Wednesday 27 September 2017

Zanzibar na Uingereza ndio nchi pekee zilizopogana vita kwa muda Mfupi , dakika 40

Unaambiwa ukishangaa ya Musa utaona ya firauni, na siku hizi watu wanasema akili za mtu anazijua mwenyewe. Ili kudhibitisha hayo najaribu kukuletea simulizi hizi za kweli zilizotokea nyakati tofauti tofauti katika uso wa dunia. Siku zote migogoro huwa inatokea katika maisha ya binadamu na kunakuwa na sababu za kimasilahi kusababisha migogoro hio, wakati mwingine kumekua na migogoro ambayo mantiki za kimasilahi hazionekani, nakusababisha watu au pande mbili kwenda mbali Zaidi kiasi cha kutanagaza vita. Zifutazo ni vita vilivyo wahi kutokea kayika historia ya dunia na kuonekana za ajabu sana kulingana na sababu, muda au mbinu zilizotimika.

Wednesday 6 September 2017

Manji avuliwa udiwani baada ya kushindwa kuhudhuria vikao

Aliyekuwa mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Yusuf Manji amevuliwa nafasi ya udiwani wa kata ya Mbagala Kuu baada ya kushindwa kuhudhuria vikao kutokana na kukabiliwa na kesi Mahakama ya Kisutu.

Watoto wawili kati ya wanne waliokuwa wametekwa wapatikana wakiwa wamekufa

Wananchi wakishuhudia zoezi la uopoaji wa miili ya watoto wawili

ARUSHA: ​ Watoto wawili  Ikram na Maureen waliokuwa wametekwa wamepatikana katika shimo la choo ambalo bado halijaanza kutumika. Muda huu askari ndio wanafanya utaratibu wa kuwatoa.

Chanzo cha uhakika kinasema mtekaji aliwatumbukiza ndani ya shimo hilo wakiwa hai kabla ya kuondoka na kuelekea Geita kabla ya kukamatwa na kusema walipo watoto hao.

Mwanafunzi awekewa sh. bilioni 2.2 na bodi ya mikopo kimakosa

Eastern Cape, Afrika Kusini. Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Walter Sisulu alilala masikini na kuamka tajiri baada ya kukuta akaunti yake ikiwa na Dola 1 milioni za Marekani sawa na Sh2.2 bilioni kutoka katika bodi ya mikopo ya wanafunzi.

Alijiona mwenye bahati na kuanza kuzitumbua, asijue kumbe alikuwa akichochea kugundulika haraka kwa kuwa ndani ya wiki mbili kitumbua chake kiliingia mchanga.

Viongozi wanne wa CUF wanaomuunga mkono prof .LIPUMBA wamefariki kwenye ajali wakitokea Dodoma

Viongozi wanne wa Chama cha Wananchi CUF wanaomuunga mkono Profesa Ibrahim Lipumba wamefariki dunia baada ya msafara wao kupata ajali maeneo ya Ubenazomozi Mkoa wa Pwani.

Ajali hiyo imetokea jana usiku wakati Viongozi hao wakitokea Dodoma kwenye sherehe za kuapishwa kwa Wabunge wapya wa Chama hicho.