Friday 24 November 2017

EMMERSON MNANGAGWA AAPISHWA KUWA RAIS WA ZIMBABWE... JIONEE LIVE ANAVYOAPISHWA

Rais mtarajiwa wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa anatarajiwa kutawazwa leo Ijumaa, siku tatu baada ya mtangulizi wake Robert Mugabe kuachia ngazi kwa shinikizo la jeshi na chama chake cha Zanu-PF.

Aliyekua makamu wa rais anamrithi Mugabe, baada ya uhasama kati yake na mkewe Mugabe, Grace Mugabe, kutokea na kusababisha kufutwa kazi na kukimbilia nchini Afrika Kusini.

Grace Mugabe alitaka kumrithi mumewe, baada ya kukalia kiti cha makamu wa rais wa Zimbabwe.

Bw. Emmerson alirejea siku ya Jumatano jioni, siku moja tu baada ya mtangulizi wake kujiuzulu.


Kufutwa kwake kazi mwezi huu kulipelekea chama tawala cha Zanu-PF na jeshi kuingilia kati na kumlazimisha Mugabe ang'atuke .

Upinzani unamtaka Emmerson Mnangagwa, ambae amekuwa mmoja wa watawala kumaliza "utamaduni wa ufisadi".

Vyombo vya habari vya serikali vimesema kuwa Robert Mugabe atahudhuria sherehe za kuapishwa kwa Bw. Munangagwa.

Sherehe hizo zitafanyika katika uwanja wa michezo mjini Harare, huku waandalizi wakiwataka wa Zimbabwe kuhudhuria kwa wingi sherehe hizo.


UNAWEZA KUANGALIA HAPA NAMNA SWALA KA KUAPISHWA KWA RAIS WA ZIMBABWE LINAVYOENDELEA
👇👇👇👇👇👇👇👇👇

Wednesday 22 November 2017

MSANII MATATANI KWA KUTOA VIDEO AKILA NDIZI KWA MADAHA


Msanii wa kike wa muziki wa Pop nchini Misri ajulikanaye kwa jina la, Shyma amejikuta mikononi mwa polisi Jumamosi ya wikiendi iliyopita baada ya kuachia video ya wimbo wake mpya ujulikanao kwa jina la ‘ I have Issues’ kwa kosa la kuonekana akila tunda aina ya ndizi kwenye video hiyo kwa mbwembwe mbele ya wanaume.

ALIYEKUWA MAKAMU WA RAIS ZIMBABWE KUAPISHWA RASMI KAMA RAIS WA TAIFA HILO

  ​


Aliyekuwa Makamu wa Rais wa Taifa la Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa huenda akaapishwa rasmi leo au kesho kuwa Rais mpya wa nchi hiyo. Taarifa hii ni kwa mujibu wa Katibu wa Sheria wa Chama cha ANU-PF.

Bwana Mnangagwa ataliongoza taifa hilo hadi wakati wa uchaguzi mkuu mwakani. Mugabe aliwamua kujiuzulu ikiwa ni dakika chache kabla ya Bunge la nchi hiyo alijaanza mchakato wa kumuondoa kwa kura ya kutokuwa na imani naye.

Tuesday 21 November 2017

NASA ya Kenya Kumwapisha Odinga kama Rais wa kenya Jumanne

Wakati Uhuru Kenyatta anatarajiwa kuapishwa kuwa Rais wa Kenya Jumanne ya wiki ijayo, Umoja wa Vyama vya Upinzani (NASA) nchini humo pia umetangaza kuapishwa kwa Raila Odinga kuwa

CCM YAMREJESHA KUNDINI SOPHIA SIMBA UPYA

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Wanawake CCM (UWT), Sophia Simba aomba radhi na kuomba kurejea CCM baada ya kufukuzwa uanachama.
Mwenyekiti wa CCM Rais John Magufuli amesoma barua ya Sophia kuomba radhi mbele ya Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) na kuwahoji wajumbe kama wanakubali kumsamehe jambo lililokubaliwa.

Friday 17 November 2017

KENYA: ASKOFU ASLIMU NA KUGEUZA KANISA KUWA MSIKITI


Habari zilizotufikia kutoka Kenya, Askofu Charles Okwany ambaye baada ya kuichagua dini ya Kiislamu kuwa mwongozo wake wa wokovu duniani na Akhera amechagua jina la Ismail Okwany.

Amesema amesilimu baada ya kufanya utafiti wa kina kuhusu Uislamu. Amesema baada ya kusilimu, kanisa alilokuwa akihurbiri, lililoko katika eneo la Nyalgosi kaunti ya Homa Bay magharibi mwak Kenya, ambalo lilijulikana kwa jina la God’s Call Church of East Africa sasa limegeuzwa jina na kuwa Msikiti wa Jamia wa Nyalgosi.

Wananchi Mikoa Yote Kupimwa UKIMWI

MIKOA yote nchini imeagizwa kuwapima wananchi wake, virusi vya ukimwi (HIV) bure kwenye wiki ya kuadhimisha Siku ya Ukimwi.


Wiki hiyo inaanza Novemba 24 na kuisha siku ya kilele cha Siku ya Ukimwi duniani Desemba Mosi. Kaulimbiu ni “Changia mfuko, okoa maisha, Tanzania bila Ukimwi inawezekana”. Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na watu Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama alisema hayo jana.
Alikuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani yanayofanyika kitaifa Dar es Salaam. Aliagiza kupatikana wataalamu wa kutosha kwa kila mkoa kwa upimaji huo na ushauri nasaha.
Alisema katika wiki hiyo, kutazinduliwa Ripoti ya utafiti wa kitaifa wa virusi vya Ukimwi, utafiti ambao hufanyika kila miaka minne. Alitaja shughuli nyingine ni uzinduzi wa mkakati wa kondom wa kitaifa, kongamano la kitaifa la wataalamu watakaojadiliana kukabili Ukimwi na huduma ya kupima kwa hiari.


Chanzo-Habarileo

Wednesday 15 November 2017

ALiyekuwa makamu wa Rais Zimbabwe Atangazwa Kuwa rais wa Chama cha ZANU-PF



ZIMBABWE: Aliyekuwa Makamu wa Rais, Emerson Mnangagwa atangazwa kuwa Rais mpya wa Chama cha ZANU-PF
> Mapema leo atua Uwanja wa Ndege wa Jeshi wa Manyame

Jeshi la Zimbabwe la kanusha kufanya mapinduzi

Jeshi la Zimbabwe limekanusha madai kwamba mapinduzi ya kijeshi yamefanyika kuiondoa serekali, na kudai kwamba rais Robert Mugabe na familia yake wapo salama.Katika taarifa iliyotolewa na jeshi kupitia televisheni ya taifa, imeelezwa kwamba jeshi linalenga wahalifu wanaosababisha shida za kijamii na kiuchumi na kuwafikisha mbele ya sheria.

Thursday 9 November 2017

Ndoa ya Dogo Janja na Uwoya imedhibitika ni Fake: Wema sepetu ahusika

PICHA: Dogo Janja akionekana anatia saini kwenye cheti cha ndoa
Ndoa ya Irene Uwoya na Dogo Janja yabainika kuwa reel na sio real, Uwoya ampora Wema dili la million 400 toka kituo kikubwa cha TV barani Afrika !
Nyuma ya sarakasi ya kile kinachosemekana ni ndoa kati ya staa wa wa filamu nchini Irene Pancras Uwoya na dogo wa Bongo Fleva, Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’ kuna mengi, Amani limeibuka na jipya.
Ubuyu wa motomoto uliolifikia gazeti la Amani mapema wiki hii, ulidokeza kuwa, hapana shaka kuwa kilichokuwa kikiendelea kati ya Uwoya na Dogo Janja si ndoa bali ni tamthiliya inayotarajia kuanza kurushwa na kituo kikubwa cha runinga barani Afrika.

Monday 6 November 2017

HESLB yatoa majina ya mikopo awamu ya tatu 2017/2018


Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu imetoa orodha ya Awamu ya Tatu ya wanafunzi 7,901 wa Mwaka wa Kwanza waliofanikiwa kupata mikopo na hivyo kufanya jumla ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza waliopangiwa mikopo hadi sasa kufikia 29,578.