Friday 21 July 2017

Mawakili Kigali walaani kukamatwa Rais wa wanasheria Tanganyika, Tundu Lissu

Baadhi ya Mawakili jijini Kigali wamekosoa kitendo cha Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar Es Salaam cha kumkamata rais wa chama cha wanasheria Tundu Lissu ambaye alikuwa njiani kuelekea jijini humo kuhudhuria mkutano.
Tundu Lissu ni Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), amekamatwa leo, Alhamisi, Julai 20 katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA)  akielekea Kigali, Rwanda  kwenye kikao cha Halmashauri ya EALS kinachoanza kesho.
”Huu ni mpango wa kumdhoofisha, kwanini asingekamatwa jana?” amehoji wakili wa kujitegemea Rwebangiza Kiondo kutoka Tanzania, ambaye yupo jijini humo kwa shughuli za kufuatilia uchaguzi wa Rwanda.
Wakili Rwebangiza ameiambia BBC, kuwa Polisi wanatumia nguvu nyingi kupambana na Mwanasheria huyo ambaye alikuwa akitekeleza majukumu yake.
”Unamkamata Wakili akiwa katika pilika za kutekeleza wajibu wake, tena kwa kumshtukiza utafikiri ni jambazi anayetafuta, sikatai kwamba huenda pana hoja lakini kwanini umshtukize, mtu ambaye ni mbunge?”

magazeti ya leo tarehe 21.7.2017


Monday 17 July 2017

TETESI ZA USAJILI LEO TAREHE 17/7/2017

Kulingana na gazeti la Sky Sports Klabu ya chelsea inataka kukamilisha dili la kumsajili mshambuliaji wa Borussia Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang , katika harakati hizo chelsea imeongeza dau lake kutoka paundi milion 65 hadi kufikia paundi ilion 70 kuhakikisha wanapata saini ya mchezaji huyo baada ya kumkosa Romeu Lukaku aliyetua Man U .

Thursday 13 July 2017

Ajira mpya 10,184 kuziba waliachishwa kazi kwa vyeti feki

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais anayeshughulikia Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki
OFISI ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imetangaza kutoa vibali vya ajira 10,184 ili kuziba nafasi zilizoachwa wazi na watumishi wa umma waliobainika kughushi vyeti vya elimu, imefahamika.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Rais, Utumishi, Florence Temba, ilieleza kuwa agizo hilo linazihusu Mamlaka za Serikali za Mitaa, Sekretarieti za Mikoa, Wakala wa Serikali, pamoja na Taasisi na Mashirika ya Umma.
Ilimnukuu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angela Kairuki akitoa agizo hilo wakati akizungumza katika kikao kazi na watumishi wa Umma wa Wilaya ya Kigamboni mkoani Dar es Salaam jana.
“Mgawanyo wa vibali vya ajira umezingatia upungufu uliojitokeza baada ya kukamilika kwa zoezi la uhakiki, vipaumbele vya Taifa kwa sasa na upatikanaji wa watumishi kutoka katika soko la ajira,” alisema Kairuki.

Wednesday 12 July 2017

Tetesi za usajili leo tarehe 12.7.2017



Klabu ya Chelsea iliyo na maskani yake jiji la London imetuma ofa ya paund million 65 kwaajili ya kumsajili mshmbuliaji wa Borusia Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang raia wa Gaboni.
Meneja wa Chelsea Antoni Conte ametuma ofa hiyo baada ya kukosa saini ya aliyekuwa mchezaji wa Everton Romeo Lukaku ambaye sasa amejiunga na mahasimu wao Manchester United jumatatu ya wiki hii. Mpango wa kumsajili mshambuliaji huyo uekuja baada ya Chelsea chini ya meneja wake Conte kuonekana hana mpango na Diego Costa kwa msimu ujao ,Kwa Upande wa Dortmund wamefungua milango kwa mchezaji huyo kuuzwa , ripoti kutoka gazeti la “The Sun ” zineleza kuwa Pierre-Emerick Aubameyang anatamani sana kucheza ligi ya Uingereza. Aubemeyang aliibuka mpachikaji bora wa magoli katika ligi ya ujerumani msimu wa 2016/17, PSG na AC MILLAN pia zinafuatilia saini ya mchezaji huo kwa karibu zaidi

Tuesday 11 July 2017

MCHUNGAJI :Ni rahisi kufanya ngono na walokole kuliko wasio walokole



MCHUNGAJI WA KANISA LA KIPENTEKOSTE AMESEMA KUWA NI RAHISI KUFANYA NGONO NA WASICHANA WANAOKWENDA KANISANI KULIKO AMBAO HAWAENDI KANISANI.


Mchungaji wa Kanisa la Kipentekoste huko Afrika Kusini amesema kuwa ni rahisi sana kwa mhubiri kufanya ngono na wasichana wanaokwenda kanisani kuliko ambao hawaendi kanisani.
Mchungaji Benard Pumalaka amesema hayo Jumatano iliyopita baada ya kuokoka.
Amesema kuwa wengi wanaojiita "manabii" ni maarufu kwa ngono na wasichana na wake za watu.
Bernard alisema "kabla sijawa mchungaji wa Pentekoste, nilikuwa nimelala na watu wawili tu-mke wangu, na mwanamke mwingine mmoja tu.
Lakini nilipopata uchungaji nimelala na wanawake zaidi ya 200 ktk miaka kumi! Na nimepata utajiri mkubwa kwa kuwadanganya waumini wangu.
Nimejipatia fedha nyingi,magari na nyumba kwa kuwahadaa waumini wangu.Hakika sikuwa na Yesu ndani mwangu."

Monday 10 July 2017

Ngeleja arejesha hela alizopewa na Rugemalira

Mbunge wa Sengerema na waziri wa zamani wa Nishati na Madini, William Ngeleja (kushoto) akionesha nakala ya risiti aliyokabishiwa na mamlaka ya Mapato nchini (TRA) baada ye kurejesha serikalini kiasi cha Sh40.4 milioni alizopewa kama msaada toka kwa mfanyabiashara James Rugemalira wa Kampuni ya VIP Engeneering and Marketing Ltd. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari, Zamaradi Kawawa.

Thursday 6 July 2017

JAY-Z athibitisha mamake mzazi ni mpenzi wa jinsia moja

JAY-Z na mkewe BeyonceMsanii wa muziki wa Rap JAY-Z ameonekana kuthibitisha kuwa mamake ni mpenzi wa jinsia moja
Kulingana na maneno ya wimbo wa albamu yake 4:44, msanii huyo alisema:Mama alikuwa na watoto wanne lakini ni mpenzi wa jinsia moja licha ya kujifanya kuwa muigizaji.
Haijalishi kwangu iwapo ni mume ama mke nataka kukuona ukifurahi baada ya chuki zote.
Mapema katika kipindi chake chote cha kazi ya muziki JAY-Z aliandika nyimbo zilizokuwa na maneno ya watu wa mapenzi ya jinsia moja lakini akawacha kurekodi nyimbo zenye maneno hayo
Maneno hayo ya muziki yapo katika wimbo unaoitwa Smile ambao pia unashirikisha picha ya mamake Gloria Carter akisoma shairi.

Klabu ya Arsenal imekamilisha usajili wa mshambuliaji Alexandre Lacazette

Klabu ya Arsenal imekamilisha usajili wa mshambuliaji Alexandre Lacazette toka timu ya Lyon kwa dau la pauni Milioni 52.6 na kuvunja rekodi ya usajili ya timu hiyo.
Usajili wa kiungo wa Kijerumani Mesut Ozil ndio ulikua usajili wa bei ghali zaidi klabuni hapo aliposajiliwa mwaka 2013, kutokea Real Madrid kwa dau la pauni 42.4.
Lacazette amesaini mkataba wa miaka mitano kuwatumika washika mitutu hao wa London, mshambuliaji huyu atasafiri na timu wikiendi hii kuelekea Sydney kwa ajili ya michezo miwili ya kirafiki.
Msimu uliopita, Lacazette alikuwa mfungaji bora wa ligi ya Ufaransa alikozipasia nyavu mara 28 na ameshapiga jumla ya mabao 129 katika mechi 275 tangu alipoanza kuichezea timu ya kwanza msimu wa 2009/10.