Tuesday 30 June 2015

Mwandishi wa habari avunjwa Miguu Z'bar

Mwandishi wa Habari kwa jina Omar Ali mzaliwa wa Mkoani Kangani kisiwani Pemba, jana mida ya asubuhi ameshambuliwa na kupigwa vibaya sana na jeshi la Polisi Zanzibar na kutupwa maeneo ya Maisara mjini Zanzibar.

Mwandishi huyu alikuwa anachukua habari kutoka kituo cha uandikishaji dafatari la kudumu maeneo ya Migombani Zanzibar na polisi hao inasadikiwa walisema ni mwandishi wa Chama cha Wananchi CUF na ndipo walipomshika na kuanza kumpiga vibaya sana na kumvunja miguu kama anavyoonekana kwenye picha akiwa hospital mahutui miguu ikiwa imevujika.

Ikumbukwe:
Matukio haya yanakuja baada ya wananchi wa Zanzibar kuhakikisha kila kituo hawezi kuandikishwa mtu ambaye hahusiki kama ambavyo tumeona na kuskia kupitia vyanzo mbali mbali mpango wa CCM kupeleka mamluki visiwani Zanzibar kujiandikisha kwaajili ya kukiokoa Chama cha Mapinduzi hasa Zanzibar ambako kuna kila dalili kungoka madarakani Oktoba mwaka huu

Arsenal yamsainisha Peter cech kwa mkataba wa miaka 4

Petr Cech akionyesha jezi yake alipojiunga na timu ya Arsenal ya jijini London, Uingereza akitokea Chelsea pia ya London
Hatimaye yametimia kwa Arsenal kupata saini ya mlinda mlango Petr Cech kutoka Chelsea kwa kitita cha pauni milioni kumi.
Mlinda mlango huyo wa kimataifa kutoka Jamhuri ya Czech, ambaye amecheza zaidi ya mechi 400 katika misimu 11 akiwa na timu ya Chelsea, amejiunga na Arsenal the Gunners kwa mkataba wa miaka minne.
Cech, mwenye umri wa miaka 33, alicheza mechi saba tu msimu uliopita baada ya nafasi yake kunyakuliwa na mlinda mlango kutoka Ubelgiji Thibaut Courtois.

Monday 29 June 2015

Kitu cha ajabu cha Mmulika messi Usoni akiwa Uwanjani

Messi na timu yake ya taifa wamefanikiwa kuingia nusu fainali ya Copa America hayo tuliyajua baada ya mechi kuisha, tuliyoyajua  ni kuhusu Messi kumulikwa na kitu cha kijani ambacho kitajwa kama “green laser” ambapo miale hiyo ilipiga sehemu ya mbele ya kichwa chake.

Wanajeshi 60 wa Burundi wauawa na al shabaab

Wanajeshi 60 wa Burundi wauawa SomaliaWanajeshi 60 wa Burundi wauawa na al shabaab, taasisi za kiraia zalazimisha kuahirishwa kwa uchaguzi ili kuomboleza
Wanajeshi 60 wa vikosi vya kulinda amani nchini Somalia kutoka Burundi wauawa katika shambulio lililoendeshwa na wanamgambo wa al shabaab.
Kutokana na shambulio hilo wanaharakati wa asasi za kiraia wametoa wito kwa serikali kuahirisha tarehe ya uchaguzi wa wabunge unaotarajiwa kufanyika Jumatatu Juni 29 ili kuomboleza vifo vya wanajeshi hao waliouawa na wanamgambo wa al shabaab.

Wahamiaji haramu zaidi ya 50 wazuiwa kujiandikisha

Waziri wa Mambo ya Ndani, Mathias Chikawe.ZAIDI ya wahamiaji haramu 50 wanaoishi katika kijiji cha Tamau wilayani Bunda, mkoani Mara, akiwemo mwenyekiti wa kijiji hicho wamezuiwa kujiandikisha kwenye daftari hilo.
Ofisa uhamiaji wa Mkoa wa Mara, Ally Dady jana amethibitisha kuzuiwa kwa watu hao wanaodaiwa kuwa ni raia wa nchi jirani Kenya. Dady alisema taratibu za kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria watuhumiwa hao zinafanyika na kuongeza kuwa baadhi yao, wapo ambao walikamatwa wakiwa tayari wamekwishajiandikisha katika daftari hilo.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, waliobainika kuwa ni wahamiaji haramu ni pamoja na mwenyekiti wa kijiji hicho, John Seda, ambaye anatafutwa baada ya kutoroka.
Aidha, ilielezwa kuwa wale ambao tayari walikuwa wamekwishajiandikisha katika daftari hilo, wameamriwa kurudisha vitambulisho hivyo kwa ofisa mtendaji wa kijiji na wa kata hiyo ya Kunzugu.
Ilidaiwa kuwa tayari watu hao wamepewa fomu maalumu ya kujieleza na ofisi ya uhamiaji wilayani hapa, ambapo vyanzo vya habari vinasema kuwa wahamiaji hao wamo askari polisi kutoka nchini Kenya ambao wanaishi kijijini hapo kinyume cha sheria.
Aidha, vyanzo hivyo vya habari vimedai kuwa watu hao wanaishi kijijini hapo kinyemela na kwamba mwenyekiti huyo aliyechaguliwa katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliopita alitumia mbinu nyingi ya kupata uongozi huo ikiwa ni pamoja na kutoa rushwa.
Pia vyanzo hivyo vinasema kuishi kijijini hapo kwa wahamiaji hao kwa kipindi chote hicho ni kutokana na viongozi wa serikali kuwahalalisha watu hao kuishi hapo baada ya kupewa kitu kidogo, yaani pesa, mbuzi na ng’ombe.
Hata hivyo, Kaimu Ofisa Mtendaji Bernard Methew alipotafutwa na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu, alisema kuwa hana taarifa yoyote juu ya jambo hilo na wala hakuna wahamiaji haramu kijijni hapo.
“Hizo habari umezipata wapi wewe, mbona mimi sijui….. kama ni uhamiaji nenda uwaulize huko huko” alisema Ofisa mtendaji huyo na kukata simu.

AU yajiweka kando uchaguzi Mkuu Burundi

Makao makuu ya Umoja wa Afrika, Addis Ababa,Ethiopia
Umoja wa Afrika umesema hautawapeleka waangalizi wake wa uchaguzi katika uchaguzi wa wabunge wa Burundi utakaofanyika Jumatatu kwa sababu masharti ya uchaguzi huru na wa haki hayajazingatiwa.
Vyama vya upinzani vimesusia uchaguzi wakipinga uamuzi wa Rais Pierre Nkurunziza wa kugombea muhula wa tatu katika uchaguzi wa rais mwezi ujao.

Paka aliyehudumu kama mkuu wa kituo cha reli aaga dunia na Kuzikwa kiheshima

Paka azikwa kwa hafla ya kufana Japan
Paka mmoja wa Japani ambaye alipata umaarufu alipofanywa kuwa mkuu wa kituo cha reli, amefariki, na waombolezaji wengi wamejitokeza.
Wakuu na washabiki walihudhuria mazishi ya paka huyo, katika kituo cha reli, ambako alitumika.
Paka huyo aliyejulikana kwa jina ''Tama'' ambaye alipatikana akiranda randa katika kituo cha reli cha Kishi miaka minane iliyopita kabla yake kutawazwa kuwa meneja wa kituo hicho,
aliaga dunia majuzi kutokana na umri wake mkubwa wa miaka 16.
Tama aliishi katika kituo hicho akiwa amevalia sare rasmi ya afisa mkuu wa kituo cha reli na kuibuka kuwa kivutio kikubwa cha watalii.

Sunday 28 June 2015

Paraguay yaiondoa Brazil


Paraguay imejikatia tikiti ya nusu fainali ya mchuano wa Copa America baada ya kuilaza Brazil katika hatua ya robo fainali.
Paraguay ilijikatia tikiti hiyo baada ya kuilaza Brazil mabao 4-3 kwa mikwaju ya penalti.
Timu hizo zilikuwa zimetoka sare ya 1-1 katika muda wa kawaida.
Paraguay sasa itakabiliana na Argentina katika nusu fainali.

Yanga yabanwa Mbavu na Sport club Villa

Mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara timu ya Yanga wameshindwa kutamba mbele mabingwa wa kombe la FA nchini Uganda timu ya Sports Club Villa baada ya mabingwa hao kulazimishwa sare ya bila kufungana kwenye mchezo wa kirafiki wa kimataifa wa hisani ulioandaliwa na taasisi ya Numbani Kwanza kwa ajili ya kuchangia watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi uliomalizika muda mfupi kwenye uwanja wa Taifa.

Winga wa Yanga na timu ya Taifa Simon Msuva alikosa penati baada ya yeye mwenyewe Msuva kufanyiwa madhambi na golikipa wa Sports Club Villa wakati alipopata nafasi ya kwenda kufunga na mwamuzi wa mchezo huo kuamuru ipigwe penati lakini penati hiyo iliota mbawa baada ya Msuva kuipaisha juu.

Mchezo huo kwa upande wa Yanga ulikuwa ni sehehemu ya maandalizi kwa ajili ya michuano ya Kagame ambayo inatarajia kuanza kutimua umbi mapema mwa mwezi Julai ikishirikisha vilabu bingwa vya Afrika Mashariki na Kati.

Kinacho msababisha wema Kubadili wanaume chajulikana

IMEBAINIKA! Kufuatia tabia yake ya kubadili wanaume, mrembo asiyeishiwa matukio Bongo, Wema Isaac Sepetu imefahamika kuwa chanzo cha yote ni kusumbuliwa na ugonjwa ujulikanao kitaalamu kwa jina la Sex Maniac.

Wema Sepetu na Diamond.

Akizungumza na gazeti hili, mtaalam wa masuala ya utabiri na nyota, Maalim Hassan Yahya alisema kwamba suala la Wema kubadili wanaume kila mara si kulogwa bali anasumbuliwa na ugonjwa huo ambao mtu akiwa nao kila wakati anawaza mapenzi na raha yake ni kufanya tendo la ndoa.

Maelfu watirirka dar kumlaki Lowasa, Kingunge atia sain kumdhamini Lowasa

WAZIRI  Mkuu wa zamani, Edward Ngoyai Lowassa amepata udhamini wa kishindo katika mkutano uliofanyika jana  katika ofisi kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kinondoni.

Lowassa alipata udhamini huo baada ya wanachama kujitokeza katika ofisi za Makao Makuu ya CCM ya Wilaya ya Kinondoni, Mkwajuni, Dar, ambapo alipata zaidi ya wadhamini  212,150 huku akisema Dar  imevunja  rekodi  ya mikoa yote ya Tanzania.

Akizungumza na maelfu ya wananchi waliofika katika mkutano huo Lowassa alisema kuwa amefurahishwa na watu waliojitokeza kumdhamini kwa kishindo kikubwa na hivyo hatavunjwa moyo  na maneno ya watu yanayovumishwa  kuwa anawapatia fedha ili wafike kwenye mkutano wake

Jela siku moja kwa kukojoa hadharani

Siku 1 jela kwa kukojoa hadharani India
Watu 109 wamehukumiwa kifungo cha siku moja jela kwa kukojoa hadharani huko India.
Polisi waliwakamata takriban watu 109 kwa kukojoa katika vituo vya usafiri wa umma na reli.
Wale wote waliokamatwa wanatuhumiwa kwa kupatikana na hatia ya kukojoa nje ama ndani ya vituo vya reli mjini Agra Kaskazini mwa India .
Waliokamatwa watahukumiwa kifungo cha saa 24 korokoroni ama walipe faini ya kati ya dola mbili na kumi au vyote.
nullWaliokamatwa watahukumiwa kifungo cha saa 24 korokoroni ama walipe faini ya kati ya dola mbili na kumi au vyote.
Maafisa wa afya ya umma wanasema walifanya operesheni hiyo kwa ghafla ilikukabili uvundo wa mkojo unaoathiri afya ya mamilioni ya watu wanaotumia huduma hiyo ya reli nchini India.
Mkuu wa polisi katika eneo hilo GRP, Gopeshnath Khanna aliyeongoza operesheni hiyo anasema kuwa itaendelea hadi wahindi wanaolaumiwa kwa kuharibu mazingira kwa kutema mate ukutani baada ya kutafuna thambuu na tumbako iliyowekwa rangina kukojoa katika maeneo ya umma watakapo badili tabia zao.
Aidha wasafiri wa reli wanasemekana kupigwa na harafu mbaya ya mkojo pindi wanapoingia ndani ya vituo hivyo.
nullOperesheni hii ni sehemu ya kampeini ya Waziri mkuu mpya Narendra Modi ya kuimarisha afya ya umma al maarufu 'Swachh Bharat.
Operesheni hiyo ni sehemu ya kampeini ya waziri mkuu mpya wa India Narendra Modi ya kuimarisha afya ya umma al maarufu 'Swachh Bharat.
Waandishi wa habari katika eneo hilo la Agra wanasema hii ndio mara ya kwanza kwa maafisa wa kulinda afya ya umma kwa ushirikiano na serikali ya majimbo kuwakamata vikojozi.
Takwimu za afya nchini humo zinaonesha kuwa takriban watu milioni mia sita 600m ama nusu ya raia wa India hawana vyoo.

Raia 47 wa kigeni wakuliwa mateka waokolewa huko Sudan

Raia 47 wa kigeni waliochukuliwa mateka waokolewa SudanKikosi cha usalama chapambana na kundi la wahaini wa biashara haramu ya binadamu nchini Sudan

Kikosi cha usalama kimeripotiwa kuwaachilia huru raia 47 wa kigeni waliokuwa mikononi mwa wahaini wa biashara haramu ya binadamu katika eneo la mashariki mwa Sudan.
Mkuu wa polisi mkoani Kassala, Jenerali Omar Al Mukhtar, alitoa maelezo na kuarifu kuachiliwa huru kwa mateka hao baada ya mapambano makali kati ya kikosi cha usalama na watu 10 waliojihami kwa silaha.
Al Mukhtar alifahamisha kwamba mateka hao walioachiliwa huru, wote walikuwa ni wanaume kutoka nchi ya Eritrea na Ethiopia.

Polisi wakamata washukiwa wawili wa ugaidi katika eneo la mpaka wa Kenya na Tanzania

Washukiwa wawili wa ugaidi watiwa mbaroni nchini KenyaPolisi wakamata washukiwa wawili wa ugaidi katika eneo la mpaka wa Kenya na Tanzania

Polisi nchini Kenya wameripotiwa kuwakamata watu wawili wanaoshukiwa kujihusisha na kundi la Al-Shabaab katika eneo la mpaka wa Tanzania.
Maafisa wa polisi waliwatia mbaroni washukiwa wawili wa ugaidi waliokuwa wakijaribu kuingia nchini Kenya kwa lengo la kuwachukuwa wanawake wanaotaka kujiunga na kundi la Al-Shabaab.
Waziri wa Ulinzi nchini Kenya Joseph Nkaissery, alitoa maelezo na kuarifu kwamba washukiwa hao wawili wa ugaidi waliowekwa chini ya ulinzi watafikishwa mahakamani wiki ijayo.

Vifaa vya uchaguzi wachomwa moto mkoani Kirundo kaskazini mashariki mwa Burundi

Vifaa vya uchaguzi vyachomwa moto BurundiWatu waliobebelea silaha walivamia kituo kimoja kilichokuwa kimehifadhiwa vifaa vya uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Jumatatu nchini Burundi.

Shambulio hilo lilifanyika usiku wa Ijumaa ambapo masanduku 59 yameripotiwa kuchomwa moto na watu hao.
Kwa mujibu wa taarifa iliotolewa na mwenyekiti wa wilaya, Marineau Hitimana alifahamisha kuwa mapambano bain aya watu hao na askari Polisi ilichukuwa muda wa dakika takriban 10.

Simba warajea Rwanda baada ya miaka 20

Simba warejea Rwanda baada ya miaka 20
Mfalme wa mwituni Simba ,atarejea Rwanda kwa mara ya kwanza tangu aangamie wakati wa mauaji ya kimbari mwaka wa 1994
Maafisa wanaowalinda wanyama pori wa Rwanda, wanasema kuwa simba watarudi nchini humo siku ya jumatatu kwa mara ya kwanza, tangu walipoangamizwa baada ya mauaji ya kimbari,ya mwaka wa 1994.
Simba wawili dume, na majike watano, wanasafirishwa kutoka mbuga ya wanyama ya Kwazulu Natal, Afrika Kusini, na Jumatatu watawasili Rwanda kwa ndege.
nullSimba hao 7 wanasafirishwa kutoka mbuga ya wanyama ya Kwazulu Natal, Afrika Kusini.
Simba hao saba watawekwa kwenye karantini kisha waruhisiwe kutembea huru katika mbuga ya wanyama.
Wanyama hao watapelekwa katika mbuga ya taifa ya Akagera.
Maafisa wakuu huko Rwanda walisema, kurejeshwa tena kwa simba nchini Rwanda ,ni Kilele cha juhudi kubwa ya kuhifadhi mazingira katika mbuga hiyo na kwa taifa zima kwa jumla.
nullSimba hao ni sehemu moja ya kampeini ya kuhifadhi Mazingira nchini Rwanda
Baada ya mauaji ya kimbari mwaka wa 1994, watu wengi waliokimbia makwao waliikalia mbuga hiyo ya Akagera.
Simba waliokuwa humo walikimbia au kuuawa, huku watu wakijaribu kulinda mifugo yao na maisha yao.

Uchaguzi mkuu kufanyika kesho Nchini Uganda

Balozi wa Burundi katika umoja wa mataifa amekariri kuwa uchaguzi utaendelea mbele Jumatatu licha ya shinikizo uahirishwe
Balozi wa Burundi kwenye umoja wa mataifa amesema kuwa uchaguzi utaendelea jinsi ulivyopangwa siku ya jumatatu licha ya ombi kutaka uahirishwe kutoka kwa katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban Ki moon.
Ban anasema kuwa ana wasiwasi kuhusu hali ya usalama nchini Burundi kufuatia mzozo wa kisiasa unaoendelea huko.

Blatter:Sikujiuzulu kama rais wa FIFA

Blatter:Sikujiuzulu kama rais wa FIFA
Rais wa shirikisho la soka duniani Sepp Blatter amekariri kuwa hakujiuzulu kama rais wa shirikisho hilo.
Kiongozi huyo mswissi mwenye mri wa miaka 79 alikuwa amedhaniwa kujiondoa madarakani juni tarehe 2 kufuatia kashfa kubwa ya ufisadi ulajirushwa na matumizi mabaya ya madaraka iliyokumba shirikisho lake lakini sasa anaonesha dalili za kubadili mtazamo huo.
Blatter ambaye ameiongoza FIFA kwa miaka 17 alikuwa ametangaza kuwa atajiondoa mbele ya kamati kuu ilikufanyike uchunguzi wa kina katika FIFA lakini sasa ameikumbusha jarida moja la uswisi BLICK kuwa yeye ndiye rais wa FIFA na kuwa aliweka hatima yake mikononi mwa kamati kuu ya shirikisho katika mkutano wa dharura.

Friday 26 June 2015

Serikali yakili kushindwa kudhibiti wahamaiji haramu Kyerwa na Karagwe mkoani Kagera.

Viongozi wa vyama vya kisiasa, maafisa uandikishaji na kamati za ulinzi na usalama wilaya ya Karagwe na Kyerwa mkoani Kagera zimekili kushindwa kudhibiti wimbi la watu wanaosadikiwa kuwa wahamia haramu kutoka nchi ya Burundi, Rwanda na Uganda kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura BVR wakishawishi baada ya watendaji wa serikali za vijiji, vitongoji na mawakala kuwapatia rushwa ya fedha na mifugo.
Wamebainisha hayo siku chache baada ya kukamilika kwa zoezi la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura BVR katika mkoa wa Kagera ambapo wilaya ya Kyerwa imevuka lengo kwa kuandikisha watu wengi zaidi wakiwemo wahamiaji haramu zaidi ya 4000 huku wilaya ya Karagwe ikiandikisha kwa asilimia 97 na kubainisha kwamba wahamiaji haramu walioweka makazi katikati ya mapori na misitu ya hifadhi ya taifa walivamia zoezi la BVR kwa lengo la kujiandikisha kinyume cha sheria za nchi.

Magonywa ya ngono yaongezeka kwa wapenzi wa jinsia moja

Wapenzi wa jinsia moja
Maradhi ya zinaa yanayosambazwa miongoni mwa wapenzi wanaume wa jinsia moja inatamausha.
Haya ni kwa mjibu wa shirika la afya ya umma nchini Uingereza.
Takwimu za mwaka 2014 zinanonesha kuwa asilimia 46 ni maambukizi ya kaswende, ilihali asilimia 32 ni maambukizi ya kisonono, huku maambukizi ya maradhi ya "chlamydia" ikiwa kwa asilimia 26.
Ripoti hiyo inasema kuwa kumekuwa na viwango vya juu vya visa ya kufanya ngono bila ya kutumia mipira ya kondomu, hali iliyozidisha kusambaa zaidi kwa maambukizi ya virusi vya HIV miongoni mwa wanaume hao.

Thursday 25 June 2015

Polisi awa baba wa mtoto baada ya ajali

Polisi awa baba baada ya ajali
Afisa mmoja wa polisi nchini Marekani alilazimika kuwa mzazi baada ya kumpata mtoto akiwa hai kufuatia ajali mbaya iliyosababisha kifo cha babake.
Mauti yaliikumba familia hiyo ya baba mama na watoto wanne mjini Colorado Marekani.
Hata hivyo mtoto wao wa miaka miwili alinusurika bila hata ya kuchubuka !
Mtoto huyo wa kike alipatikana na makundi ya waokoaji akiwa analia huku babake akiwa ameaga dunia kufuatia ajali hiyo.

Nyalandu; CCM jiandaeni kwa ushindi

Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu.WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu amesema CCM ni chama pekee nchini ambacho kimefanikiwa na kinaendelea kupanua wigo wa demokrasia.
Nyalandu ni miongoni mwa wanachama wa chama hicho nchini waliotia nia ya kugombea nafasi ya urais katika uchaguzi ujao, aliyasema hayo jana wakati anazungumza na viongozi na wanachama wa CCM wilayani Masasi waliojitokeza kumdhamini.
Alisema hakuna tunu bora nchini zaidi ya kuendeleza umoja, amani na mshikamano uliopo hivi sasa ndani ya chama hicho huku akitoa mwito kwa wagombea wenzake ndani ya chama kuacha kukitia madoa chama na hata wao wenyewe, kwani kwa sasa CCM inahitaji umoja.

Wednesday 24 June 2015

Kondomu inayotambua maambukizi ya Zinaa

Kondomu inayotambua maambukizi ya zinaa
Wanafunzi katika shule moja nchini Uingereza wameunda mipira ya kondomu inayowaonya watumiaji wanapojamiana na mtu aliyeambukizwa maradhi ya zinaa.
Kondomu hiyo inabadili rangi pindi inapokutana na majimaji ya mtu anayeugua maradhi ya zinaa.
Kondomu hiyo S.T.EYE inaweza kutambua maambukizi ya Chlamydia Kaswende na Kisonono.
Kulingana na wanafunzi hao kondomu hiyo inabadili rangi tofauti kulingana na bakteria iliyopo.
Uvumbuzi huu ni wa Daanyaal Ali, 14, Muaz Nawaz, 13 na Chirag Shah, 14, ambao ni wanafunzi katika shule ya Isaac Newton Academy iliyoko Ilford, Essex, nchini Uingereza.
nullKondomu hiyo S.T.EYE inaweza kutambua maambukizi ya Chlamydia Kaswende na Kisonono.
''tuliazimia kumpa onyo mtumiaji wa mipira hii kuwa mpenzi wake yuko salama ama ni mgonjwa bila ya wasiwasi wa kupimwa hospitalini''.
Wanafunzi hao tayari wametunukiwa, tuzo la ubunifu la ''the TeenTech'' .
Daanyall alisema kuwa "Walizindua kondomu hiyo ilikuifaidi kizazi kijacho''
''Kwa hakika swala la usalama wa mpenzi wako ni swala la kibinafsi kwa hivyo ni swala linalopaswa kupewa kipaombele haswa ikifahamika kuwa tunawajibu wa kuchochea ngono salama bila ya kuwashurutisha wapenzi wetu kufika hospitalini bila wao wenyewe kukusudia''
nullWavumbuzi hao wanasema kuwa hiyo ni mojawepo ya njia salama ya kubaini usalama penzi lenyu
Wanafunzi hao waliwalitunukiwa pauni elfu moja pamoja na fursa ya kuzuru Kasri la Malkia wa Uingereza Buckingham Palace.
Muasisi wa kampuni ya ubunifu wa kiteknolojia, TeenTech, Bwana Maggie Philbin, alisema kuwa
"Ni wajibu wetu kama jamii kuchochea ubunifu unaopatikana madarasani kuchochewa na kupigwa msasa kwa minajili ya kuboresha maisha ya mwanadamu'

Liverpool imesajili mshambuliaji wa Brazil Roberto Firmino

Liverpool imesajili mshambuliaji wa Brazil Roberto Firmino
Klabu ya Liverpool imemsajili mshambuliaji wa Brazil Roberto Firmino kutoka klabu ya Hoffenheim kwa kanadarasi ya miaka mitano itakayogharimu pauni millioni 29.
Mkataba huo utaandamana na ukaguzi wa kimatibabu ambao utafanyika baada ya mchezaji huyo kurudi kutoka Chile ambapo amekuwa akiichezea Brazil katika michuano ya Copa America.

Mhe. Makinda ameahirisha kikao cha bunge kutokana na kifo cha mbunge wa Geita

Mhe. Makinda ameahirisha kikao cha bunge kutokana na kifo cha mbunge wa Geita Mhe Donald Max.
Spika wa bunge Mhe.Anna Makinda ameahirisha kikao cha bunge kutokana na kifo cha mbunge wa jimbo la Geita kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Mhe Donald Kelvin Max kilichotokea katika hospitali ya taifa ya Muhimbili juni 23 mwaka huu.
Akiahirisha kikao cha bunge Mhe.Makinda amesema marehemu amekuwa akiugua kwa muda mrefu hali iliyopelekea kulazwa hospitalini kwa kipindi kirefu ambapo amesema taratibu za mazishi zinafanywa na anatarajiwa kuzikwa jijini Dar es Salaam siku ya jumamosi ya Jun 27.

Wananchi washauriwa kutumia juhudi na umoja kujiletea maendeleo.

Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dr Reginald Mengi amesema Maendeleo ya Watanzania hayataletwa na watu wa nje, bali yataletwa na Watanzania wenyewe kwa kutumia juhudi na umoja wao.
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dr Reginald Mengi ameyasema hayo jijini Dar es salaam wakati akizindua rasmi uuzwaji wa hisa za Asasi ya kifedha ya YETU Microfinance P.L.C, ambapo alinunua hisa 40,000 zenye thamani ya shilingi milioni 20, ili kudhuhirishia imani yake kwa  asasi hiyo iliyoasisiwa na Watanzania.
 Dr Mengi pia amewahamasisha wajasiriamali kujitokeza kwa wingi kununua hisa za asasi hiyo, na kuwataka wajibidishe katika kuusaka ujajiri kwa njia zinazompendeza  Mwenyezimungu.

Malaria yaua watu nchini Guinea

Wafanyakazi wa sekta ya afya wakiuondoa mwili wa mtu aliyekufa kwa ebola.
Watafiti wa magonjwa wanasema kwamba janga kubwa la ugonjwa wa ebola nchini Guinea linazidi kuongeza idadi ya vifo vya watu wanaofariki dunia kwa maradhi ya malaria .
Utafiti huo,uliochapishwa katika jarida moja la magonjwa ya kuambukiza nchini humo,linakadiria kwamba watu wapatao elfu sabini na watano wanaougua ugonjwa wa malaria hawakupatiwa dawa, pengine kutokana na kufungwa kwa vituo vya afya,ama pengine wagonjwa walikuwa wana hofu kubwa ya kutafuta msaada wa kitabibu.

Ebola yaibuka mjini Freetown

Bango lenye elimu kwa umma Sierra Leone
Maofisa wa afya nchini Sierra Leone wamesema kwamba kuna wagonjwa wawili wapya wanaougua ugonjwa wa ebola na kwamba wamegunduliwa katika mji mkuu wa nchi hiyo Freetown.
Hapo awali ilidhaniwa kwamba mji huo ulikuwa hauna maambukizi ya ugonjwa huo,na hakukuwa na wagonjwa walioripotiwa hapo kabla kwa muda wa wiki kadhaa.
Naye msemaji wa kituo cha karantini cha taifa hilo amesema kwamba kulikuwa na wasiwasi mkubwa kwasababu vituo vyote vya karantini na vitendea kazi vyake vilikuwa vimefungwa mjini Freetown.
Na akaongeza kusema kwamba kuna shaka kuwa kutatokea maambukizi mapya kutoka katika eneo lenye msongamano wa makazi duni.

Mwalimu ashiriki ngono na wanafunzi wake

Mwalimu mmoja mkuu amekiri kufanya ngono na wavulana wawili wenye umri mdogo.
Anne Lakey, mwenye umri wa miaka 55, kutoka eneo la Stanley, katika kaunti ya Durham, amekanusha makosa 13 dhidi yake ya kufanya matendo ya aibu kwa kushikashika sehemu za siri wavulana wawili miaka ya themanini.
Lakini jaji katika mahakama ya Teesside Crown, alimpata na hatia ya makosa hayo yote baada ya kesi iliyochukua majuma mawili.
Mahakama ilisikiza ushahidi wa namna alivyokuwa akitenda matendo hayo ya kuudhi na aibu katika kipindi cha miaka mitatu mfululizo.
Atahukumiwa jela Jumatano wiki hii.

Mtunzi wa filamu ya Titanic afariki dunia

James Horner
James Horner, mtunzi nguli wa eneo maarufu kwa watu maarufu la Hollywood ambaye aliandika na kushinda katika tuzo za Oscar juu ya filamu maarufu ulimwenguni ya Titanic,amefariki dunia mjini California kutokana na ajali ya ndege akiwa na umri wa miaka 61.
James alipata mafunzo ya urushaji wa ndege,inaarifiwa alikuwa peke yake wakati alipopata ajali hiyo,na ndege binafsi ndogo ambayo alipata nayo ajali eneo la Kusini mwa Santa Barbara mwanzoni mwa wiki hii .
Mwandishi huyu na mtunzi wa tungo mbali mbali ametia mkono wake katika kazi tatu tofauti za filamu za msanii James Cameron , pamoja na filamu ya A Beautiful Mind, Braveheart, Troy na ile ya Apollo 13.katika utendaji kazi wake uliotukuka, James alipewa tuzo ya Oscar kwa filamu ya Titanic na wimbo uliotawala humo na nyinginezo .

Tuesday 23 June 2015

Jonas mkude atimkia Afrika kusini kwa majaribio

mkude-768x403
Kiungo wa Klabu ya Simba Jonas Mkude anatarajiwa kwenda Afrika Kusini  Alhamisi Juni 26 mwaka huu kwa majaribio ya wiki mbili katika Klabu ya Bidvest Wits.
Akiongea na tovuti ya Simba, Mkude alisema fursa hii ni adimu na anaamini akifanikiwa ataiwakilisha vyema Simba na Tanzania kwa ujumla. 
Akizungumzia pengo litakaloachwa ikiwa atafanikiwa majaribio alisema “pengo langu linaweza kuzibwa kwani Simba ina wachezaji nyota wanaojituma na wenye uwezo”

Puff Dadddy akamatwa kwa mashambulizi

Puff Dadddy
Mwanamuziki mashuhuri wa nyimbo za Hip hop P Diddy amekamatwa kwa kushukiwa kumshambulia mtu kwa silaha mjini Los Angeles.
Kisa hicho kinadaiwa kufanyika katika chuo kikuu cha California Jumatatu alasiri, mahala ambapo mwanawe wa kiume ni mmojawapo ya wachezaji katika timu ya soka ya Marekani.
Hayo ni kwa mjibu wa maafisa wa polisi.

Wanaovalia suruali za kubana waonywa

Suruali ndefu zinazobana zina madhara
Mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 35 alilazimika kutolewa ndani ya suruali ndefu aina ya Jeans, baada ya miguu yake kuvimba kupita kiasi.
Hayo ni kwa mjibu wa jarida la Neurology, ambalo huandika habari kuhusu upasuaji.
Alichuchumaa kwa muda mrefu sana ili kuondoa bidhaa ndani ya kabati alipokuwa akijiandaa kuhama nchini Australia.
Ilipofika jioni, miguu yake ilikuwa imekufa ganzi na akashindwa kutembea.

Joto kali lauwa watu zaid ya 700 huko Pakstan

Joto kali
Waziri mkuu nchini Pakistan Nawaz Sharrif ametaka hatua za dharura kuchukuliwa huku idadi ya watu waliofariki kutokana na wimbi la joto katika mkoa wa kusini wa Sindh ikifikia 700.
Mamlaka ya kukabiliana na majanga ya dharura NDMA imesema kuwa imepokea maagizo kutoka kwa Nawaz Sharrif kuchukua hatua za dharura.
nullJoto kali
Jeshi tayari limepelekwa katika eneo hilo kujenga vituo vya kukabiliana na joto hilo ili kuisaidia mamlaka hiyo.

Membe, Nikiwa rais ikulu nitazihamishiwa Chamwino

WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Bernard Membe, amesema kama CCM kitamteua kuwa mgombea urais na kushinda katika Uchaguzi Mkuu ujao, atahakikisha Ikulu na nyumba za wizara zote zinahamia Dodoma. 

Bw. Membe ambaye ni miongoni mwa wagombea urais ndani ya CCM, aliyasema hayo jana wakati akizungumza na wakazi wa mkoa huo na wana CCM waliojitokeza kumdhamini.

"Hili jambo nimelifikiria muda mrefu, hayati Mwalimu Julius Nyerere, alitumia nguvu na fedha nyingi kujenga Ikulu ya Chamwino hivyo nikiwa rais, nitahamia Dodoma.

Mbowe akishirikiana na wananchi kusafisha mji

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Freeman Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Hai (mwenye kofia katikati) akishirikiana na wananchi wa Lukeni, Kata ya Masama-Mashariki kufanya usafi katika Soko la Masama-Mula juzi, katika kampeni ya kutunza mazingira kwenye jimbo hilo iliyopewa jina la 'Keep Hai Clean' ikitumia gari maalum la kukusanyia taka lenye uwezo wa kubeba tani 32 za taka ambalo mbunge huyo alitoa msaada kwa wananchi wake hivi karibuni.

Polisi hatumwonei lema


Aidha alisema katika tukio la kurushiwa mawe mlinzi wake, Abdallah Mazengo alipigwa jiwe kichwani na kuzimia kwa masaa kadhaa, hata hivyo hali yake inaendelea vizuri.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Liberatus SabasKAMANDA wa Polisi mkoani Arusha, Liberatus Sabas, amesema kuwa tuhuma alizotoa Mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema si za kweli.
Kamanda huyo alisema madai kwamba polisi wanamuonea Lema kwa kumkamata na kumweka mahabusu wakati yeye siyo mhalifu siyo za kweli na kwamba yeye (Lema) ni chanzo cha vurugu katika uandikishwaji wa daftari la wapigakura.
Akizungumza jana kwa njia ya simu jana Sabas alisema Lema anasababisha vurugu kwa kutembelea maeneo ambayo watu wamejitokeza na kujiandikisha na kuanza kupiga hotuba kitu ambacho kinyume cha sheria.
Alisema Lema kama anataka kuhamasisha watu hatukatai, aende maeneo ambayo daftari bado halijafika akahamasishe na likifika aache wananchi wajiandikishe na siyo kuwafuata kwenye mistari na kuanza kupiga hatuba, siyo sahihi.
Alisema polisi hawawezi kuonea mtu wala yeye mbunge, isipokuwa likipata taarifa kama siku ya tukio ya Juni 20 alipokamatwa kuwa analeta vurugu na wananchi hawataki kumwona katika maeneo ya uandikishaji ndipo walipokwenda kumkamata.
Alisema siku ya tukio walipata taarifa toka kwa askari walioko doria kwenye kituo cha Osunyai kuwa kuna vurugu toka kwa mbunge na kuomba ulinzi uongezwe na askari wakapelekwa zaidi na kumtia mbaroni na wenzake 24 na kuwa jumla ya watuhumiwa 25 walikamatwa na siyo yeye aliyetoa taarifa Polisi kuomba ulinzi.
“Lema yeye anaongozana na kundi la watu toka maeneo tofauti na uandikishwaji, kitu ambacho siyo sahihi pia nacho kinakera baa- dhi ya watu,” alisema.
Hata hivyo uchunguzi dhidi ya tuhuma zake unaendelea na upelelezi ukikamilika atachukuliwa hatua stahiki.
Awali Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema, aliyekamatwa alilalamikia Polisi, kwa kumkamata na kumweka mahabusu masaa kadhaa juzi wakati akiwa kwenye kata ya Osunyai Manispaa ya Arusha, akizungukia waandikishwaji wa daftari la wapiga kura, ili kujionea hali halisi.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Lema alisema ameshangazwa na kitendo hicho kwani yeye ndiyo aliyewaita polisi ili kumsaidizi ulinzi, baada ya kuvamiwa kwa kupigwa mawe na kundi la vijana wanaosadikiwa kuwa wa kundi la mgombea ubunge wa chama cha CCM.
Alisema mara baada ya kupiga simu Polisi kuomba msaada polisi walifika kwa haraka, lakini badala ya kukamata vijana hao ambao walikuwa wakizuia watu kujipanga mstari kwa madai siyo wakazi wa maeneo hayo kwa madai wakazi wa maeneo hayo Wamasai na Waarusha, wakanikamata mimi na wafuasi wangu 25 na kutuweka mahabusu.
Alisema walikaa ndani Juni 20 mwaka huu, kuanzia saa 1:30 usiku hadi saa 4:00 usiku na kuwataka wajidhamini wenyewe, kisha kuwaachia.
Lema alisema yeye ni kiongozi na sheria inamtaka ahamasishe watu kujitokeza na kujiandikisha na inapobidi kutoa elimu, lakini, hapaswi kudhalilishwa kwa kuwekwa mahabusu kwa kejeli na dharau.
“Hawa watu wanaopita kwenye kata za wenyeji na gari aina ya Land Cruiser yenye namba T.122 ATR na wakati mwingine hubadilisha kibao na kusomeka T. 122 ABR, na kuwatoa watu kwenye mistari kwa madai siyo wakazi wa maeneo hayo wakati wameuza maeneo na watu wamechanganyikana, walipaswa wakamatwe, badala yake wanakamata mbunge na watu wake kuwa wanahamasisha fujo, hiyo siyo haki,” alisema.

Mwanamke mwingine ajitosa urais CCM

Kada wa CCM, Ritha Ngowi akikabidhiwa mkoba wa fomu za kuomba kuteuliwa kugombea nafasi ya Urais na Katibu wa NEC (Oganaizesheni), Dk Mohamed Seif Khatib katika Makao Makuu ya CCM, mjini Dodoma jana. (Picha na Fadhili Akida).IDADI ya wagombea wanaochukua fomu kwa ajili ya kuwania kuteuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) jana walifikia 39 baada ya mwanachama wake, Ritha Ngowi kuchukua fomu.
Ngowi, mkazi wa Dar es Salaam, anakuwa mwanamke wa tano kuchukua fomu, ambapo waliochukua fomu wa awali ni Balozi Amina Salum Ally, Waziri wa Katiba na Sheria Dk Asha-Rose Migiro, Dk Mwele Malecela na Monica Mbega.
Katika mkutano wake na waandishi wa habari alisema yeye ni msomi ambaye ana shahada ya Maendeleo ya Jamii na pia amepitia kozi mbalimbali katika ngazi za diploma na cheti. Alisema vipaumbele vyake vitakuwa ni kwenye sekta ya elimu na uchumi.
“Nimeguswa sana na kuamua kugombea nafasi ya Urais lengo langu kubwa ni kutaka kuboresha elimu na Uchumi” alisema.

Monday 22 June 2015

Vurugu za ibuka katika vituo vya kujiandikisha kupiga kura

Mbunge wa Arusha Mjini, Godbles Lema.MILIO ya risasi ilisikika katika vituo vya uandikishaji kura katika kata ya Sokoni One jijini hapa, baada ya kuibuka kwa vurugu zilizohusisha vijana wa Chadema na wenzao wa CCM, chanzo kikitajwa madai ya kuwepo kwa watu ambao sio wakazi wa eneo hilo kutaka kujiandikisha.
Vurugu hizo zilisababisha takribani watu 15 kukamatwa akiwemo Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema) ambaye hata hivyo baadaye aliachiwa huru. Alishikiliwa kuanzia saa 1:30 usiku hadi saa 4:00 usiku juzi.
Patashika hiyo ilichukua zaidi ya saa moja, kwani baadhi ya polisi waliokuwa na silaha za moto aina ya bastola walifyatua risasi hewani kwa lengo la kutawanya vurugu hizo, lakini hali ilikuwa mbaya zaidi hadi polisi walipoongezwa na kufanikiwa kutuliza ghasia hizo.
Wakati hayo yanatokea Lema alisisitiza kuwa kamwe hawezi kukubali kutohamasisha wananchi kwenda kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapigakura licha ya kudai kuwa, kundi la vijana wanaosadikiwa kuwa wa CCM wamempiga mawe sambamba na watu wengine waliojitokeza kujiandikisha katika kata mbalimbali.

ATM za kununulia maji za zinduliwa Kenya

Maji ya ATM nchini Kenya
Wakazi wa kitongoji duni cha Mathare katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi, sasa wanaweza kupata maji safi ya kunywa na kwa matumizi mengine.
Mpango unaoungwa mkono na serikali umezinduliwa kwenye mji mkuu wa Kenya Nairobi unaowawezesha watu wanaoishi kwenye mitaa ya mabanda kununua maji kwa kutumia kadi.