Saturday 20 June 2015

Zaidi ya sh.milioni 250 zilizotakiwa kutengeneza Barabara zimeliwa ikungi Singida.

Wananchi wa kijiji cha Ngongosoro katika wilaya ya Ikungi jimbo la Singida mashariki wamemuomba mbunge wao mheshimiwa Tundulisu,kufuatilia  fedha zilizo liwa zaidi ya shilingi milioni miambili hamsini ambazo zilitakiwa kutengeneza barabara yenye  umbali wa kilometa zaidi ya thelasini  kutoka isuna hadi kijiji kwao.
Wanachi hao pamoja na kumpogeza mbunge wao kusimamia kupinga michango ambayo siyo ya lazima na wao sasa wamekuwa huru kwa kutokamatwa ovyo na vyombo vya dola,wamesema barabara hiyo ambayo imetengenezwa kwa kiwango cha chini  ukilinganishwa na fedha zilizo tolewa,kutokana na ubovu wa barabara hiyo wamekuwa wakipatashida  kufuata huduma za afya na zingine makao makuu ya wilaya ya Ikungi. 
Akiongea kwenye mkutano wa hadhara na wananchi wa kijiji cha Ngogosoro mbunge wa jimbo la Singida mashariki  mheshimiwa Tundu Lisu amesema  pamoja na kufuatilia swala la barabara kuhakikisha fedha zilizo tolewa zinatumika ipasavyo, kukwama  kwa miradi ya maendeleo katika jimbo la singida mashariki ni kwa sababu ya madiwani wengi wa ccm kushindwa kuishindikiza halamashauri ya wilaya ya ikungi kutekeleza miradi ya maendeleo kama jinsi ilivyo pangwa.
 
Katika hatua nyingine Mhesimiwa Tundu Lisu amewataka wananchi kujitokeza kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapigakura,kwa kufanya hivyo itakuwa ndio njia pekee ya kuwatoa madarakani viongozi ambao hawatekelezi majukumu yao kwa ufanisi na wanaodidimiza maendeleo kwa  kumbatia vitendo vya rushwa.

No comments: