ya hatua zilizodaiwa na wakopeshaji. Mageuzi haya yanahusu sheria za kijamii na mabenki.

Mageuzi haya ni sehemu ya masharti ya mwendelezo wa mazungumzo kwa ajili ya mpango wa tatu wa msaada.
Kwa kura 230 za ndio kwa jumla ya kura 300, serikali ya Alexis Tsipras ilibidi tena kutegemea sauti za upinzani za vyama vya Conservative (New Democracy), Kisoshalisti cha Pasok na chama cha mrengo wa kati cha To Potami.

Benteke atua rasmi Liverpool

Timu ya livepool imekamilisha kumsajili rasmi mshambuliaji mwenye asili ya Jamuhuri ya Kidemokrasia wa kongo Christian Benteke kutoka Aston Villa kwa kitita paundi milion 32.5.
Benteke alikubali mkataba wa muda mrefu na kuwa mchezaji wa pili kununuliwa kwa gharama kubwa huko England.

Wednesday 22 July 2015

Wabunge toka chadema wamkaribisha Lowasa kwa Mikono yote

Baadhi ya wabunge wa Chadema wamezungumzia taarifa zinazosambaa zikieleza kuwapo mkakati wa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kuhamia katika chama hicho, wengi wao wakimkaribisha.

Wakati wabunge hao wakikubali kumpokea, Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa amesema wananchi wasubiri mambo yatakapokuwa tayari badala ya kutegemea mitandao ya kijamii.

“Nitazungumza pale mambo yatakapokuwa sawa, siwezi kuzungumza sasa, subirini… sasa hivi mambo mengi yanazungumzwa kwenye mitandao,” alisema Dk Slaa ambaye pia anatajwa kuwa mgombea wa chama hicho ndani ya Ukawa.

Msemaji wa Lowassa, Aboubakary Liongo alipoulizwa kuhusu kuwapo kwa mpango huo alisema hawezi kulizungumzia hilo kwa kuwa ni suala la mtu binafsi. Hata hivyo, jitihada za kumpata Lowassa jana hazikufanikiwa kwani simu yake iliita pasi na kupokewa.

Sitti Mtemvu na Dada yake Hapatoshi Ubunge Viti Maalumu Morogoro

Dustan Shekidele, Morogoro
HAPATOSHI! Vita kali ya kugombea ubunge imezuka katika familia ya Mbunge wa Temeke Abbas Mtemvu kufuatia watoto wake wawili, Lulu na Sitti Abbasi Mtemvu ambao kwa pamoja wamechukua fomu ya kugombea ubunge viti maalum kupitia kundi la umoja wa Vijana (UVCCM) Mkoa wa Morogoro.

Kiongozi wa Al-Quaeda auawa

Muhsin al-Fadhli
Jeshi la Marekani linasema kuwa mmoja viongozi wa kundi la kigaidi la al-Qaeda, ameuwaua katika shambulio la angani lililotekelezwa na ndege za kijeshi za Marekani Nchini Syria.
Idara ya ulinzi ya Pentagon imesema kuwa Muhsin al-Fadhli, alikuwa kinara wa kundi la Khorasan, lililotumwa na al-Qaeda, kutoka Pakistan hadi nchini Syria.

Lowasa Huyooooo njian kuelekea Chadema

http://mzalendo.net/wp-content/uploads/2015/07/11760299_753973754710974_4205268567101047013_n.pngDar es Salaam. Baadhi ya wabunge wa Chadema wamezungumzia taarifa zinazosambaa zikieleza kuwapo mkakati wa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kuhamia katika chama hicho, wengi wao wakimkaribisha.
Wakati wabunge hao wakikubali kumpokea, Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa amesema wananchi wasubiri mambo yatakapokuwa tayari badala ya kutegemea mitandao ya kijamii.
“Nitazungumza pale mambo yatakapokuwa sawa, siwezi kuzungumza sasa, subirini… sasa hivi mambo mengi yanazungumzwa kwenye mitandao,” alisema Dk Slaa ambaye pia anatajwa kuwa mgombea wa chama hicho ndani ya Ukawa.
Msemaji wa Lowassa, Aboubakary Liongo alipoulizwa kuhusu kuwapo kwa mpango huo alisema hawezi kulizungumzia hilo kwa kuwa ni suala la mtu binafsi. Hata hivyo, jitihada za kumpata Lowassa jana hazikufanikiwa kwani simu yake iliita pasi na kupokewa.

Wednesday 15 July 2015

Aliyekamatwa na milion 700 Dodoma arudishiwa pesa zake, polisi wasema alikwenda Dodoma kununua nafaka

Aliyekamatwa na milion 700 Dodoma arudishiwa pesa zake, polisi yasema alikwenda Dodoma kununua nafaka
Jeshi la polisi mkoani Dodoma limekanusha taarifa zilizozagaa kuhusiana na Raia wa Asia kukamtwa na fedha zaidi ya sh. m.700 kwa madai ya kuwahonga wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM ili wamchague mmoja kati ya waliokuwa wanawania nafasi ya Urais
Polisi imesema kuwa uchunguzi uliofanywa na jeshi la polisi umebaini kuwa hakuna kosa la jinai lililothibitika licha ya kukutwa na kiasi hicho cha fedha, tuhuma za rushwa ambazo ndiyo zilikuwa msingi wa ukamataji wa mtu huyo hazikuthibitika, kwa kuwa hakuna aliyeona akizigawa fedha hizo wala hakuna aliyedai kushawishiwa au kugawiwa fedha hizo.

Askofu mstaafu Desmond Tutu amelazwa katika hospitali moja mjini Cape Town Afrika Kusini.

Askofu mstaafu Desmond Tutu amelazwa katika hospitali moja mjini Cape Town Afrika Kusini.
Familia yake inasema kuwa amekuwa akiugua maambukizi yasioisha na kwamba huenda akatoka hospitalini hivi karibuni.
Bwana Tutu alijiuzulu katika maisha ya umma miaka minne iliopita lakini anaendelea kusafiri maeneo mengi.
Amelazwa hosptalini mara kadhaa katika miaka ya hivi karibuni na kutibiwa saratani ya tezi dume kwa mara kadhaa.

Tuesday 14 July 2015

:Iran yakubaliana na mataifa 6 makubwa kuhusu nyuklia

Makubaliano yameafikiwa baina ya Iran na mataifa sita yenye nguvu duniani
Baada ya mazungumzo ya miezi kadhaa makubaliano ya kihistoria yametangazwa kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran na mataifa 6 makubwa duniani.
Mawaziri wa mambo ya nje kutoka Iran na mataifa sita zenye nguvu duniani wanakutana kwa mara ya mwisho huko Vienna baada ya makubaliano rasmi kutatangazwa katika mkutano na waandishi habari.
Balozi Federica Mogherini, alipotangaza mapatano hayo
Balozi wa maswala ya kigeni wa bara Ulaya Federica Mogherini, amechapisha mwenye mtandao wake wa kijamii wa Twitter kuwa makubaliano kuhusiana na mradi wa kinyunklia wa Iran yameafikiwa.
Bi Mogherini amesema kuwa ni wazi mazungumzo ya kidiplomasia yanaweza kuleta mabadiliko makubwa ya sera kushinda makabiliano ya kijeshi ya miongo kadhaa.
Rais wa Iran , Hassan Rouhani, amesema kuwa majadiliano hayo yamekuwa na ufanisi mkubwa