Friday 31 October 2014

Rais wa Burkinafaso ang'olewa madarakani


Kuna hofu kuwa rais Compaore anataka kuendelea kushikilia madaraka
Msemaji wa jeshi amewaambia waandishi wa habari mjini Ouagadougou kuwa bwana Compaore hayuko mamlakani tena.
Rais Compaore alikuwa ametangaza kuwa atajiuzulu baada ya kipindi cha serikali ya mpwito ya mwaka mmoja .
Lakini wanasiasa wa upinzani wakakataa kata kat kuendelea kwa utawala wake na wakamtaka ajiuzulu maramoja.
Rais Compaore alikuwa ameongoza kwa zaidi ya miaka 27 tayari.
Kumeripotiwa maandamano mapya nchini Burkina Faso ya kutaka kujiuzulu mara moja kwa rais wa nchi hiyo Blaise Compaore.
Viongozi wa upinzani wanakutana kwenye mkji mkuu Ouagadougou kukubaliana kwa pamoja hatua watakazochukua.
Siku ya Alhamisi waandanamaji walikarisishwa na jitihada za rais za kuongeza kipindi chake chake miaka 27 madarakani na wakateketeza bunge na kusaka kituo cha runinga cha serikali.
Rais Compaore ametangaza kuvunjwa kwa serikali na bunge
Bwana Compaore alitupilia mbali jitihada za kubadilisha katiba ambayo ingemruhusu kuwania tena muhula mwingine kama rais lakini akasema kuwa atabaki madarakani kwa mwaka moja zaidi .
Viongozi wa Upinzani Nchini Burkina Faso wamewaomba waandamanaji kutolegeza kamba bali kuendelea na maandamano huku wakimtaka Rais Blaise Campaore ang'atuke mamlakani mara moja.
Licha ya Rais Compaore wa Burkina Faso kuhutubia taifa siku moja baada ya vurugu kubwa na kutangaza kuvunja serikali waandamanaji hawataki kusikia kwamba apewe muda wa mwaka mmoja ndipo aondoke madarakani.
Jana jioni kiongozi wa Jeshi  General Honore Traore alitangaza kuundwa kwa serikali ya mpito itakayodumu kwa kipindi cha mwaka mmoja japo hakusema ninani atakayeiongoza.

Mmiliki wa kampuni ya Apple ajitatangaza kuwa ni Shoga

Mkuu wa kampuni ya Apple
Mkuu wa kampuni ya Apple Tim Cook ametangaza jinsia yake akisema kuwa ''anajivunia kuwa shoga''..
Bwana Cook alitoa tamko hilo ili kujaribu kuwasaidia watu wanaong'ang'ana kutangaza jinsia zao katika ripoti iliochapishwa katika gazeti la biashara la kila wiki la Bloomberg.
Amekuwa wazi kuhusu jinsia yake,lakini pia amejaribu kuweka maisha yake katika faragha hadi sasa alisema.
Nembo ya kampuni ya Apple
Wiki hii Bwana Cook alitoa changamoto kwa jimbo lake la Alabama kuhakikisha kuwa haki za mashoga na wale wanaobadili jinsia zinaheshimiwa.
''Mimi sijitambui kama mwanaharakati,lakini nimegundua nilivyofaidika na mikakati iliowekwa na wengine'',alisema bwana Cook.
''Kwa hivyo iwapo watu wakisikia kwamba mimi ni shoga kutawasaidia baadhi yao ,ama kumpa faraja yule anayejisikia mpweke ama kuwashinikiza wengine kupigania haki zao,basi afadhali kutangaza maisha yangu ya faragha''aliongezea.
Bwana Cook amesema amekuwa wazi kuhusu jinsia yake na watu wengi wakiwemo wafanyikazi wenzake katika kampuni ya Apple,lakini hilo halikuwa chaguo rahisi kutangaza hadharani kuhusu jinsia yake.

TFF yataka jezi mpya Taifa stars

Shirikisho la soka Tanzania, TFF, limesema linakaribisha wabunifu watakaobuni mwonekano wa jezi mpya za timu ya taifa kwa mechi za nyumbani na ugenini.
Hata hivyo sharti la ubunifu huo lazima uzingatie rangi za bendera ya taifa ambazo ni kijani, njano, nyeusi na bluu.
Wakati tangazo hili likitolewa na TFF, tayari uongozi mpya chini ya rais wake Jamal Malinzi umebadili jezi zinazotumiwa katika mechi za timu ya taifa, Taifa Stars, kutoka zile zilizozoeleka na mashabiki na Watanzania wote hadi jezi mpya zinazolalamikiwa na mashabiki wengi kuwa hazina mvuto na hazionyeshi rangi halisi ya bendera ya taifa la Tanzania.

Jezi mpya ya timu ya taifa ya Tanzania, ambayo nayo inatakiwa kubadilishwa
TFF ilipoamua kutumia jezi mpya zinazotumika sasa haikuwashirikisha wabunifu wa mavazi kuhusu jezi mpya ya timu ya taifa na badala yake ikaja na jezi ambayo imekuwa ikilalamikiwa na mashabiki kuwa haina mvuto na haiwakilishi rangi halisi za bendera ya taifa, huenda ndio maana safari hii wametoa tangazo hilo.
Mbunifu atakayeshinda atapata zawadi ya shilingi milioni moja za Kitanzania sawa na karibu dola mia saba za Kimarekani kwa atakayebuni jezi ya kuchezea mechi za nyumbani na vile vile mshindi atakayebuni jezi za kuchezea mechi za ugenini naye atapata kiasi kama hicho cha fedha.
Jezi ya sasa ina rangi ya samawati na bluu nyeusi

Thursday 30 October 2014

Ajali iliyotokea Tengeru yapeleka kilio katika sekta ya Elimu mwanachuo na maafisa elimu wanne waaga dunia

Watu 13 akiwamo mke wa Jaji, Profesa John Luhangisa, Retisia Luhangisa ambaye ni Ofisa Elimu wa Taaluma wa Halmashauri ya Meru mkoani hapa, wamefariki duniani baada ya gari la abiria aina ya Hiace walilokuwa wamepanda kugongana uso kwa uso na lori la mafuta.
Katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru maelfu walifurika kwa ajili ya kutambua jamaa zao ambapo mke na mume ambao ni Elly Kaaya, Ofisa Elimu na Kumbukumbu wa Halmashauri ya Meru na mumewe Kundaeli Kaaya ambaye ni mwalimu wa Shule ya Msingi Ndoombo wilayani Arumeru walikuwa ni miongoni mwa maiti zilizotambulika katika ajali hiyo.
Tukio hiilo limetokea jana eneo la Madila kwenye Kijiji cha Sing’isi saa 10 jioni baada ya gari hilo la abiria lililokuwa linatokea Usa River kwenda Arusha kugongana na lori hilo lililokuwa linatoka Arusha kwenda Kilimanjaro.
Wengine waliotambuliwa katika ajali hiyo ni pamoja na Ofisa Elimu wa Taaluma Halmashauri ya Meru, Zakia Katunga na kondakta wa gari hilo, Simon Wilenya na abiria Kundaeli Kadoya pamoja na mwanafunzi wa chuo kikuu cha maendeleo ya jamii Tengeru (CDTI-TENGERU) aliyefahamika kwa jina la Loretha Baruti wa mwaka wa Kwanza ambae alikuwa na mwanafunzi mwenzake ambaye yuko kwenye vyumba vya wagonjwa mahutihuti katika hospitali ya Mount Meru jina lake halijafahamika kwa haraka lakini ni Mwanafunzi wa CDTI-TENGERU, pi
Hadi jana jioni, miili mingine sita ilikuwa bado haijatambulika, huku mamia ya watu wakiendelea kufika katika uwanja wa chumba cha kuhifadhi maiti kutambua miili hiyo.
Hata hivyo, hadi jana dereva wa gari la abiria alikuwa hajulikana alipo na majeruhi wengine watatu walikuwa wamelazwa wakiwa mahututi Hospitali ya Wilaya ya Meru.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alithibitisha jana kutokea kwa tukio hilo na kuahidi kesho (leo) angetoa taarifa ya tukio hilo.
Jaji Luhangisa aliteuliwa hivi karibuni, kuwa Jaji na Rais Jakaya Kikwete.
Kabla ya uteuzi huo, alikuwa msajili wa Mahakama ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki

Msiba tena Bongo Muvi; Mzee Manento afariki

Habari zilizotufukia hivi punde zinasema kuwa muigizaji Mzee Manento amefariki dunia hapo jana. Bado tunafuatilia kwa karibu habari hizi nz chanzo ch kifo cha mzee wetu huyu.
Mzee Mnento atakumbukwa hasa kwa filamu alizocheza kiumakin na marehemu Kanumba. Hero of the church, Dar to lagos,fake pastor n.k pumzika kwa Amani
Mungu ailaze Roho ya maerehemu mahali pema peponi amina

Mke amwandalia Mumewe Mlo wa kondomu kumkomesha

kondomu
Mwanamke mmoja mwenye watoto watatu katika wilaya ya Kole nchini Uganda alimuandalia mumewe mlo wa mipira ya kondomu kufuatia ugomvi usiokwisha kati yao.
Mwanamke huyo ambaye ni mkaazi wa eneo la Arao aliripotiwa kununua paketi tatu za kondomu aina ya "Trust" kutoka duka jirani kabla ya kuzipika na kumuandalia mumewe kama chakula baada ya kurudi nyumbani akiwa amelewa chakari.
Kwa mujibu wa gazeti la Daily Monitor la nchini Uganda, mwanamke huyo aliikata kata mipira hiyo ya kondomu ambayo ilikuwa haijatumika katika vipande vidogo vidogo na kuvichemsha kwa muda kabla ya kuvikaanga kwa mafuta ya kupikia na viungo vingine.
Wakati mumewe alipowasili kutoka kubugia pombe katika eneo jirani la kibiashara la Odede,aliandaliwa mlo huo katika sahani tofauti moja ikiwa na mipira hiyo kama mboga na nyingine ikiwa na mkaa.
Lakini jamaa huyo alibaini njama za mkewe baada ya kuonja mlo huo na kugundua ulikuwa na ladha tofauti.
Hatua hiyo ilikuwa ikilenga kumfunza mume huyo ambaye amedaiwa kuzua ugomvi na mkewe kila anapolewa na kurudi nyumbani.

Utafiti unaonyesha kufanya Mapenzi ni tiba ya saratani

Kulala na wanawake wengi kunapunguza hatari ya kupatikana na ugonjwa wa saratani ya kibofu cha mkojo,kulingana na utafiti.
Katika utafiti uliochapishwa katika jarida la saratani,Watafiti kutoka chuo kikuu cha Montreal wamebaini kwamba ikilinganishwa na wanaume walio na mpenzi mmoja katika maisha yao yote,kulala na zaidi ya wanawake 20 kunapunguza uwezekano wa kupatikana na ugonjwa huo kwa asilimia 28.
Wanaume 3,208 walishiriki katika utafiti huo ambapo kati yao Wanaume 1,590 walipatikana na ugonjwa huo kati ya Septemba mwaka 2005 na Agosti mwaka 2009.
Kwa jumla watafiti hao walibaini kwamba wanaume wenye saratani ya kibofu cha mkojo kuna uwezekano mara mbili kwa wao kuwa na watu wa familia zao wenye saratani.
Hatahivyo ushahidi unaonyesha kwamba idadi kubwa ya wapenzi wa kike miongoni mwa wanaume inapunguza tishio la ugonjwa huo.
Mwanamume anapojamiana na zaidi ya wanawake 20 katika maisha yake,tisho la kupata ugonjwa huo linapoungua kwa asilimia 28 mbali na asilimia 19 kwa aina yoyote ya ugonjwa wa saratani.
Utafiti huo pia umebaini kwamba mmoja kati ya wanaume wanne wa kiafrika hupatikana na saratani

Wananchi walalamikia kupandishwa kwa gharama mUHIMBILI

Baadhi ya wananchi wamelalamikia mabadiliko ya gharama za utoaji huduma katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kwa madai kuwa wanaumia kutokana na kuwa na vipato vidogo.
Mabadiliko hayo yaliyotangazwa hivi karibuni kwa wagonjwa wa rufaa ni malipo ya kitanda ya Sh5,000 na Sh2,000 ya chakula kwa siku.
Akizungumza jijini hapa jana, Yasinta Mlole alisema alitozwa gharama hizo alipompeleka mgonjwa wake kutoka Morogoro.
Alisema ilimlazimu kulipia gharama hizo kwa sababu mgonjwa wake alipewa rufaa ya kutibiwa katika hospitali hiyo.
“Mgonjwa wangu ana hali mbaya. Kwa kweli hali inakuwa ngumu na sijui atakaa hapa mpaka lini,” alisema.
Naye James Mbela alisisitiza umuhimu wa kuipa kipaumbele sekta ya afya ili kuhakikisha dawa zinapatikana wakati wote na watendaji wake wanatimiza wajibu.
Awali, msemaji wa MNH, Aminiel Algaesh alisema tangu mwaka 2003 wagonjwa walikuwa wakilipa Sh20,000 kwa muda wote walipokuwa hospitali.

Ufaransa yatoa somo uwekezaji gesi

ufaransaBALOZI wa Ufaransa nchini, Malika Berek, amesema watanzania wana fursa kubwa kuwekeza katika sekta ya mafuta na gesi kwa kushirikiana na wawekezaji wa nje  kwani mtaji wao ni rasilimali zao.
Alisema mtaji pekee wa watanzania katika uwekezaji huo ni rasilimali yao na wawekezaji wa nje watakuja na mitaji na teknolojia yao.
Balozi huyo, alitoa kauli hiyo jana wakati alipomtembelea Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi katika Ofisi ya Makao Makuu ya IPP jijini Dar es Salaam.
Balozi huyo mpya nchini, alipingana na dhana kwamba watanzania hawawezi kuwekeza kwenye sekta hiyo kwani hawana mitaji na badala yake alisisitiza mtaji wa rasilimali iliyopo nchini, inatosha kuwa mtaji wao kuwekeza kwa ubia na wawekezaji wa nje.
“Sikubaliani na dhana kwamba watanzania hawana mitaji ya kuwekeza kwenye gesi, hapana. Nakubaliana nawe kwamba rasilimali iliyopo inatosha kuwa mtaji wa kuwekeza kwa ubia na wawekezaji wa nje,” alisema Balozi Berek.
Alisema lengo la Serikali yake ni kuimarisha zaidi mahusiano yake na Tanzania na iko tayari kutoa mafunzo kwa vijana wa kitanzania na kutolea mfano wa baadhi ya waandishi wa habari nchini waliokwenda nchini Ufaransa kwenye ziara ya mafunzo kwa vitendo na kubadilishana mawazo na wenzao wa Ufaransa.
Pia alisema Serikali yake imeandaa mkutano maalum wa Biashara kati ya wafanyabiashara wa Tanzania na Ufaransa, utakofanyika Paris Desemba 15 na kwamba mkutano huo utafungua milango ya uwekezaji nchini.
Balozi huyo alitoa kauli hiyo wakati akijibu swali la Dk. Mengi aliyetaka kujua maoni yake kuhusu dhana kwamba watanzania ni masikini na hawawezi kuwekeza kwenye sekta ya gesi na mafuta.
Dk. Mengi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF), alisema kumekuwa na maoni na dhana potofu kwamba watanzania ni masikini sana, hivyo hawana uwezo wa kuwekeza kwenye sekta hiyo wakati wanamiliki rasilimali kubwa ya ardhi, mafuta, madini na nyinginezo.

Mdee awashauri Viongozi wa Dini waweimara

MWENYEKITI wa Taifa Baraza la Wanawake CHADEMA, (BAWACHA), Halima Mdee, amesema kuwa siasa za matamko ndizo zinazowapa jeuri watawala hivyo amewashauri viongozi wa dini wasimame kidete kupigania maslahi ya umma kwa vitendo.
Aidha, amesema kuwa Jeshi la polisi lilifikia hatua ya kuwapiga mabomu kutokana na Jeshi hilo kujitoa kwenye majukumu yake ya msingi na kuamua kufanya siasa kwa lengo la kukisaidia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambako lilishitushwa na mapokezi makubwa wanayoyapata kwa wananchi wa kanda ya Ziwa na ujumbe mzito wanaoufikisha, jambo ambalo hawakulitarajia.
Mdee, aliyasema hayo jana wilayani Karagwe, wakati alipokuwa akifanya mahojiano maalum na kituo cha redio jamii cha Fadeco, mara baada ya kumaliza ziara wilayani humo akiwa ameambatana na Makamu wake, Hawa Mwaifunga, Katibu Grace Tendega na Naibu Katibu, Kunti Yusuh.
Alisema kuwa viongozi wa dini wamekuwa wakitoa matamko mara kwa mara wakielezea misimamo yao juu ya mambo mbalimbali yanayoedelea nchini ikiwemo umuhimu wa kuheshimiwa kwa maoni ya wananchi kwenye mchakato wa Katiba, lakini watawala wamekuwa hawawasikilizi hivyo ni vema wakabadili njia ya kufikisha ujumbe.
Mbunge huyo wa Kawe, alisema kuwa suala la katiba ni la kila wananchi hivyo wabadilike waache kulalamika na badala yake wachukue hatua kwa kuhakikisha maoni yao  waliyotoa kwenye Tume ya Mabadiliko ya Katiba yanaheshimiwa ikibidi kwa kufanya maandamano ya amani.
Alisema kuwa jukumu la kupigania katiba bora inayozingatia maoni ya wananchi lisiachiwe Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA ), kwani katiba ni kitu muhimu sana, ndiyo injini ya nchi na itasaidia kurekebisha mfumo wa nchi kwani kuna maeneo mengi yana utajiri mkubwa wa rasilimali lakini wananchi wake ni fukara wa kuindukia.

Mahakama ya ICC yamzuia Gbagbo kumzika mama yake

Rais wa zamani wa Ivory Coast Gbagbo
Majaji katika mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai na uhalifu wa kivita huko The Hague wametupilia mbali ombi la raisi wa zamani wa Ivory Coast kwenda kuhudhuria katika maziko ya mamake mzazi.
Mahakama hiyo ilikua inaangalia zaidi suala la usalama wa huko aendako,na hivyo kumzuia kwenda kwao Laurent Gbagbo kwa muda wa siku tatu.
Gbabo anakabiliwa na makosa ya uhalifu wa kibinaadamu kufuatia uchaguzi ulofanyika mwaka 2010,ambapo inakadiriwa watu elfu tatu waliuawa.

Nyalandu adai Obama anamshawishi agombee Urais 2015

Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, amerejea kauli yake ya kwamba Serikali ya Marekani inamtaka awe mrithi wa Rais Jakaya Kikwete mwakani.
Tangu mwaka 2012, Nyalandu amekuwa akisisitiza kuwa Rais Barack Obama pamoja na uongozi mzima wa Marekani, wanataka ashike nafasi hiyo kubwa kwa kile anachosema wanaridhishwa na kipaji chake cha uongozi.
Awali, waziri huyo anayetajwa kuwa wakala wa taifa hilo lenye ushawishi mkubwa duniani, alitoa kauli hiyo kwenye hafla iliyoshirikisha watu walio karibu naye.
“Wakati huo tulidhani anatania, lakini sasa amekuwa akipita huku na kule nchini akisisitiza kuwa Rais Obama amenuia kuhakikisha yeye (Nyalandu) anakuwa Rais wa Tanzania mwaka 2015,” amesema mmoja wa watu walio karibu naye.
Akiwa mkoani Mbeya hivi karibuni, Nyalandu amenukuliwa akijipigia debe la urais kwa kusema: “Watanzania wahakikishe wanapata rais aliyeandaliwa na Mungu ili kuweza kuwavusha kutoka walipo kuelekea kwenye nchi ya neema kutokana na utajiri mkubwa wa rasilimali tulizo nazo.”
Mgombea huyo kwa sasa anakabiliwa na shinikizo linalotokana na utendaji kazi wake mbovu, amebuni mpango wa kuwapoza wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira kwa kuwaandalia safari nje ya nchi.
Hata hivyo, taarifa zinasema wajumbe kadhaa wa Kamati hiyo waliokutana wiki iliyopita jijini Dar es Salaam walipinga kwa nguvu zote mpango huo, wakisema hiyo ilikuwa ‘rushwa’ ili wasiweze kuhoji utendaji kazi mbovu wa Nyalandu.
Miongoni mwa wajumbe ambao chanzo chetu kinasema walikuwa mstari wa mbele kupinga mpango huo ni Mbunge wa Viti Maalum, Esther Bulaya (CCM).
"Esther alitoa hoja nzuri sana. Alihoji iweje waziri kabla ya kuwasilisha ripoti yake kwa wajumbe aanze kuwapa ‘habari njema’ ya kuwapa safari za nje ya nchi. Wajumbe wengi waliunga mkono hoja hiyo na mwisho wa siku ikawa safari hizo zimekataliwa na wajumbe,” mmoja wa wabunge ameiambia waandishi wa habari.
Kwa upande wake, Bulaya ameulizwa na waandishi wa habari na kusema: “Siwezi kusema mengi, lakini ni kweli mjadala ulikuwa mkali.”
Ripoti ya Wizaya hiyo ambayo Nyalandu alikuwa aiwasilishe kwenye kikao hicho, ilikwama kuwasilishwa baada ya wabunge hao kuipinga wakisema ni nyepesi mno.
“Ilikuwa ripoti ya ajabu sana, ilikuwa shallow (haikuwa ya kina) sana, haikuwa na mambo mazito ambayo tulitarajia kuyaona,” alisema mjumbe mwingine.
Habari za uhakika zilisema Nyalandu alikuwa amerejea Dar es Salaam kutoka nje ya nchi saa kadhaa kabla ya kwenda kuwasilisha ripoti hiyo kwa wabunge, hatua ambayo ilionekana wazi kwamba hata yeye alikuwa hajui kilichomo.
Kama ilivyotarajiwa, Mwanyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, James Lembeli, alijaribu kumtetea Nyalandu akiwasihi wajumbe watulie wajue kilichomo. Madai yake yakawa kwamba hata kama kuna kasoro, hilo lilikuwa kosa la wasaidizi wa Waziri kwa hiyo wa kulaumiwa ni wao.
Kauli hiyo ilipingwa na wajumbe ambao walisema ilimradi ripoti hiyo inayo saini ya Nyalandu, basi yeye ndiye anayewajibika kwa upungufu wote.
Mjumbe mwingine (jina tunalo) akasema wajumbe wanataka maelezo kuhusu kashfa ya uuaji wanyamapori 704 kwa kutumia Leseni ya Rais ambayo Nyalandu alimwamuru Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori awape rafiki zake Wamarekani.
Walitaka maelezo kuhusu kashfa ya kujigawia vitalu vya miti inayomkabili Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mahmoud Mgimwa, na walitaka kujua matumizi ya fedha zinazodaiwa kutumiwa na Nyalandu kuwahudumia wasanii anaokwenda nao ughaibuni. Matumizi ya fedha kwa ajili ya malipo ya hoteli za kitalii Dar es Salaam na Arusha; mgongano wa kiutumishi kati yake na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Maimuna Tarishi, na mengine mengi.
“Ile ripoti haikuwa na kitu, ilikataliwa na akatakiwa aondoke. Ilipofika kwenye saa nne tukaahirisha kikao.  Akaondoka na wataalamu wake. Aliagizwa ajipange upya awasilishe ripoti inayolingana na uzito wa Wizara na tuhuma zinazowakabili,” kimesema chanzo chetu.
Chanzo kingine cha habari kinasema Nyalandu alisema anaandamwa kwa fitina na magazeti mawili (hakuyataja) kwa sababu ya utendaji wake wa kazi, hasa kwa kuwa amewadhibiti majangili na mafisadi. Hata hivyo, utetezi huo ulipingwa na mmoja wa wajumbe aliyehoji: “Unasema unaandamwa na magazeti kwa mambo yasiyo ya kweli! mbona magazeti yanaandika na kutoa vielelezo? Kwanini wewe usitoke ukazungumza na waandishi wa habari na wewe ukatoa vielelezo vyako vya kukanusha kama kweli ni ya uongo?
Pamoja na kubanwa kwa swali hilo, Nyalandu akaendelea kusisitiza kuwa anaandamwa kwa sababu amegusa maslahi ya mafisadi ambao amewafutia kile alichokiita 'ulaji wa rasilimali za nchi'.
Hata hivyo, Nyalandu ndiye anayehusishwa mno na matumizi mabaya ya madaraka pamoja na utoro kazini. Mara nyingi amekuwa akisafiri nje ya nchi, na hata anapokuwa nchini, amekuwa akitumia muda mrefu Dar es Salaam na Arusha. Wiki mbili zilizopita, katika kuonesha ‘wizara ina waziri’ alitumia ndege kuzuru maeneo kadhaa yakiwamo ya Mbeya, Njombe, Singida, Tabora, Arusha, na Kilimanjaro. Pia alikwenda Serengeti kinyemela kupata taarifa za kuuawa kwa ndovu kadhaa.
Amejitahidi kuzima habari zinazohusu matukio ya kuuawa kwa ndovu kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kutaka kuuhadaa umma kwamba amefanikiwa kwenye mapambano dhidi ya ujangili.
“Hakuna habari ya kuuawa ndovu ambazo utaziona; mtasikia habari za kukamatwa pembe tu. Magazeti hayaandiki. Mitandao ya kijamii (ukiwamo mtandao maarufu nchini) haiandiki tena habari za kashfa za Nyalandu, na hata zile zilizokuwamo zimefutwa au kufungwa kabisa. Amehakikisha kila mahali anadhibiti,” kimesema chanzo chetu.
mwandishi wetu   aliripoti kwa kina juu ya Nyalandu kuwa na safari na wasanii wawili, Aunty Ezekiel na Kassim Mganga.
Licha ya Aunty Ezekiel kukanusha juu ya ziara hiyo ya kikazi ya Nyalandu, lakini Mganga kwa upande wake ameibuka na kuthibitisha kwamba safari hiyo iliratibiwa na Nyalandu.
Mganga aliyekwepa kuzungumza  Ijumaa iliyopita, siku moja kabla taarifa zake zilisomeka kwenye gazeti la HabariLeo, toleo Na. 02864 la Alhamisi ya Oktoba 23, mwaka huu.
Katika kurasa za katikati za gazeti hilo linalomilikiwa na Serikali, Mganga amesema walipelekwa Marekani na Nyalandu.
Msanii huyo aliyerejea hivi karibuni kutoka huko Ughaibuni katika tamasha aliloliita ni la kutangaza utalii wa Tanzania nchini humo, anasema ametengeneza mtandao kwa ajili ya kazi za nje.
Mganga anasema huko alifanya kazi kama ya kutoa burudani, akiwa na Msanii wa maigizo Aunt Ezekiel na Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu ambaye ndiye aliyewapeleka.

Guy Scott mzambia mwenye asili ya kizungu ndiye Kaimu rais wa Zambia

Kaimu rais wa Zambia Guy Scott
Serikali ya Zambia imemchagua makamu wa rais Guy Scott, mzambia mwenye asili ya kizungu kuwa kaimu rais wa nchi hiyo ya Kusini mwa Afrika hadi pale uchaguzi utakapofanyika ndani ya siku 90.
Kaimu rais wa Zambia Guy Scott
Scott amekuwa kaimu rais hii leo baada ya kifo cha rais Michael Sata kilichotokea mjini London Jumanne Jioni. Guy Scott sasa ni kiongozi wa kwanza mzungu katika taifa la kiafrika tangu F.W. de Klerk, rais wa mwisho katika enzi ya ubaguzi wa rangi Afrika Kusini iliomalizika mwaka wa 1994.
Rais Michael Sata aliye na miaka 77 aliondoka Zambia kuelekea jijini London zaidi ya wiki moja iliopita kwa matibabu ya ugonjwa ambao bado mpaka sasa haujawekwa wazi. Sata aliandamana na mke wake pamoja na watu wengine wa karibu wa familia yake. Kwa mujibu wa katibu Msiska, Rais Sata alifariki Jumanne jioni.

Lakini vyombo vya habari awali vilikuwa vimeripoti Sata aliruhusiwa kutoka hospitali ili apate matibabu chumbani mwake huko nchini Uingereza. Rais huyo wa Zambia ameiongoza nchi hiyo ya kusini mwa Afrika, ya pili kwa ukubwa wa uzalishaji shaba tangu mwaka wa 2011.
Rais wa Zambia Michael Sata
Rais wa Zambia Michael Sata
Katibu wa bunge la Zambia Rowland Msiska ametoa wito wa kuwepo utulivu nchini humo huku akisema taarifa ya mipango ya mazishi itatolewa hivi karibuni. Wasiwasi wa hali ya afya ya Sata ulianza pale rais huyo aliposhindwa kuonekana hadharani kuanzia mwezi wa Juni mwaka huu.
Wiki iliopita Waziri wa Ulinzi Edgar Lungu aliongoza sherehe za kuadhimisha miaka 50 tangu nchi hiyo ilipojipatia Uhuru wake kutoka kwa Uingereza.
Hali ya afya ya rais Sata iliokuwa inazidi kudhoofika ilisababisha mgogoro wa nani atakayemrithi rais huyo ndani ya chama tawala cha Patriotic Front ambapo mwezi Agosti rais Sata alimfuta kazi waziri wa sheria Wynter Kabimba, aliyeonekana kama mtu anayefaa kabisa kukirithi kiti hicho.
Kaimu rais wa Zambia Guy Scott na Mkewe Charlotte Scott
Guy Scott hawezi kuwa rais wa Zambia
Kaimu rais wa Zambia Guy Scott na Mkewe Charlotte Scott Kwa upande mwengine Kaimu rais wa Zambia Guy Scott hawezi kuwa rais kwa sababu wazazi wake wanatokea Scottland. Kulingana na katiba ya Zambia, rais wa nchi hiyo ni lazima awe mzambia kamili kwa maana ya kwamba wazazi wake wote wawili wanapaswa kuwa wamezaliwa nchini humo.
Rais Michael Sata alizaliwa katika eneo moja la Kaskazini lijulikanalo kama Mpika mwaka 1937. Alianza kazi yake ya kwanza kama afisa wa polisi, baadaye akaajiriwa kama mfanyakazi wa reli na kisha mwanachama wa chama cha wafanyakazi.
Baada ya Uhuru wa mwaka 1964, Sata alijiunga na chama tawala cha muungano wa kitaifa wa Uhuru yani United National Independence Party na kuwa gavana wa mji mkuu Lusaka katika miaka ya 80. Alijulikana sana wakati huo kama mchapa kazi na alikuwa akichangia pia kwa kusafisha bara bara yeye mwenyewe.

Rais wa Zambia Michael Sata
Rais wa Zambia Michael Sata
Baadaye akajitenga na rais wa kwanza baada ya kupatikana Uhuru Kenneth Kaunda, na kujiunga na vuguvugu la demokrasia ya vyama vingi, Movement for Multi-Party democracy, (MMD) ambayo kampeni ya vuguvugu hilo ilichangia kufanyika kwa uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi mwaka wa 1991.
Chini ya serikali ya MMD, Sata alihudumu kama waziri wa serikali mitaa, kazi, afya, na pia kama waziri asiyekuwa na wizara maalum. Mwaka wa 2001 aliunda chama chake cha Patriotic Front, kilichoshinda uchaguzi wa mwaka 2011 kwa takriban asilimia 42 ya kura.
Sata alijulikana kwa jina la Utani kama King Cobra kutokana na maneno yake makali, kuwakemea mawaziri wake hadharani na kuwahi pia kumuita rais wa zamani wa Marekani George W Bush kuwa kijana mdogo aliye mkoloni wakati alipochelewa kuwasili katika mkutano wao.
Sata pia alishutumiwa na wakosoaji wake kwa kuongoza kimabavu na kuukandamiza upinzani na hata vyombo vya habari.