Wednesday 24 June 2015

Wananchi washauriwa kutumia juhudi na umoja kujiletea maendeleo.

Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dr Reginald Mengi amesema Maendeleo ya Watanzania hayataletwa na watu wa nje, bali yataletwa na Watanzania wenyewe kwa kutumia juhudi na umoja wao.
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dr Reginald Mengi ameyasema hayo jijini Dar es salaam wakati akizindua rasmi uuzwaji wa hisa za Asasi ya kifedha ya YETU Microfinance P.L.C, ambapo alinunua hisa 40,000 zenye thamani ya shilingi milioni 20, ili kudhuhirishia imani yake kwa  asasi hiyo iliyoasisiwa na Watanzania.
 Dr Mengi pia amewahamasisha wajasiriamali kujitokeza kwa wingi kununua hisa za asasi hiyo, na kuwataka wajibidishe katika kuusaka ujajiri kwa njia zinazompendeza  Mwenyezimungu.
Mapema Mkurugenzi wa Yetu Microfinance P.L.C  Bw. Altemius Millinga  alisema asasi ya fedha ya Yetu Microfinance P.L.C  imepata kibali kutoka Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana,  cha kuuza hisa zipatazo milioni 25 kwa shilingi  500 kila moja, katika kipindi cha kati ya Juni 18, 2015 na Julai 30, 2015. Kwa sababu hiyo amewahimiza wajasiriamali kuchangamkia hisa hizo, ambapo kima  cha chini cha ununuzi ni ni hisa 200 zenye thamani ya shilingi laki moja.
 
Wakati wa uzinduzi huo  wajasiriamali wawili Bi. Johari Mkonde  na Bi Lucia Kimamba walitoa ushuhuda wa jinsi walivyofanikiwa katika ujasiriamali wao.

No comments: