Friday 17 November 2017

KENYA: ASKOFU ASLIMU NA KUGEUZA KANISA KUWA MSIKITI


Habari zilizotufikia kutoka Kenya, Askofu Charles Okwany ambaye baada ya kuichagua dini ya Kiislamu kuwa mwongozo wake wa wokovu duniani na Akhera amechagua jina la Ismail Okwany.

Amesema amesilimu baada ya kufanya utafiti wa kina kuhusu Uislamu. Amesema baada ya kusilimu, kanisa alilokuwa akihurbiri, lililoko katika eneo la Nyalgosi kaunti ya Homa Bay magharibi mwak Kenya, ambalo lilijulikana kwa jina la God’s Call Church of East Africa sasa limegeuzwa jina na kuwa Msikiti wa Jamia wa Nyalgosi.


Katika mahojiano na Jarida la Nairobian, Ismail Okwany amesema, wakati alipokuwa muhubiri wa Kikristo alikuwa akisafiri katika miji mbali mbali ya Kenya na Tanzania hasa katika maeneo ya pwani na alipata fursa ya kufanya utafiti kuhusu maisha ya Waislamu. Ismail Okwany anaongeza kuwa aliweza kulinganisha Uislamu na Ukristo na akaamua kufuatia Uislamu.

Aidha anasema moja ya mambo yaliyokuwa yakimkera sana wakati akiwa muhubiri wa Ukristo ni tabia ya wanawake kuingia ndani ya kanisa wakiwa wamevaa sketi fupi katika hali ambayo wanawake Waislamu wanakuwa wamejisitiri kwa Hijabu wakati wa ibada msikitini na hata nje ya msikiti.

Okwany mwenye umri wa miaka 65 alisilimu tarehe 26 Septemba akiwa na wafuasi wengine 23 wa kanisa lake na sasa wako mbioni kusajili rasmi msikiti wao.

Anasema Allaah (Subhanahu wa Ta’ala):

“Nyinyi ndio Ummah bora kuliko Ummah zote zilizodhihirishiwa watu (ulimwenguni) mnaamrisha yaliyo mema na mnakataza yaliyo maovu, na mnamuamini Allaah.” Aal ‘Imraan: 110


“Sema hii ndio njia yangu, ninaita (ninalingania) kwa Allaah kwa ujuzi wa kweli, mimi (nafanya hivi) na (kila) wanaonifuata. Na Allaah Ametakasika na kila upungufu, wala mimi simo miongoni mwa wanaomshirikisha (Allaah).” Yuusuf: 108

CHANZO: JAMII FORUM

No comments: