Thursday 30 October 2014

Wananchi walalamikia kupandishwa kwa gharama mUHIMBILI

Baadhi ya wananchi wamelalamikia mabadiliko ya gharama za utoaji huduma katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kwa madai kuwa wanaumia kutokana na kuwa na vipato vidogo.
Mabadiliko hayo yaliyotangazwa hivi karibuni kwa wagonjwa wa rufaa ni malipo ya kitanda ya Sh5,000 na Sh2,000 ya chakula kwa siku.
Akizungumza jijini hapa jana, Yasinta Mlole alisema alitozwa gharama hizo alipompeleka mgonjwa wake kutoka Morogoro.
Alisema ilimlazimu kulipia gharama hizo kwa sababu mgonjwa wake alipewa rufaa ya kutibiwa katika hospitali hiyo.
“Mgonjwa wangu ana hali mbaya. Kwa kweli hali inakuwa ngumu na sijui atakaa hapa mpaka lini,” alisema.
Naye James Mbela alisisitiza umuhimu wa kuipa kipaumbele sekta ya afya ili kuhakikisha dawa zinapatikana wakati wote na watendaji wake wanatimiza wajibu.
Awali, msemaji wa MNH, Aminiel Algaesh alisema tangu mwaka 2003 wagonjwa walikuwa wakilipa Sh20,000 kwa muda wote walipokuwa hospitali.

No comments: