Tuesday 19 December 2017

Diwani wa Sombetini Kupitia Chadema amesema yuko tayari Kujiunga CCM kama waliomuua Mawazo watapatikana

Diwani wa (CHADEMA), Kata ya Sombetini, Ally Bananga amesema yupo tayari kurudi (CCM) ikiwa viongozi wa chama hicho ambao wanataka kumnunua ikiwa watamuonyesha watu waliowatuma kumuua Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Geita, Alphonce Mawazo.


Ally Banaga amedai kuwa yeye yupo tayari kurudi CCM kama viongozi hao watatimiza jambo hilo na kusema hiyo ndiyo itakuwa gharama yake kurudi CCM na siyo fedha au mali kama ambavyo wengine wanadaiwa kupewa.

"Ma CCM wanaotaka kuninunua, leo nataja gharama za kurudi CCM. Nionyesheni mliowatuma kumuuwa Mawazo, nitajiunga nanyi siku hiyo hiyo" alindika Ally Banaga

Wawili wakamatwa na kilo 64 za madawa ya Kulevya

Wakazi wawili wa Dar es Salaam wamekamatwa eneo la Kilambo mkoani Mtwara lililopo mpakani na nchi ya Msumbiji wakiwa na pakiti zenye uzito wa kilo 64 za dawa za kulevya aina ya heroin.

Akizungumza na Mwananchi jana, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Rogers Sianga alisema watuhumiwa walikamatwa Desemba 7 wakiwa na dawa hizo zikitokea mkoani Pemba nchini Msumbiji kuingizwa Tanzania.

Sianga alisema pakiti hizo zilifichwa kwenye gari na kila moja ilifungwa kwa ujazo wa kilo moja.

Alisema watuhumiwa walipokamatwa walipelekwa kwa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya kwa ajili ya ukaguzi wa kina.

Monday 18 December 2017

ROSE MHANDO AJIUNGA RASMI CCM

Mwanamuziki wa nyimbo za Injili, Rose Muhando amejiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM) akiwa kwenye Mkutano Mkuu wa Taifa wa chama hicho unaofanyika Mjini Dodoma.

Nasary Afunguka baada ya TAKUKURU kutupilia mbali Ushahidi wake


Mbunge wa Arumeru Mashariki Mh.Joshua Nassari leo ameandika kupitia Moja ya ukurasa wake wa Mitandao ya kijamii maneno haya baada ya TAKUKURU kutupilia mbali ushahidi alioutoa kwa madiwani walionunuliwa na Kujiunga ccm

Mahakama kuu ya mwachia Huru Sheikh Issa Ponda

Mahakama Kuu imemuachia huru Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu, Sheikh Issa Ponda katika rufaa iliyokatwa na Jamhuri kupinga hukumu ya Mahakama ya Morogoro iliyokuwa imemuachia huru. Alishtakiwa kwa kesi ya kutoa maneno ya uchochezi.

Friday 15 December 2017

WASHTAKIWA WA MAPENZI YA JINSIA MOJA WAACHIWA HURU MWANZA

Washtakiwa wanne katika shauri la kufanya vitendo vinavyoashiria mapenzi ya jinsia moja na makosa la kimtandao wameachiwa kwa dhamana baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Mwanza kutupilia mbali hoja za kuzuia dhamana zao zilizowasilishwa na upande wa Jamhuri.


Uamuzi huo umetolewa na Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi, Wilbert Chuma leo Desemba 15, baada ya kukubaliana na hoja za mawakili wa utetezi, Mashaka Tuguta, Ogastini Kulwa na Jebra Kambole kuwa hoja zilizowasilishwa na upande wa mashtaka ni dhaifu mbele ya macho ya sheria.
Washtakiwa katika shauri hilo namba 548/2017 ni Milembe Suleiman na Janeth Shonza wanaodaiwa kuvishana pete ya uchumba licha ya wote kuwa wanawake.

Thursday 14 December 2017

ASKARI AMPIGA RISASI ASIKARI MWENZIE KWA WIVU WA MAPENZI

Akizungumza na waandishi wa habari mtu wa karibu na askari hao amesema kuwa chanzo cha ugomvi wa askari hao ni wivu wa mapenzi ambapo marehemu pamoja na mtuhumiwa ambaye ametambulika kwa jina la Faustine Masanja wameona nyumba moja.

Amedai marehemu alipofika asubuhi kazini ndipo mtuhumiwa Masanja alimpiga mwenzake risasi ya kichwa na alipokimbizwa katika hospitali ya Mkoa Mount Meru alifariki dunia.

ALIYEKUWA MBUNGE WA SIHA KUPITIA CHADEMA AJIUZULU NA KUJIUNGA CCM






Mbunge wa Jimbo la Siha kwa tiketi ya CHADEMA, Godwin Ole Mollel ajiuzulu nafasi hiyo pamoja na uanachama wa CHADEMA kuanzia leo Disemba 14, 2017.

Wednesday 13 December 2017

RAIS WA KOREA KASKAZINI AMJIA JUU TRUMP KUHUSU JERUSALEMU

Rais wa Korea-Kaskazini Kim Jong Un amesema kuwa uamuzi wa Trump kutangaza kuutambua mji wa Jerusalem kama mji mkuu wa Israel hauna maana yeyote.
Mpango wa Marekani kuamisha ubalozi wake Tel Aviv na kuhamia Jerusalem ni jambo la kukemewa.
Kim Jong Un anapinga uamuzi wa Trump kuhusu jiji la Jerusalem.
Rais wa Korea-Kaskazini amesema kwa kejeli kuwa iwapo kuna taifa linaitwa Israel basi mji wake mkuu uwe Jerusalem.

FAMILIA YA BEN SAANANE YA ANDIKA HAYA KUKUMBUKA SIKU YA KUZALIWA KWA BEN SAANANE

Ni mwaka mmoja na siku kadhaa tangia Ben Saanane atoweke/atoweshwe katika mazingira tatanishi.
Leo Ben, anamitiza miaka kadhaa tangia kuzaliwa kwake. Happy beloved birthday bro, hero and comrade!

Naelewa namna Baba, Mama, dada, kaka na ndugu zako wanavyo jisikia, ulikuwa kaka mkubwa, lango la familia, tegemeo, ulikuwa sehemu ya furaha ya familia, Leo walio kulea wanaumia, walitamani siku ya leo mshereheke siku hii pamoja, ila imekuwa tofauti, siku imekuwa ya mawazo na mateso kuliko tegemeo.
Masonokeno na Maumivu yao tumeyaishi, machozi katika mioyo yao hayakuwahi kauka, furaha yao imekuwa ya msimu, kila wakijaribu kupata furaha, kukosenaka kwako kunaondosha

Tuesday 12 December 2017

Babu wa Loliondo aoteshwa tena, Atabiri ummati Kurudi kupata huduma ya Kikombe

Mchungaji Ambilikile Mwasapile maarufu Babu wa Loliondo akitoa huduma ya kikombe kwa wagonjwa
NGORONGORO . Mchungaji Ambilikile Mwasapile maarufu Babu wa Loliondo aliyehudumia maelfu ya watu ndani na nje ya nchi kwa dawa aliyoitoa kwa kipimo cha kikombe amedai ameoteshwa kuwa umati utarudi kijijini Samunge kupata dawa.
Amesema ana uhakika wa jambo hilo kwa kuwa hata mwaka 2011 kabla ya maelfu ya watu kufika nyumbani kwake alioteshwa, hivyo amejiandaa kuweka miundombinu bora zaidi na hasa ujenzi wa vibanda atakavyovitumia kutoa huduma.
Mchungaji Mwasapile alisema hayo jana Jumapili Desemba 10,2017 mbele ya ujumbe wa Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi, Joseph Kakunda aliyekuwa mkoani Arusha kukagua miradi ya maendeleo, ikiwemo ya kuwawezesha wananchi kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.
Miongoni mwa waliofika kupata ‘kikombe’ kwa gharama ya Sh500 mwaka 2011 walikuwemo wafanyabiashara maarufu, wanasiasa na viongozi waandamizi serikalini.
Akizungumzia dawa yake anayodai inatibu maradhi mengi amesema kwa sasa anaitoa kwa watu wachache wanaofika kijijini hapo.

Monday 11 December 2017

HATUA YA 16 BORA UEFA , CHELSEA USO KWA USO NA BARCELONA HUKU REAL MADRID NA PSG

Kikosi cha Klabu ya chelsea 
Chelsea wamepangwa kukutana na Barcelona hatua ya 16 bora katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya, Tottenham nao wakapewa mabingwa wa Italia Juventus baada ya droo kufanywa.
Viongozi wa Ligi ya Premia Manchester City watakutana na FC Basel ya Uswizi, Manchester United wakutana na Sevilla wanaocheza La Liga nao Liverpool wakutane na FC Porto ya Ureno.

MIILI YA WANAJESHI WA TANZANIA WALIOUAWA kONGO KUWASILI LEO NCHINI

Wanajeshi wa Kulinda amani Nchini Kongo wakitoa heshima za Mwisho kwa wanajeshi waliopoteza maisha katika shambbulio lililofanywa na waasi nchini humo

Dar es Salaam. Miili ya askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) waliouawa na waasi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) inarejeshwa nchini leo.

Taarifa ya ofisi ya habari ya JWTZ imesema miili ya askari hao itawasili nchini leo Jumatatu Desemba 11,2017 saa kumi na mbili jioni katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA).

Mwenyekiti na Katibu wa ACT wazalendo Singida ajiunga CCM


SINGIDA: Mwenyekiti wa ACT wazalendo, Wilfred Kitundu na Katibu wake Loth Thomas wamejivua uanachama wa chama hicho na kujiunga na CCM.Wadai kuridhishwa na utendaji wa Rais Magufuli