Wednesday 13 December 2017

RAIS WA KOREA KASKAZINI AMJIA JUU TRUMP KUHUSU JERUSALEMU

Rais wa Korea-Kaskazini Kim Jong Un amesema kuwa uamuzi wa Trump kutangaza kuutambua mji wa Jerusalem kama mji mkuu wa Israel hauna maana yeyote.
Mpango wa Marekani kuamisha ubalozi wake Tel Aviv na kuhamia Jerusalem ni jambo la kukemewa.
Kim Jong Un anapinga uamuzi wa Trump kuhusu jiji la Jerusalem.
Rais wa Korea-Kaskazini amesema kwa kejeli kuwa iwapo kuna taifa linaitwa Israel basi mji wake mkuu uwe Jerusalem.

Kwa mujibu wa kituo cha habari cha Ufaransa cha AFP ni kwamba msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Korea-Kaskazini amesema kuwa Marekani inatishia amani na utulivu ulimwenguni .

Ujumbe wake ulimalizia kwa kusema kuwa Korea-Kaskazini ipo bega kwa bega na wapalestina na waarabu wanaopigania haki yao

No comments: