Tuesday 29 December 2015

Arsenal yapaa kileleni

Washika bunduki wa London, Arsenal wamekaa kileleni mwa ligi ya England kwa pointi 39 baada ya kuichapa Bournemouth kwa mabao 2-0.
Arsenal walipata mabao yao kupita kwa beki Gabriel Paulista aliyefunga bao la kwanza Dakika ya 27 ya mchezo kisha kiungo wa Kijeruman Mesut Ozil, akahitimisha kazi kwa bao la pili alilolifunga katika dakika ya 63.

Hiddink: Chelsea waonyeshe hamu dhidi ya Man Utd

WatfordChelsea walitoka sare 2-2 mechi dhidi ya Watford Jumamosi
Kaimu meneja wa Chelsea Guus Hiddink amesema timu yake inafaa kuonyesha hamu ya kutaka kushinda dhidi ya Manchester United uwanjani Old Trafford leo.
Vijana hao wameshinda mechi moja pekee kati ya tano zilizopita, nao United wameshindwa mara tatu mfululizo ligini.
Chelsea walitoka sare 2-2 na Watford Jumamosi mechi ya kwanza Hiddink akiwa kwenye usukani baada ya Jose Mourinho kufutwa.
Mholanzi huyo amesema: "Mechi yoyote kati ya Chelsea na Manchester United ni kubwa lakini hii ni ya kipekee bila shaka.”
"Natumai tutaweza kuonyesha hamu ya kutaka kushinda kama tulivyofanya sehemu kubwa ya mechi (dhidi ya Watford).”
  • LVG: Naweza kuondoka mwenyewe Man United
Klabu hiyo ya Stamford Bridge itamkosa mshambuliaji Diego Costa ambaye haruhusiwi kucheza baada ya kuonyeshwa kadi ya tano ya manjano Jumamosi.
United huenda nao wakabadilisha kikosi cha kuanza mechi baada ya kushindwa 2-0 na Stoke City Jumamosi.
Kwenye mechi hiyo, nahodha wao Wayne Rooney alianza akiwa benchi kwa mara ya kwanza tangu Januari 2014.

Chelsea v Manchester United

Takwimu muhimu

8
Mechi ambazo Chelsea wameenda bila kushindwa na United ligini na katika kombe
5
Wachezaji ambao wamepewa kadi nyekundu mechi sita za ligi kati ya Chelsea na United
  • 6 Mechi za EPL ambazo Chelsea wameshinda Old Trafford, ni zaidi ya timu nyingine
Matokeo mabaya kwa United yamezidisha shinikizo kwa meneja Louis van Gaal ambaye baada ya mechi hiyo alisema anaweza kuamua kuondoka kwenye klabu hiyo.
Alipoulizwa iwapo atakuwa bado anasimamia timu hiyo dhidi ya Chelsea, alisema: “Mtahitaji kusubiri na kuona yatakayojiri, lakini nafikiri hivyo (kwamba atakuwa bado kwenye usukani) Ninahisi uungaji mkono kutoka kwa kila mtu katika klabu.”

Tuesday 22 December 2015

Waislamu waokoa wakristo waliotekwa na Alshabab

Waislamu waokoa wakristu waliotekwa na Alshabab
Watu wawili wameuwawa na wengine watatu kujeruhiwa vibaya baada ya wapiganaji wa kundi la al Shabaab kushambulia basi moja la abiria lilokuwa likielekea eneo la Mandera Kaskazini mwa kenya kutoka Nairobi.
Shambulio hilo la kigaidi lilitekelezwa hii leo asubuhi.
Walioshuhudia wameambia mwandishi wa shirika la utangazaji la uingereza  BBC kuwa abiria wa kiislamu waliwalinda wenzao wakristo kwa kukataa kugawanywa kwa makundi.

Marekani yashambuliwa Afghanistan

Mshambuliaji wa kujitolea muhanga huko nchini Afghanistan amewaua askari sita wa vikosi vya jeshi la Marekani miongoni mwa shambulio baya kuwahi kutokea miezi ya hivi karibuni.
Mshambuliaji huyo akiwa kwenye pikipiki, aliwalenga askari wa vikosi vya muungano kati ya majeshi ya NATO na askari wa doria wa Afghanistan karibu na kambi ya vikosi vya anga. Taliban wamekiri kufanya shambulio hilo.

Friday 18 December 2015

Jose Mourinho afutwa kazi Chelsea

MourinhoMourinho alikuwa tayari amekiri Chelsea hawawezi kumaliza katika nne bora ligini
Meneja wa klabu ya Chelsea ya Uingereza amefutwa kazi baada ya klabu hiyo kuandikisha msururu wa matokeo mabaya.
The Blues walishinda Ligi ya Premia msimu uliopita lakini msimu huu mambo yamekuwa kinyume, na wamo alama moja tu juu ya eneo la kushushwa daraja ligini.
Bodi ya klabu hiyo ilikutana jana kujadili hatima ya Mourinho chini ya mmiliki wa klabu hiyo, Mrusi Roman Abramovich.

Thursday 17 December 2015

Magufuli: Elimu ya bure itapatikana Tanzania

ShuleMagufuli amesema serikali itatenga dola milioni 65 za kutumwa shuleni
Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli amewahakikishia Watanzania kwamba elimu ya bure itapatikana kama alivyoahidi.
Akijibu swali la fedha zitapatikana wapi za kutimiza ahadi yake ya elimu ya bure, Magufuli amesema, mwezi huu wa Desemba pekee, Tanzania inatarajiwa kukusanya kiasi cha dola bilioni 1, ambazo hazijawahi kukusanywa.

Maelfu waandamana kupinga serikali ya Jacob Zuma nchini Afrika Kusini

Maandamano ya kumpinga rais Zuma Afrika KusiniMaelfu waandamana kupinga serikali ya Jacob Zuma nchini Afrika Kusini

Maelfu ya wananchi wa Afrika Kusini walifanya maandamano hapo jana katika miji mikubwa ya Afrika Kusini kwa ajili ya kumpinga rais Jacob Zuma.
Waandamanaji hao waliokusanyika katika mitaa ya miji ya Johannesburg, Pretoria, Cape Town na Port Elizabeth, walimshutumu Zuma kwa madai ya ufisadi na kuzorotesha uchumi wa nchi.
Maandamano hayo yaliongozwa na kiongozi wa zamani wa muungano wa biashara Zwelinzima Vavi aliyemlaumu Zuma kwa kumbadilisha waziri wa fedha mara mbili ndani ya wiki moja.
Mnamo tareheh 9 Desemba, Zuma alimfuta kazi aliyekuwa waziri wa fedha Nhlanhla Nene na kumteua David van Rooyen kuziba pengo hilo.
Ndani ya wiki hiyo, Zuma baadaye akamuondoa David van Rooyen na kumteua Pravin Gordhan kuwa waziri mpya wa fedha.

Raia wa Rwanda walio ng’ambo wapiga kura

KagameBw Kagame anatarajiwa bado hajatangaza iwapo atawania tena urais
Raia wa Rwanda wanaoishi nje ya nchi wanapiga kura ya maoni ya marekebisho ya katiba, ambayo yakiidhinishwa yatamruhusu Rais Paul Kagame kuwania urais kwa muhula wa tatu.
Raia wanapigia kura katika afisi za ubalozi.
Mabadiliko hayo yakiidhinishwa, huenda yakamuwezesha Bw Kagame kusalia madarakani hadi 2034.
Raia walioko Rwanda watapiga kura hapo kesho Desemba 18.
Marekani imetoa wito kwa Bw Kagame kuonyesha uzalendo na kuondoka madarakani muda wake ukimalizika mwaka 2017.

Wednesday 16 December 2015

Miili ya watu wapatao 19 imepatikana katika jimbo la Mexico la Guerrero

Miili ya watu wapatao 19 imepatikana katika jimbo la Mexico la Guerrero, ambako wanafunzi 43 walitoweka mwaka jana.
Polisi wanasema miili hiyo ilitupwa kwenye mto mwembamba, wenye kina cha mita mia tano katikati ya miamba na miti karibu na kijiji cha Chichi-hua-lco.
Miili nane kati ya hiyo ilikuwa inaonekana kuchomwa baadhi ya viungo.
Vipimo vya DNA vinatarajiwa kuchukuliwa kutoka katika familia za wanafunzi hao waliokufa, kuweza kujua kama ni kweli ni hao, ambao hawajapatikana mpaka sasa

Tuesday 15 December 2015

Chelsea yachapwa tena na Lester City

Wachezaji wa Leicester City wakishangilia ushindi
Mabingwa watetezi wa ligi kuu England Chelsea wamezidi kuwa katika wakati mgumu msimu huu baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-1 dhidi ya Leicester City.
Mshambulijai wa Jamie Vardy ndie aliyeanza kupeleka msiba kwa The blue baada ya kuandika bao la kwanza katika katika ya 34 ya mchezo. Winga Riyard Mahrez akaongeza bao la pili na la ushindi katika dakika ya 48 ya mchezo.

Sunday 13 December 2015

21 wafariki baada ya moto mkubwa kuzuka kwenye hospitali moja ya vichaa nchini Urusi

Moto wazuka kwenye hospitali ya vichaa Urusi21 wafariki baada ya moto mkubwa kuzuka kwenye hospitali moja ya vichaa nchini Urusi

Watu 21 wameripotiwa kupoteza maisha baada ya moto mkubwa kuzuka kwenye hospitali moja ya vichaa iliyoko Voronezh, kusini magharibi mwa Urusi.
Kulingana na maelezo yaliyotolewa na wizara ya maafa na misaada ya dharura nchini Urusi, miili ya watu 19 ilipatikana kwenye eneo la tukio, huku wengine wawili wakiripotiwa kufariki wakati wa matibabu.
Watu wengine 55 pia wameweza kuokolewa na kuondolewa kutoka kwenye hospitali hiyo, huku baadhi yao wakiwa na majeruhi madogo ya kuunguzwa na moto huo.

Mhongo aahidi kushusha bei ya umeme

WAKATI wapinzani wakipinga uteuzi wa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, waziri huyo amewasihi wananchi kumvumilia kidogo, ili baada ya muda mfupi atoe mpango wa maendeleo ya wizara hiyo, ambao pamoja na mambo mengine, utaelezea bei ya nishati hiyo itakavyoshuka. Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kuapishwa kushika wadhifa huo jana Ikulu jijini Dar es Salaam, Profesa Muhongo alisema mbali na mkakati wa kushusha bei ya umeme, kasi ya kusambaza umeme vijijini kupitia miradi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA), itarejea palepale.
“Nimepokea uteuzi huo, kinachofuata ni kuwatumikia wananchi, niwaombe tu wanivumilie kidogo nitawapa mpango wangu wa maendeleo wa muda mfupi na mrefu, lakini nisisitize tu nishati sio siasa, ni suala la utaalamu, liachwe lifanywe kitaalamu,” alisema Profesa Muhongo.

Saturday 12 December 2015

Hodgson: Itakuwa vigumu kumuacha Vardy

VardyVardy amevunja rekodi ya Van Nistelrooy iliyodumu miaka 12
Meneja wa timu ya taifa ya Uingereza Roy Hodgson amesema itakuwa vigumu kumuacha Jamie Vardy nje ya kikosi chake cha Euro 2016 iwapo mshambuliaji huyo wa Leicester ataendeleza makali yake ya sasa.
Vardy alivunja rekodi ya Ruud van Nistelrooy iliyodumu miaka 12 kwa kufunga mechi 11 mfululizo Ligi ya Premia.

Makaburi matatu nchini Moscow yawekwa Wi-Fi

ChekhovMwandishi mashuhuri Anton Chekhov ni mmoja wa watu mashuhuri waliozikwa Novodevichy
Makaburi matatu yanayotembelewa sana na watu jijini Moscow yatawekewa huduma ya mtandao ya wi-fi.
Wanaotembelea makaburi hayo wataweza kutumia mtandao wa intaneti bila malipo katika makaburi ya Novodevichy, Troyekurovskoye na Vagankovo kuanzia mapema 2016 kwa mujibu wa tovuti ya Moscow City.
Mkuu wa huduma za makaburi mjini Moscow Artem Yekimov anasema lengo ni kusaidia wageni kwenye makaburi hayo kutafuta habari zaidi kuhusu watu mashuhuri waliozikwa humo.
Aidha, kuwafanya wafurahie matembezi yao makaburini.

Mtoto wa Gaddafi aachiwa huru

HannibalHannibal amekuwa kwenye kizuizi cha nyumbani Oman tangu 2012
Mwana wa kiume wa aliyekuwa kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi, Hannibal, ameachiliwa huru baada ya kutekwa nyara kwa muda na kundi la wapiganaji, duru za kiusalama zinasema.
Kwenye video iliyoonyeshwa kwenye runinga ya Lebanon, mfanyabiashara huyo alionekana akiitisha habari zaidi kuhusu kutoweka kwa mhubiri mashuhuri wa dhehebu la Washia nchini Lebanon Musa al-Sadr. Al-Sadra alitoweka mwaka 1978. Alionekana kwenye video hiyo akiwa amejeruhiwa machoni.

Ronaldo atarajia kugombea urais wa shirikisho la kandanda la Brazil

Ronaldo apanga kuwa kiongozi wa CBFRonaldo atarajia kugombea urais wa shirikisho la kandanda la Brazil

Nyota wa zamani wa soka wa Brazil Ronaldo, ametangaza uwezekano wake wa kugombea nafasi ya urais wa shirikisho la kandanda la Brazil CBF.
Ronaldo alitoa tangazo hilo baada ya rais wa CBF Marco Polo del Nero kukabiliwa na kashfa za ufisadi kutoka kwa viongozi wa Marekani.
Naibu wa rais wa CBF Jose Maria Marin pia aliwahi kutangaza kuachia ngazi kutokana na kashfa za ufisadi zilizomuandama mwezi Mei.
Akizungumza na vyombo vya habari mjini Sao Paulo, Ronaldo alimshutumu Del Nero kwa kutumia mbinu ya kumchagua Antonio Nunes kuziba nafasi ya Marin kwa lengo la kuendeleza ufisadi.

Friday 11 December 2015

Lipumba, Lissu wamvaa Magufuli kwa uteuzi wa baraza la mawaziri

Saa chache baada ya rais Magufuli kutangaza baraza lake la Mawaziri ambalo limekuwa baraza dogo kama alivyoahidi, aliyekuwa mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) na mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu wamekosoa uteuzi wa Profesa Sospeter Muhongo na Dk. Harison Mwakyembe.

Dk. Mwakyembe alikuwa waziri wa Uchukuzi katika serikali ya awamu ya nne na hivi sasa ameteuliwa kuwa waziri wa Katiba na Sheria. Profesa Muhongo ambaye alijiuzulu kwa kashfa ya Escrow katika serikali ya awamu ya nne, amerudishwa katika wizara ya Nishati na Madini.

Tanzania yapata maabara ya kuchunguza Ebola

TanzaniaTanzania na Nigeria ndizo nchi pekee zenye maabara ya aina hiyo Afrika kusini mwa jangwa la Sahara
Tanzania ni moja kati ya nchi zilizofanikiwa duniani kuratibu maabara inayohamishika kwa ajili ya mapambano dhidi ya Ebola na magonjwa mengineyo ya mlipuko.
Maabara hii inaweza kusafirishwa mpaka kwenye maeneo yaliyoathirika, ikiwa ndani ya masanduku yaliyofungwa vyema badala ya kusafirisha sampuli kwa ajili ya vipimo kutoka eneo moja kwenda jingine na kuwa katika hatari ya kuathiriwa na vijidudu vingine.

Yaya Toure ndiye mshindi wa Tuzo ya BBC ya Mwanasoka Bora wa Afrika wa Mwaka 2015.

YayaHii ni mara ya pili kwa Toure kutwaa tuzo hiyo
Yaya Toure ndiye mshindi wa Tuzo ya BBC ya Mwanasoka Bora wa Afrika wa Mwaka 2015.
Kiungo huyo wa kati wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 32 anakuwa wa tatu, baada ya Wanigeria Nwankwo Kanu na Jay-Jay Okocha, kushinda tuzo hiyo mara mbili.
Mashabiki walimpigia Toure, anayechezea Manchester City, kura nyingi kushinda Yacine Brahimi, Pierre-Emerick Aubameyang, Andre Ayew na Sadio Mane.
Alishinda tuzo hiyo mara ya kwanza 2013.
Brahimi kutoka Algeria amewahi kushinda tuzo hiyo 2014 naye Mghana Ayew aliishinda 2011. Aubameyang kutoka Gabon alikuwa akishindania tuzo hiyo kwa mwaka wa tatu mtawalia, huku Mane, kutoka Senegal, akishindania kwa mara ya kwanza.

Wednesday 9 December 2015

Msanii mkongwe Morgan Freeman alinusurika katika ajali ya ndege mjini Mississippi Marekani.

Msanii mkongwe Morgan Freeman alinusurika katika ajali ya ndege mjini Mississippi Marekani.
Msanii mkongwe Morgan Freeman alinusurika katika ajali ya ndege mjini Mississippi Marekani.
Duru zinaarifu kuwa mshindi huyo wa tuzo ya Oscar pamoja na rubani wake walinusurika kufariki baada ya ndege waliokuwa wakisafiria kupasuka gurudumu lake ilipokuwa ikikwenda kwa kasi kabla ya kupaa angani.

Man U yapigwa nje michuano ya UEFA

NaldoNaldo alifungia Wolfsburg mabao mawili
Manchester United wameondolewa kutoka kwenye Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya baada ya kushindwa na klabu ya Wolfsburg kutoka Ujerumani Jumanne usiku.
Vijana hao wa Old Trafford waliondoka Ujerumani na kichapo cha 3-2.
Red Devils walikuwa wameanza vyema Anthony Martial alipowafungia baada ya kupata pasi kutoka kwa Juan Mata.

Sunday 6 December 2015

Polisi: Shambulizi la kisu London ni la 'kigaidi'

Polisi wanasema Aliyemdunga kisu abiria London ni 'gaidi'
Idara ya polisi nchini Uingereza inasema kuwa inalichukulia kisa cha udungaji kisu katika kituo cha gari moshi jijini London, kama tendo la kigaidi.
Mtu mmoja aliyekuwa amejihami kwa kisu aliwashambulia abiria katika kituo cha treni kilichoko eneo la Leytonstone.

Gazeti latangaza kifo cha father christmas

SantaFather Christmas alifariki akiwa na umri wa miaka 227, kwa mujibu wa tangazo gazeti hilo
Gazeti moja nchini Norway limelazimika kuomba radhi baada ya kuchapisha tangazo la kicho cha "Father Christmas".
Tangazo hilo lilikuwa la "Mpendwa Father Christmas, aliyezaliwa 12 Desemba 1788", ambaye alidaiwa kufariki tarehe 3 Desemba mjini Nordkapp, ulio kaskazini mwa Norway.

Jose Mourihno azungumzia Usajili baada ya kipigo cha jana kutoka Afc Bornmouth

Mo 3Baada ya kipigo cha kushangaza kutoka kwa Bernoumoth cha goli 1-0 katika uwanja wao wa nyumbani wa Stamford Bridge, kocha Jose Mourinho wa Chelsea ameitoa Chelsea katika kuwania nafasi nne za juu huku akisisitiza kuwa wanahitaji kupigana kwa ajili ya nafasi sita za juu.
Akiongea mara tu baada ya mchezo huo kumalizika, Jose amesema kuwa kabla ya mchezo huo wakikua na imani na mipango ya kugombana kuingia top 4 baada ya awali kujitoa katika mbio za ubingwa, na sasa anasema top 6 ndio kitu pekee wanahitaji kugombania kama timu.

Monday 30 November 2015

Sheikh Ponda aachiwa huru

Mahakama ya hakimu mkazi Morogoro imemuachia huru Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda aliyekuwa akituhumiwa kwa makosa ya uchochezi baada ya mahakama kutoridhishwa na ushahidi wa upande wa mashtaka na hivyo kuonekana hana hatia

Friday 27 November 2015

Mganga atupwa rumande kwa kushindwa kufufua maiti

Mkazi  wa Dar es Salaam, Dunia Salumu maarufu kwa jina la Dk. Manyaunyau, amehukumiwa kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela pamoja na kulipa fidia ya Sh milioni 10 baada ya kupatikana na hatia ya kujipatia fedha Sh milioni 29.6 kwa njia ya udanganyifu.

Manyaunyau anadaiwa kujipatia kiasi hicho cha fedha kutoka kwa mlalamikaji, Tekra Modesta kama malipo ya kazi ya kumfufua marehemu kaka yake aliyefahamika kwa jina moja la Modest ambaye alifariki dunia miaka kadhaa iliyopita.

Akitoa hukumu hiyo jana, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam, Flora Haule, alisema mtuhumiwa huyo ametiwa hatiani baada ya ushahidi uliowasilishwa na upande wa mashtaka kujitosheleza.

Ndoa za utotoni zaongezeka barani Afrika

Msichana mmoja kutoka NigeriaIngawa ni kinyume cha sheria kuoza wasichana walio chini ya umri katika nchi nyingi za Afrika, lakini waatalamu wanasema utekelezaji wa sheria hizo hauna nguvu na mila ya kale kuelekea wasichana na wanawage ingali na nguvu.

 Takwimu mpya zinaonyesha viwango vya kushtusha vya kuongezeka kwa ndoa za utotoni barani Afrika, na kusababisha waatalamu kukutana pamoja nchini Zambia kujadili namna ya kukomesha mila hiyi.
Ingawa ni kinyume cha sheria kuoza wasichana walio chini ya umri katika nchi nyingi za Afrika, lakini waatalamu wanasema utekelezaji wa sheria hizo hauna nguvu na mila ya kale kuelekea wasichana na wanawage ingali na nguvu.
Idadi ya watu barani Afrika inatarajiwa kuongezeka kwa  mara mbili miaka 35 ijayo, na iwapo mwenendo wa sasa hautabadilika, basi hata idadi ya wasichana watakaoozwa itaongezeka vivyo hivyo, na kufikia milioni 310.

Wizara ya ulinzi ya China yaidhinisha mpango wa kuunda kambi ya jeshi nchini Djibouti

China kuunda kambi ya jeshi nchini DjiboutiWizara ya ulinzi ya China yaidhinisha mpango wa kuunda kambi ya jeshi nchini Djibouti

Wizara ya ulinzi ya China imetangaza kuidhinishwa kwa mpango wa kuunda kambi ya jeshi katika nchi ya Djibouti.
Msemaji wa wizara ya ulinzi ya China Wu Chien, alifahamisha lengo la kuundwa kwa kambi hiyo kuwa ni kusaidiana na UN kwa ajili ya kutoa misaada ya kibinadamu katika maeneo ya Somalia na Ghuba ya Aden.
Wu aliongezea kusema kwamba kambi hiyo pia itasaidia kurahisisha harakati za vikosi vya kulinda amani katika kanda hiyo.

Mtoto mchanga apatikana katika hori la kanisa moja mjini New York Marekani

Mtoto mchanga apatikana katika hori la kanisa moja mjini New York Marekani
Zaidi ya miaka 2000 iliyopita, Yesu Kristu alizaliwa kwenye hori mjini Bethlehem.
Na katika tukio ambalo ni linafanana na hilo mtoto mdogo ambaye alikuwa kwenye hori amepatikana ndani ya kanisa moja mjini New York.
Inaaminika kuwa mtoto huyo mchanga ambaye ni mvulana aliachwa na mama yake, katika eneo takatifu la kanisa hilo siku ya Jumatatu jioni.
Mtoto huyo alipatikana na padre Christopher Heanue anayesimamia kanisa hilo.
Padre huyo amesema alishangazwa sana na tukio hilo ila alijawa na huruma nyingi.
Amesema kanisa ni mahala ambako watu wanaohitaji misaada na makao huenda na kwa kuwa papa Francis amekuwa akihubiri na kuhimiza waumini wote wawe na huruma, na zaidi ya yote mwaka huu ni mwaka wa huruma, amefarajika sana kuumpa mvulana huyo matumaini na mahala pa kuishi kwa kuwa anahitaji huruma na malezi.

Thursday 26 November 2015

Man U yajiweka pabaya kusonga mbele UEFA

Man U vs PSV
Kikosi cha Manchester United bado kipo kwenye wakati mgumu kuhakikisha kinafuzu hatua ya mtoano ya mashindano ya klabu bingwa barani Ulaya kufuatia ulazimishwa sare ya bila kufungana na ya timu ya PSV kwenye uwanja wa Old Trafford mchezo uliopigwa usiku wa Jumatano November 25, 2015.
Ulikuwa ni usiku wa aina yake kwa upande wa United ambao walitawala mchezo huo kwa kila idara lakini hawakufanikiwa kutumbukiza mpirakwenye nyavu za wapinzani wao.
Jesse Lingard alipana nafasi nzuri ya kufunga  lakini mpira ukagonga mwamba huku shuti la Morgan Schneiderlin likiokolewa.

Bunge la Uingereza la jadili kuhairishwa kwa uchaguzi Zanzibar

http://mtanzania.co.tz/wp-content/uploads/2015/11/mtz14.jpgHALI ya kisiasa na kufutwa kwa uchaguzi wa urais pamoja na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar hatimaye imetua na kujadiliwa katika Bunge la mabwanyenye la nchini Uingereza.
Uamuzi huo umekuja siku moja baada ya wapinzani wawili wa kisiasa visiwani humo, Rais Dk. Ali Mohamed Shein na Makamu wake wa Kwanza ambaye pia alikuwa mgombea wa urais kupitia CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, kuendelea na vikao vya siri vinavyoshirikisha marais wastaafu wa Zanzibar.
Sakata hilo liliibuka jana nchini Uingereza katika kikao cha Bunge ambapo mbunge Lord Steel wa Aikwood kutoka Chama cha Liberal Democrat, alitaka kujua tathmini ya Serikali ya Uingereza kuhusu uchaguzi nchini Tanzania, hasa ule wa Zanzibar na kilichoelezwa kwa Serikali ya Tanzania au Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola kuhusu uchaguzi huo.

Didier Drogba ataka Ukocha chelsea

Mshambulizi wa zamani wa Chelsea na Ivory Coast Didier Drogba amesema kuwa atarejea Stamford Bridge kuwa kocha.
Mshambulizi wa zamani wa Chelsea na Ivory Coast Didier Drogba amesema kuwa atarejea Stamford Bridge kuwa kocha.
Drogba, ambaye kwa sasa anasakata soka ya kulipwa huko Canada, aliifungia the Blues mabao 164 katika enzi yake huko Stamford Bridge.
"Ningependa kuihudumia klabu hiyo hata baada ya kukamilika kwa kipindi changu cha uchezaji''
''Tayari nimekubaliana na wakurugenzi wa klabu hiyo kuwa ninaweza kurejea kuwa mkufunzi kwa sababu klabu hiyo ilinifaa sana nilipoanza'',alisema mshambulizi huyo mwenye umri wa miaka 37.
''Kwani siwezi kuwa meneja ? kwani siwezi kuwa mkurugenzi wa kiufundi,mkufunzi wa chuo cha mafunzo ya wachezaji ama hata mshauri wa washambuliaji ?

Wednesday 25 November 2015

Rubani wa Urusi aokolewa Syria

Rubani wa Urusi aokolewa Syria
Urusi inasema kuwa msaidizi wa rubani wa ndege ya kijeshi iliyodunguliwa na Uturuki hapo jana ameokolewa na kurejeshwa katika kambi yao ya kijeshi iliyoo Syria.
Urusi inasema kuwa afisa huyo yuko katika hali njema katika kambi ya kijeshi ya Lattakia.
Wizara ya ulinzi nchini Urusi inasema kuwa rubani mwingine na mwanajeshi aliyeshiriki katika operesheni ya kwenda kuwaokoa marubani hao wa ndege iliyodunguliwa nao waliuawa.
 
Ubalozi wa Urusi na taarifa kutoka kwa serikali ya Syria zinasema kuwa rubani huyo aliokolewa na wanajeshi wa Syria
Ubalozi wa Urusi na taarifa kutoka kwa serikali ya Syria zinasema kuwa rubani huyo aliokolewa na wanajeshi wa Syria na anarudishwa kwenye kambi ya jeshi la urusi eneo la Lattakia huko Syria.
Moscow inasema kuwa operesheni nchini Syria zitaendelea kuwakabili wapiganaji wa Islamic State na makundi mengine ya kijihadi.
Aidha Urusi imesema kuanzia leo ndege zinazoelekea kutekeleza operesheni za mashambulizi dhidi ya makundi ya kijihadi zitapewa ulinzi mkali na ndege za kivita.
Vilevile mitambo ya rada ya Urusi itatumika kuimarisha ulinzi wa angani katika maeneo ya mipakanai ya Syria.
Mitambo ya rada ya Urusi itatumika kuimarisha ulinzi wa angani katika maeneo ya mipakanai ya Syria.
Mitambo hiyo itawekwa katika kambi ya kijeshi ya Urusi iliyoko Lattakia.
Hayo yamejiri huku rais wa Marekani Barack Obama amemhakakishia mwenzake rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan kuwa nchi yake inaiunga mkono Uturuki katika jitihada za kulinda mipaka yake.
Hakikisho hilo la rais Obama linafwatia hatua ya Uturuki kuidungua ndege ya Urusi karibu na mpaka wa Syria.

Kilimanjaro stars yapaa , Zanziber Heros yabanwa

Michuanao ya Cecafa Chalenji Cup Imeendelea tena jana kwa michezo miwili katika hatua ya makundi.
Zanzibar ilifungwa bao 4-0 na Uganda ikiwa ni Mechi ya Kundi B.
Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) imeichapa Rwanda bao 2-1 katika mchezo uliopigwa mjini Awassa na kupaa kileleni mwa Kundi A wakiwa na Pointi 6 kwa Mechi 2 na kujihakikishia kucheza hatua ya Robo Fainali.

Barcelona washusha mvua ya magoli kwa As Roma

Barcelona wakiwa nyumbani walichomoza na ushindi wa mabao 6-1 dhidi ya As Roma.
Buyen Munich wakiichapa Olympiakos bao 4-0, Maccabi Tel Aviv wakila hio kwa Chelsea kwa kichapo cha mabao 4-0.
BATE Borislov wakifungana bao 1-1 na Buyer Liverkusen , FC Porto wakilala bao 2-0 dhidi ya Dynamo Kiev, Zenit St P wakiichapa Valencia bao 2 – 0 na Lyon wakilala mbele ya KAA Gent bao 2-1.
Michuano hiyo inatarajia kuendelea tena hii leo kwa michezo kadhaa.
Miongoni mwa mechi hizo ni Man United dhdi ya PSV Eindhoven, Atletico Madrid na Galatasaray, Juventus dhidi ya Man City na Shakhtar Donetsk watawaalika Real Madrid.

Tuesday 24 November 2015

Marekani yatoa tahadhari kwa raia wake

Tahadhari ya kusafiri na mashambulio ya kigaidi
Serikali ya Marekani imetoa tahadhari ya kusafiri duniani kote kwa raia wake, ikiwaonya kuwepo kwa ongezeko la tishio la kigaidi.
Tahadhari hiyo inasema taarifa zilizopo hivi sasa zinaashiria kwamba makundi kama vile Islamic State, al-Qaeda na Boko Haram wanaendelea kupanga mashambulio katika maeneo tofauti.

Marekani yatoa tahadhari kwa raia wake

Tahadhari ya kusafiri na mashambulio ya kigaidi
Serikali ya Marekani imetoa tahadhari ya kusafiri duniani kote kwa raia wake, ikiwaonya kuwepo kwa ongezeko la tishio la kigaidi.
Tahadhari hiyo inasema taarifa zilizopo hivi sasa zinaashiria kwamba makundi kama vile Islamic State, al-Qaeda na Boko Haram wanaendelea kupanga mashambulio katika maeneo tofauti.

Monday 23 November 2015

Said Kubenea kumburuza Spika wa bunge Job Ndugai Mahakamani


Mbunge wa Ubungo (Chadema), Saed Kubenea amesema atamfikisha mahakamani Spika wa Bunge, Job Ndugai kwa kuvunja kanuni baada ya kuwaingiza polisi ndani ya ukumbi wa chombo hicho.

Polisi hao waliingia ndani ya ukumbi huo wiki iliyopita wakati Rais John Magufuli alipofika kwa ajili ya kuhutubia Bunge.

Kubenea alisema kitendo cha askari kuingia ndani ya Bunge kwa mara ya mwisho kilitokea nchini Uingereza mwaka 1930 na hakijawahi kutokea tena isipokuwa nchini.

ZINEDINE ZIDANE AMESEMA HIVI KUHUSU YEYE KUCHUKUA NAFASI YA RAFAEL BENITEZ

1622E2AB000005DC-0-image-a-22_1448238461341
Baada ya mechi ya El Classico zikavuma tetesi kwamba Zinedine Zidane anatakiwa kuchukua nafasi ya Rafael Benitez kwenye club ya Real Madrid.
Tetesi hizo zilipewa kasi baada ya mchezaji wa Brazil Rivaldo ku-post kwenye instagram yake kwamba ni wakati wa Real Madrid kumpa nafasi Zidane ajaribu ku-manage club hiyo kama Pep Gurdiola alivyopewa nafasi na Barcelona.

Baada ya Madrid Kuchapwa na Barcelona benzema ajikuta akihudhuria mazoezi mwenyewe


Benzema 2
Mshambuliaji Karim Benzema jana Jumapili alitokea pekee kati ya wachezaji wa kikosi cha kwanza cha Madrid kufanya mazoezi baada ya kocha Rafael Benitez kuwapa ofa ya mapumziko wachezaji wa kikosi cha kwanza siku ya Jumapili kutokana na kipigo cha goli 4-0 kutokana kwa mahasimu wao Barcelona.

16 wauawa katika ufyatulianaji wa Risasi marekani

Polisi wamesema walikuwa njiani kwenda kutawanya watu ufyatuaji wa risasi ulipotokea
Watu 16 wamejeruhiwa kwenye ufyatuaji wa risasi katika bustani moja mjini New Orleans, polisi wamesema.
Msemaji wa polisi Tyler Gamble amesema maafisa wa polisi walikuwa njiani kuvunja mkusanyiko mkubwa wa watu katika bustani ya Bunny Friend Park mjini pale risasi zilipofyatuliwa.
Ambiulensi ziliwapeleka watu 10 hospitalini, Bw Gamble alisema, na wengine walikimbizwa hospitalini kwa kutumia magari ya kibinafsi.

Wapinzani wachukua dola Argentina

Macri
Macri alikuwa ameshindwa kwenye duru ya kwanza

Mgombea wa chama cha upinzani cha Conservative Mauricio Macri amethibitishwa kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais Argentina, huku mgombea wa chama tawala akikubali kushindwa.
Baada ya karibu kura zote kuhesabiwa, Bw Macri alikuwa na 52% akilinganishwa na Daniel Scioli aliyepata 48%.
Shangwe na vigelegele vilitanda katika makao makuu ya kampeni ya Bw Macri baada ya kura za maoni runingani kuonyesha alikuwa ameshinda.
Bw Macri, meya wa zamani wa Buenos Aires, alikuwa ameshindwa na Scioli, ambaye ni gavana wa mkoa wa Buenos Aires, kwenye duru ya kwanza ya uchaguzi Oktoba.
Lakini wote wawili hawakuweza kushinda moja kwa moja na duru ya pili ikaandaliwa, mara ya kwanza kwa uchaguzi kuingia duru ya pili katika historia ya Argentina.
Ushindi wa Bw Macri ndio wa kwanza katika zaidi ya mwongo mmoja kwa upinzani wenye kuegemea siasa za mrengo wa kati kulia.

Saturday 21 November 2015

Rais wa Mali atangaza hali ya Hatari

MaliWengi wa mateka waliokolewa
Rais wa Mali Ibrahim Boubacar Keita ametangaza hali ya hatari nchini humo baada ya shambulio kwenye hoteli moja mjini Bamako kuua watu zaidi ya 20.
Bw keita ametangaza hali ya hatari itakayodumu kwa siku 10, pamoja na siku tatu za maombolezo ya kitaifa.
Watu wenye silaha wanaodaiwa kuwa wanamgambo wa kundi la Kiislamu walishambulia hoteli ya Radissom Blue mjini Bamako na kushikilia mateka watu 170.
Maafisa wa Marekani wamethibitisha hakuna mateka zaidi wanaoshikiliwa.
Makundi ya Al-Qaeda Afrika Kaskazini na kundi jingine la al-Murabitoun yamedai kuhusika kwenye shambulio hilo

Thursday 19 November 2015

Nadal amchapa Andry Murray

Nadal amchapa Murray
Mchezaji namba tano kwa ubora wa mchezo wa tenesi kwa upande wa wanaume Rafael Nadal,amemshinda muingereza Andry Murray.
Nadal ameshinda mchezo huo kwa jumla ya seti 6-4 6-1, mchezo uliofanyika katika uwanja wa O2 Arena.
Nae Stan Wawrinka anayeshikilia nafasi ya nne kwa ubora alimfunga mpinzani wake David Ferrer aliyeko katika nafasi ya saba kwa jumla ya seti 7-5 6-2.
Murray atacheza na Wawrinka katika mchezo wa mwisho wa makundi siku ya ijumaa.

Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ametoa amri kushikiliwa kwa afisa wa juu

Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari
Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ametoa amri kushikiliwa kwa afisa wa juu anayetuhumiwa kwa wizi wa zaidi ya dola bilioni mbili zilizotarajiwa kununua silaha za kukabiliana na wapiganaji wa Boko Haram.
Afisa huyo Sambo Dasuki alikuwa mshauri wa masuala ya usalama ya taifa kipindi cha utawala wa Rais aliyemaliza muda.

Wednesday 18 November 2015

Rufaa ya Sepp Blatter na Platini yakataliwa


Sepp Blatter na Michel Platini
Maombi ya rais wa FIFA Sepp Blatter na makamu wa rais wa shirikisho hilo Michel Platini ya kupinga kusimamishwa kazi kwa siku 90 waliowekewa na kamati ya Fifa yamekataliwa.
Wawili hao walisimamishwa kazi mnamo mwezi Octoba huku kamati ya Fifa ikichunguza madai ya ufisadi dhidi yao.

Ufaransa yawaua wapiganaji 33 Syria

wapiganaji wa islamic state mjini Raqqa

Mashambulio ya Ufaransa na mataifa mengine dhidi ya ngome ya Islamic State huko Raqqa nchini Syria siku ya jumapili yamewauwa takriban wapiganaji 33,wanaharakati wamesema.
Kundi la wapiganaji wa haki za kibinaadamu kutoka Syria limesema kuwa wengi walifariki wakati vituo vya kukagua watu vilivyoshambuliwa.

Saturday 14 November 2015

Anna Makinda aukimbia Uspika

Anna Makinda
Aliyekuwa Spika wa Bunge la Kumi, Anne Makinda ameamua kukaa kando ya mbio za Uspika wa Bunge la 11, siku chache baada ya kufanya kampeni kuwania nafasi hiyo kwa mara nyingine.

Taarifa za kuaminika zimeeleza kuwa Mama Makinda aliamua kuchukua uamuzi huo wa kujiweka kando ya mchuano huo baada ya kushauriwa na watu wake wa karibu kufuatia dalili walizoziona kwenye mchakato huo pamoja na mambo mengine.

Awali mama Makinda alidaiwa kuanza kampeni kupitia ujumbe mfupi alioutuma kwa wabunge wateule kupitia simu za mkononi akiwapongea na kuwaomba kumuunga mkono kuwa Spika wa Bunge la 11.