Friday 19 June 2015

Simba yasitisha swala la kumtangaza kocha mpya wa klabu hyo

Aliyekuwa kocha wa Simba Goran Kopunovic akitoa maelekezo kwa kiungo wa klabu hiyo Said Ndemla
Aliyekuwa kocha wa Simba Goran Kopunovic akitoa maelekezo kwa kiungo wa klabu hiyo Said Ndemla

Klabu ya soka ya ‘Wekundu wa Msimbazi’ Simba imeendelea kulipiga danadana suala la kumtangaza kocha mpya atakaechukua nafai ya Goran Kopunovic ambapo uongozi wa timu hiyo umesema unatarajia kumtangaza mapema mwanzoni mwa juma lijalo.
Afisa habari wa klabu hiyo Hajji Manara amewataka wanachama na mashabiki wa Simba kuendelea kuwa wavumilivu huhu akisema, tayari wameshampat kocha kilichobaki ni kumtangaza tu.
“Kocha tutamtangaza wiki ijayo, kwasababu tumeshampata, sisi wiki ijayo tutamtangaza rasmi. Jumamosi mimi natoa ‘press release’ nikishatoa tutawaeleza tutamtangaza lini, lakini Jumamosi natoa press release”, amesema Manara.
“Ishu ya kwamba tumemtoa nchi gani inakuwa siyo ‘story’ tena itakuwa imeshapwaya hiyo. Watu wawe na subra Jumatatu siyo mbali”, ameongeza Manara.
Juma lililopita Manara alisema, wamepanga kumtangaza kocha mpya wiki hii lakini Manara ametoa taarifa nyingine akisema kocha huyo atatambulishwa wiki ijayo. Siku chache zilizopita, mwenyekiti wa usajili wa klabu hiyo Zacharia Hans Poppe alisema, kocha waliyempata kurithi mikoba ya Kopunovic ni raia wa Uingereza.

No comments: