Thursday 19 November 2015

Nadal amchapa Andry Murray

Nadal amchapa Murray
Mchezaji namba tano kwa ubora wa mchezo wa tenesi kwa upande wa wanaume Rafael Nadal,amemshinda muingereza Andry Murray.
Nadal ameshinda mchezo huo kwa jumla ya seti 6-4 6-1, mchezo uliofanyika katika uwanja wa O2 Arena.
Nae Stan Wawrinka anayeshikilia nafasi ya nne kwa ubora alimfunga mpinzani wake David Ferrer aliyeko katika nafasi ya saba kwa jumla ya seti 7-5 6-2.
Murray atacheza na Wawrinka katika mchezo wa mwisho wa makundi siku ya ijumaa.

No comments: