Wakati tangazo hili likitolewa na TFF, tayari uongozi mpya chini ya rais wake Jamal Malinzi umebadili jezi zinazotumiwa katika mechi za timu ya taifa, Taifa Stars, kutoka zile zilizozoeleka na mashabiki na Watanzania wote hadi jezi mpya zinazolalamikiwa na mashabiki wengi kuwa hazina mvuto na hazionyeshi rangi halisi ya bendera ya taifa la Tanzania.
Mbunifu atakayeshinda atapata zawadi ya shilingi milioni moja za Kitanzania sawa na karibu dola mia saba za Kimarekani kwa atakayebuni jezi ya kuchezea mechi za nyumbani na vile vile mshindi atakayebuni jezi za kuchezea mechi za ugenini naye atapata kiasi kama hicho cha fedha.
Jezi ya sasa ina rangi ya samawati na bluu nyeusi
No comments:
Post a Comment