Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) imeichapa Rwanda bao 2-1 katika mchezo uliopigwa mjini Awassa na kupaa kileleni mwa Kundi A wakiwa na Pointi 6 kwa Mechi 2 na kujihakikishia kucheza hatua ya Robo Fainali.
Mabao ya Kilimanjaro stars yalifungwa na Said Ndemla pamoja na Simon Msuva huku bao la Rwanda likifungwa na mchezaji Tisiyege.
Michuano hiyo itaendelea tena leo jumatano kwa mechi kadhaa ambapo Kenya itachuana na Burundi.
Somalia itaivaa Ethiopia, Malawi itaikabili Djibouti na Sudan kusini watachuana na ndugu zao Sudan.
No comments:
Post a Comment