Wednesday 20 January 2016

Serikali Yatoa Tamko Kuhusu Dawa Mpya ya Ukimwi Iliyogundulika Hivi Karibuni

SERIKALI imesema kama Shirika la Afya Duniani (WHO), litapitisha matumizi ya dawa mpya ya ugonjwa Ukimwi wataitumia, lakini kwa sasa haiwezi kuzungumzia tafiti za ugonjwa huo ambazo zipo nyingi.
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Michael John, amesema kwa sasa zipo tafiti nyingi, lakini wao kama wizara wanasubiri mwongozo kutoka WHO ambao ndiyo unathibitisha ubora wa dawa na matumizi yake.
“Zipo tafiti nyingi tunazisikia zinafanyika, lakini hili la Ukimwi ni mapema mno kulizungumzia ila kinachohitajika ni kusubiri mwongozo wa WHO ambao ndio wanatuongoza kwenye orodha ya dawa na matumizi yake katika magonjwa mbalimbali,” alisema John.

Sunday 17 January 2016

CCM Chali Dar es Salaam, UKAWA Washinda Kiti ca Umeya Kinondoni na Ilala

Hatimaye baada ya danadana za muda mrefu, uchaguzi wa kuwachagua Mameya wa Manispaa za Kinondoni na Ilala, umefanyika na Umoja wa Vyama vinavyunda Katiba ya Wananchi (Ukawa) wamefanikiwa kuongoza Manispaa hizo.
Chaguzi hizo zilizhairishwa mara mbili kutokana na mvutano uliotokewa katika chaguzi za nyuma, ikiwa ni pamoja na kusimamishwa kwa amri za mahakama.

Tuesday 12 January 2016

Nikipata mwanamke atakayeweza kuziba nafasi ya Shilole ndio nitafuta tattoo zake – Nuh Mziwanda

Ingawa Shilole tayari amefunika tattoo aliyochora kifuani yenye jina la ex wake Nuh, kwa kuongeza mchoro wa ua juu yake baada ya wawili hao kuachana, Nuh Mziwanda amesema yeye bado hajaamua kufuta tattoo zake.

Nuh ambaye alichora tattoo mbili, moja ikiwa na jina la Shishi Baby na nyingine ikiwa na sura ya Shishi amesema kuwa endapo atapata mwanamke wa kuziba pengo la Shishi ndio atafuta tattoo hizo.

Samatta ataka kusherehekea tuzo yake na majirani zake





Mbwana Samatta 


Mwanasoka Bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza soka ndani ya Afrika, Mbwana Samatta hapendi makuu kwani familia yake ilipomuuliza achague hoteli watakayomfanyia sherehe ya kumpongeza kwa kutwaa tuzo hiyo ya Afrika alichowajibu kiliwaacha hoi.






Mwanasoka Bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza soka ndani ya Afrika, Mbwana Samatta hapendi makuu kwani familia yake ilipomuuliza achague hoteli watakayomfanyia sherehe ya kumpongeza kwa kutwaa tuzo hiyo ya Afrika alichowajibu kiliwaacha hoi.
Baba mzazi wa nyota huyo, Pazi Ally Samatta akielezea alichojibiwa na mwanae huyo alisema, “Baada ya kumwambia Samatta kwamba familia imekuambia chagua ni wapi utafurahia tukikufanyia sherehe ya kukupongeza,  yeye alinijibu baba nifanyie sherehe hiyo nyumbani kwa sababu nataka kufurahia pamoja na majirani wote wanaotuzunguka,” alisema.

CUF: Uchaguzi unaweza kuzua vurugu Zanzibar

Chama cha CUF kimepinga hatua ya tume ya uchaguzi ya kufuta matokeo ya uchaguzi wa urais
Chama cha Wananchi (CUF) kimeonya kuwa kurudiwa kwa uchaguzi visiwani Zanzibar kunaweza kusababisha vurugu na kumtaka Rais wa Tanzania Dkt John Magufuli kuingilia kazi kutatua mzozo ulitokana na uchaguzi visiwani humo.
Katibu mkuu wa chama hicho Maalim Seif, akihutubia wanahabari, amesema chama hicho hakitaki uchaguzi urudiwe na kuendelea kusisitiza msimamo wa awali kwamba mshindi wa uchaguzi uliofanywa 25 Oktoba mwaka jana anafaa kutangazwa.
"Ni vyema tukaweka waziwazi hapa kwamba kurudiwa uchaguzi sio suluhishona hakukubaliki. Kwani, kama nilivyoonesha hakuna hoja wala msingi wa kikatiba na kisheria wa uchaguzi kurudiwa," amesema Bw Seif.
Bw Maalim Seif, aliyekuwa mgombea urais wa chama hicho, alionekana kupendekeza mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Jecha Salim Jecha ang’atuke.

Al-Shabab wako 'huru' kushiriki soka Somalia

Wapiganaji wa Alshabaab
Mkuu wa shirikisho la soka nchini Somalia amesema kuwa kundi la wapiganaji wa al-Shabab liko huru kushiriki katika ligi kuu ya soka nchini humo.
Abdiqani Said Arab amemuambiwa mwandishi wa BBC jijini Nairobi John Nene kwamba iwapo wapiganaji hao wanataka kushiriki watepewa fursa.
''Hatuwapingi na hawatupingi," alisema.
Kundi la al-Shabab linaloendesha itikadi kali, limewaagiza wanasoka kuvaa suruali ndefu na limepiga marufuku muziki katika maeneo linalodhibiti.

Messi atwaa tuzo ya Balloon D'or

Mshambuliaji wa klabu ya soka ya Barcelona, na timu ya taifa ya Argentina Lionel Messi, ametwaa tuzo ya mchezo bora wa dunia.
Messi mwenye miaka 28 alishinda kwa 41.33% kwa kura zote zilizopigwa, huku Cristiano Ronaldo akishika nafasi ya pili kwa 27.76% na Neymer akipata 7.86%.
Hii ni mara yake ya tano kutwaa tuzo hiyo.
Kwa upande wa wanawake nyota wa Marekani Carli Lloyd, ameibuka kuwa mchezaji bora kwa upande wa wanawake.
Goli bora la mwaka likifahamika kama Puskas limwendea Wendell Lira anayekipiga katika Atletico Goianiense ya Brazil.
Kocha wa Barcelona Muhispania Luis Enrique amechaguliwa kuwa kocha bora wa mwaka kwa kuiongoza barca kufanya vizuri barani Ulaya kwa kutwa mataji matano msimu uliopita.
Jill Ellis kocha wa kikosi cha taifa cha Marekani amekuwa kocha bora wa wanawake baada ya kuongoza timu ya taifa ya Marekani kufanya vyema katika michuano ya kombe la dunia.

Sunday 10 January 2016

Mwanamke nchini Kenya achomwa kisu usoni na mume wake

Mwanamke nchini Kenya achomwa kisu usoni na mume wakeMwanamume mmoja nchini Kenya afikishwa mahakamani kwa kumchoma kisu cha usoni mke wake

Wakenya watoa wito wa kufanyika hatua za haraka, baada ya mwanamume mmoja aliyefikishwa mahakamani kwa kosa la kumchoma kisu mke wake chenye urefu wa nchi 10 usoni ambapo ilibidi kufanyiwa upasuaji kwa ajili ya kuondolewa,lakini mwanamke huyo amekataa kutoa ushahidi dhidi ya mumewe.
Kesi hiyo imeonekana kusambazwa mno katika mitandao ya twitter katika nchi za Afrika mashariki ambapo kumekuwa na unyanyasi mwingi wa wanawake huku watuhumiwa kutopata adhabu yoyote.
Picha nyingi zinazomuonyesha mwanamke huyo akiwa amechomwa kisu katika shavu na pia picha za X-ray zikionyesha kisu kimeingia upande wa kulia na kuchomoza hadi upande wa pili zimesambazwa katika mitandao ya kijamii huku zikiwa na maandishi yanayosema “haki kwa Fatuma”.
Mkurugenzi wa mashtaka alisema katika taarifa yake Twitter, kuwa Bwana Mohamed Deeq alikanusha kosa lake la kumchoma kisu mkewe Fatuma Ibrahim,wakati wa ugomvi wao wa ndani katika mahakama iliyopo katika mkoa wa Wajir kaskazini mashariki mwa Kenya siku ya Ijumaa.
Kaimu naibu wa DPP Nicholas Mutuku,aliiambia Reuters kuwa Deeq bado anashikiliwa katika  kituo cha polisi mkoani Wajir mpaka atakapo shitakiwa tarehe 13 januari.

Saturday 9 January 2016

Zitto: Rais Magufuli Ameshaipotezea Nchi Mapato ya Bilioni 8 Tangu Aingie Madarakani

Mbunge wa Kigoma mjini, Zitto Kabwe ameilalamikia serikali ya Magufuli kwa kitendo chake cha kukaa kimya kuhusu ufisadi unaoendelea kufanywa na Harbinder Singh Seth, mmiliki wa IPTL, ambaye huvuna kiasi cha malipo ya bilioni 4 kila mwezi kama malipo ya kuliuzia umeme shirika la ugavi wa umeme nchini, Tanesco.

Zitto ambaye ni mmoja wa wabunge walioibua na kusimamia kidete sakata la ufisadi wa Tegeta Escrow bungeni mwishoni mwa mwaka juzi (2014), amesema hayo kufuatia tangazo la serikali kuhusu kashfa ya Commodity Import Support ya miaka ya miaka 1980 na 1990s, ambapo ameisifu serikali kwa hatua hiyo na kuhoji iweje ikomae na kashfa hiyo tu, huku ikisita kuchukua hatua kwenye sakata la IPTL linaloigharimu serikali kiasi kikubwa cha fedha kila mwezi isivyostahili?

Kampuni ya IPTL imeshalipwa fedha mara mbili tangu Rais Magufuli aingie rasmi madarakani, hivyo kufanya hesabu zitimie bilioni 8 kwa kipindi cha miezi miwili mpaka sasa.

Msome;

"Nimeona tangazo la Serikali kuhusu kashfa ya Commodity Import Support. Hii ni kashfa ya miaka ya 1980s na 1990s. Ni hatua nzuri. Lakini ina maana gani wakati Serikali inavuta miguu kwenye suala la IPTL? Harbinder Singh Seth na genge lake wanavuta tshs 4bn kila mwezi. Kwa kutochukua hatua kuhusu IPTL, Rais Magufuli ameshaipotezea nchi mapato ya tshs 8bn tangu aingie madarakani. ‪#‎TegetaEscrow‬ ndio baba la mtandao wa ufisadi nchini kwetu" - Zitto Kabwe.

Adele aiba wimbo wa msanii maarufu Ahmet Kaya wa Uturuki

Adele aiba wimbo wa msanii maarufu wa UturukiAdele aiba wimbo wa msanii maarufu Ahmet Kaya wa Uturuki

Hakuna tena shaka muimbaji Adele kutoka Uingereza imebainishwa kuwa alitumia wimbo wa msanii maarufu wa zamani wa Uturuki aliekuwa akitambulika katika ulimwengu wa muziki kwa ina la Ahmet Kaya.
Wimbo ambao Adele aliiba si mwingine ni wimbo uliotoka kwa jina la "Acilara Tutunmak".
Wimbo huo Adele aliubadilisha jina na kutengeneza kibao chake cha "Million Years Ago" ambacho kinafanya vizuri katika soko la muziki.
Kufanana kwa nyimbo hizo mbili kumeleta gumzo katika ulimwengu wa muziki.
Iwapo mke wa Ahmet Kaya, Bi Gulten Kaya anaweza kukata rufaa mbele ya vyombo vya sheria kuhusu wimbo huo.

Mtuhumiwa namba Moja Kesi Ya Mauaji ya Dk. Mvungi Afariki

Mshitakiwa wa kwanza katika kesi ya mauaji ya aliyekuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Dk. Sengondo Mvungi ameripotiwa kufariki akiwa gerezani, siku chache kabla ya kesi kusikilizwa.
Taarifa ya kifo cha mshtakiwa huyo aliyetajwa kwa jina la Chibago Chiuguta mwenye umri wa miaka 33, zilitolewa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kueleza kuwa mshitakiwa huyo alikutwa akiwa amekutwa na umauti.
Kufuatia taarifa hizo, Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama hiyo, Thomas Simba aliagiza upande wa Magereza kuhakikisha wanafuatilia cheti cha kifo cha mshitakiwa huyo.
Marehemu alikuwa kati ya washtakiwa 11 waliodaiwa kumuua Dk. Mvungi katika eneo la Msakuzi, Kiswegere katika wilaya ya Kinondoni. Washtakiwa hao wanadaiwa kufanya kosa hilo Novemba 3 mwaka 2013.
Upelelezi wa tukio hilo bado unaendelea.

Friday 8 January 2016

Mwanachama wa IS amuua mamake hadharani

ISKundi la IS hutekeleza sheria kali za Kiislamu
Mpiganaji wa kundi la Islamic State nchini Syria amemuua mamake hadharani kwa sababu alimwambia ahame kundi hilo, wanaharakati wanasema.
Ali Saqr, 21, alimuua mamake, Lena al-Qasem, 45, nje ya afisi ya posta mjini Raqqa, Syria, watu walioshuhudia wanasema.
Mji wa Raqqa umekuwa ukihudumu kama mji mkuu wa IS tangu wapiganaji hao kutekwa mji huo Agosti 2013.
Kundi hilo huwa halivumilii watu wanaopinga msimamo wake na kutoa adhabu kali kwa wanaopinga kundi hilo, na mara nyingi adhabu hutekelezwa hadharani.
Maafisa wa Shirika la Syrian Observatory for Human Rights (SOHR) lenye makao yake Uingereza na kundi la wanaharakati wa Raqqa is Being Slaughtered Silently (Raqqa Inachinjwa Kimy akimya) wamethibitisha kisa hicho.
Lena al-Qasem alikuwa amemwambia mwanawe kwamba muungano unaoongozwa na Marekani ungeangamiza kundi hilo, na akajaribu kumshawishi ahame mji huo pamoja naye.
Mwanawe alijulisha wenzake katika IS, na agizo likatolewa auawe.
Ali Saqr anadaiwa kumpiga risasi mamake nye ya afisi ya posta mbele ya mamia ya watu.
Kundi la IS hutekeleza sheria kali za Kiislamu, zenye kuegemea madhehebu ya Kisuni.
Kundi hilo limedhibiti maeneo ya Iraq na Syria tangu 2014

Thursday 7 January 2016

Messi aing’arisha Barcelona

MessiMessi alifungia Barca mabao mawili
Mshambuliaji wa klabu ya Barcelona Lionel Messi amekuwa shujaa baada ya kufunga mabao mawili katika ushindi wa 4-1 dhidi ya Espanyol katika mchezo wa kwanza wa hatua ya 16 Bora michuano ya Kombe la Mfalme, maarufu kama Copa del Rey.
Mechi hiyo ilichezewa uwanja wa Nou Camp.
Katika ushindi wa mabao hayo manne wachezaji wengine walioiwezesha timu hiyo kushinda ni Gerard Pique na Neymar Da silva.
Bao pekee la Espanyol lilifungwa na Felipe Caicedo.
Espanyol walimaliza mechi hiyo wakiwa na wachezaji tisa uwanjani baada ya Arsensio Pérez na Diop kuonyeshwa kadi nyekundu.
Kufuatia mabao hayo, Messi sasa amefikisha idadi ya mabao aliyofunga msimu huu, licha ya majeraha, hadi 14 kutoka kwa mechi 21.
Messi ni mmoja wa wanaoshindania tuzo ya mchezaji bora wa mwaka duniani ijulikanayo kama Ballon d'Or. Mshindi wa tuzo hiyo atatangazwa Jumatatu wiki ijayo.

Wednesday 6 January 2016

Polisi wakamata silaha kadhaa nchini Kenya

Polisi wakamata silaha kadhaa nchini KenyaSilaha kadhaa zakamatwa kwenye nyumbani moja ya mshukiwa wa ugaidi mjini Mombasa

Maafisa wa polisi nchini Kenya wamekamata silaha kadhaa baada ya kuvamia nyumba moja ya mshukiwa wa ugaidi iliyoko mjini Mombasa.
Silaha hizo zilizokamatwa zilikuwa ni bunduki aina ya G3 na risasi zake 20, bunduki aina ya M4 na risasi zake 7, pamoja na risasi nyingine 318 za ziada.
Wakati huo huo, kompyuta moja na simu 15 za rununu pia zilipatikana kwenye nyumba hiyo.
Silaha na vifaa hivyo vya mawasiliano vinadaiwa kupangwa kutumika katika utekelezaji wa mashambulizi ya kigaidi mjini humo

Korea Kaskazini yafanya jaribio la bomu

Kiongozi wa Korea KaskaziniKim Jong Un kiongozi wa Korea Kaskazini
Korea Kaskazini inasema kwa mara ya kwanza imefanikiwa kufanya majaribio ya bomu la nguvu ya maji, maarufu kama bomu la haidrojeni.
Tangazo hili limetolewa na runinga ya taifa baada ya kusikika mitetemeko ya ardhi ya kipimo cha tano nukta moja, karibu na eneo kuliko na kinu cha nyukilia. Wataalamu wa Marekani wanafanya uchunguzi ikiwa yalikua majaribio ya bomu hilo au ilikua zana nyingine ya nyuklia isiyokuwa na nguvu.

 
Kiongozi wa Korea KaskaziniTangazo hilo lilitolewa na runinga ya taifa
Mwandishi wa BBC anasema bomu la nguvu ya maji lina uwezo mkubwa wa mlipuko ikilinganishwa na mabomu mengine yenye madini ya Plutonia ambayo Korea kaskazini imefanya majaribio katika miaka ya awali.
Mamkala za Pyongyang zimefanyia majaribio mengine matatu ya kinyukilia katika eneo kulikofanywa majaribio ya sasa kwa kipindi cha miaka kumi

Mbwana Ally Samatta atua Nigeria sherehe za kutuza wachezaji

Mbwana Samatta
Mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Tanzania na klabu ya TP Mazembe ya Congo DR, Mbwana Samatta leo hii anatarajiwa kuwasili nchini Nigeria kuhudhuria sherehe za utoaji wa tuzo kwa wachezaji bora barani Afrika zitakazofanyika katika mji wa Abuja Alhamisi tarehe 7 Januari.
Mbwana Samatta anawania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wa ndani, huku pia akiwa mfungaji bora wa michuano ya Ligi ya Mabingwa (CAF CL) baada ya kuifungia klabu yake ya TP Mazembe mabao 8 na kuibuka mabingwa wapya wa michuano hiyo.
Samatta anawania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika pamoja na mlinda mlango wa TP Mazembe, Robert Kidiaba (Congo DR) na mshambuliaji wa Etoile du Sahel Baghdad Boundjah (Algeria).
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Mwesigwa Selestine ameandamana na Samatta kuhudhuria sherehe hizo.

Monday 4 January 2016

TETESI ZA SOKA ULAYA

Manchester United wanajiandaa kutoa pauni milioni 140, ili kutengua kigezo cha uhamisho cha Neymar, 23 anayeichezea Barcelona, baada ya mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua (Le Sport10), Manchester United watamruhusu kiungo wao Nick Powell, 21 kwenda kwa mkopo katika timu moja ya ligi daraja la kwanza (Sun), Southampton hawatomuuza Sadio Mane, 23 au Victor Wanyama, 24 katika dirisha la usajili ya Januari (Times),

Watu 8 Wakiwemo Polisi Wafariki Dunia Kwa Kusombwa na Maji Kibaigwa Mkoani Dodoma



WATU 8 wamefariki dunia katika ajali iliyosababishwa na gari kusombwa na maji huku watu 6 wakiwa wa  familia moja.

 Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma, Davidi Misime amesema majira ya saa tatu usiku Jumapili, wananchi wa Kibaigwa walitoa taarifa jeshi la polisi kwa madai kwamba kuna gari limesombwa na maji na limetumbukia katika mkondo wa maji.

Shilole ajuta kuchora tatuu za Mziwanda kifuani kwake

Shilole ameapa kutorudia tena kuchora tattoo yenye jina la mpenzi wake.
Hivi karibuni muimbaji huyo alilazimika kuifuta tattoo ya jina la aliyekuwa mpenzi wake, Nuh Mziwanda.
Shilole amesema kujichora tattoo ya jila Nuh kumemharibia issue kibao.
“Tattoo hapa ni empty,” aliambia 255 katika kipindi cha XXL cha Clouds FM Jumatatu hii.

Saturday 2 January 2016

Mhubiri wa Kishia anyongwa Saudi Arabia

Sheikh Nimr al-NimrFamilia ya Sheikh Nimr al-Nimr inasema maandamano yake yalikuwa ya amani
Saudi Arabia imemuua mhubiri maarufu wa dhehebu la Kishia Sheikh Nimr al-Nimr, wizara ya masuala ya ndani imesema.
Mhubiri huyo ni miongoni mwa watu 47 waliouawa baada ya kupatikana na makosa yanayohusiana na ugaidi, imesema kupitia taarifa.
Sheikh Nimr aliunga mkono sana maandamano dhidi ya serikali yaliyochipuka mkoa wa Mashariki mwaka 2011, ambako Washia walio wengi walilalamikia kutengwa.

Friday 1 January 2016

Magari ya kibinafsi kuzuiwa kuingia Delhi

DelhiMagari ya kibinafsi yamekuwa yakiongezeka sana Delhi
Wasimamizi wa mji mkuu wa India, Delhi wameanza kuzuia baadhi ya magari ya kibinafsi kuingia mjini ili kupunguza uchafuzi wa hewa.
Magari ya kibinafsi yenye nambari za usajili zinayogawika na mbili bila masalio (namba shufwa) na yale yenye nambari zisizogawika na mbili (namba witiri) zitakuwa zikiruhusiwa mjini siku tofauti.
Mpango huo utafanyiwa majaribio kwa kipindi cha wiki mbili, na unatarajiwa kuzuia magari milioni moja kuingia mjini kila siku.