Saturday 20 June 2015

Shughuli za mazishi ya rais wa 9 wa Uturuki zafanyika

Mazishi ya rais wa 9 wa UturukiShughuli za mazishi za rais wa 9 wa Uturuki zilifanyika jana katika makaburi ya Ulusal na kuswaliwa katika msikiti wa Koca tepe. 
Katika shughuli za mazishi hayo wageni kutoka nje na ndani ya nchi walihudhuria akiwemo  rais wa Uturuki Reccep Tayyip Erdogan,Waziri mkuu Ahmet Davutoglu na viongozi wengine pia walihudhuria.
Rais wa Cypus alihudhuria sherehe za mazishi hayo na wawakilishi kutoka nchi mbalimbali kutoka nchi za nje.

Daktari wake ambaye alikuwa anamuhudumia , aliweka kofia ya Demirel juu ya kaburi lake kwa kumuenzi rais huyo.

Rais Recep Tayyip Erdogan, alisema kuwa Demirel alifanya huduma muhimu katika ngazi zote za siasa na serikali katika nusu karne ya uongozi wake.

No comments: