Tuesday 28 January 2014

Maadhimisho ya miaka 50 TICD -TENGERU ya vuruga na ATC

hii n timu ya mpira TICD_Tengeru
Chuo cha maendeleo ya jamii Tengeru (TICD) kimeanza vibaya maadhinisho ya miaka 50 ya chuo,wakiona cha mtema kuni wachapwa 1 0 na timu ya ATC ,Timu yampira wa miguu ya chuo hicho yanyolewa bila maji na Arusha Technical college (ATC)
Mchezo huo ulikuwa wakuvutia huku kila timu ikitafuta goli la mapema. Mnamo dakika ya 25 ya mchezo timu ya ATC ilijipatia kona ya kwanza katika mchezo lakin ilishindwa kuza matunda baada ya golikipa wa TICD Paul kuokoa mpira huo wa hatari , lakin baada ya dakika mbili tu nusura TICD wajipatie goli la mapema baada ya mshamuliaji wake machachari Godson Lema kupiga shuti kali lakin mlinda mlango wa ATC alikuwa makin na kuokoa shuti hilo .
Mchezo ulikuwa mzuri kipindi cha kwanza timu zote zilikuwa zina shambuliana kwa zamu lakin hadi mapumziko kipindi cha kwanza “Half Time” hakuna timu iliyo fanikiwa kuona lango la wenzie

Baada ya dakika moja tu kipindi cha pili kuanza dakika ya 46 mabeki wa TICD walifanya uzembe kwa kutegeana mpira na kumfanya mshambuliaji hatari wa ATC aliyekuwa amevalia jezi nambari 9 Musa alifanikiwa kumpokonya beki wa TICD na kupiga shuti kali lililo mshinda mlinda mlango wa TICD Paul john na kumwacha njia panda bila kujia la kufanya.
Mnamo dakika ya 60 timu ya TICD ililisakama lango la ATC bila mafanikio . Dakika ya 70 ya mchezo Mwamuzi ALLEN alilazimika kumwonyesha kadi ya njano mshambuliaji wa TICD Godbles Lema baada ya kumlalamikia mwamuzi kwa kuwanyima penalti baada ya mchezaji mwenzake alimaarufu kama “CHICHARITO” kufanyiwa madhambi ndani ya box
Mnamo dakika ya 79 timu zote mbili zilifanya mabadiliko kwa kuwatoa wachezaji wawili wawili kila timu lakim mabadiliko hayo hayakozaa matunda katika timu ya TICD , hadi mwamuzi wa kati Allen akipuliza kipenga cha mwisho TICD(Tengeru Instutute of community development) 0 1 ATC (Arusha technical college )

No comments: