Tuesday 21 October 2014

kocha mpya wa makipa, Mserbia Zdravkomr Djekic. ampiga chini Idd panzi

UONGOZI wa Klabu ya Simba chini Rais wake Evance Aveva, umempa mkataba wa miezi miwili kocha mpya wa makipa, Mserbia Zdravkomr Djekic.
Uteuzi wa Mserbia huyo umekuja siku chache tu tangu aliyekuwa Kocha wa makipa, Idd Pazi kuachwa katika safari ya timu hiyo nchini Afrika Kusini.
Japo hadi sasa uongozi wa Klabu hiyo haujatamka rasmi kumtema Pazi kwa hoja kuwa bado yupo katika nafasi hiyo, uteuzi wa Mserbia huyo kunathibitisha hilo.
Katibu Mkuu wa Simba, Stephen Ally, alisema jana kuwa hana taarifa ya Pazi kuachwa, hivyo ataendelea kuwepo katika benchi la ufundi.
Alisema ndio maana wamempa Mserbia huyo mkataba wa muda mfupi wa kutekeleza programu fupi ya timu yao huku Pazi akiendelea kuwa kocha wa makipa wa Simba kama kawaida.
Katika hatua nyingine, Ally alisema timu imeanza mazoezi jana jioni katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kujipanga zaidi kwa mechi dhidi ya Tanzania Prisons ya Mbeya.
Alisema kesho timu inatarajia kwenda jijini Mbeya kwa mechi hiyo itakayochezwa Jumamosi katika uwanja wa Sokoine jijini humo, ikiwa ni mara ya kwanza Simba kucheza nje ya Uwanja wa Taifa katika msimu huu.

No comments: