Thursday 30 January 2014

Balotel alimwa fain

MSHAMBULIAJI wa AC Milan, Mario Balotelli, amepigwa faini ya pauni 8,200 kwa kuwaoneshea ishara mashabiki wa Cagliari baada ya kufunga katika ushindi wao wa mabao 2-1 Jumapili.
Balotelli (23) alipewa kadi ya njano kwa kuonesha kitendo kisicho cha uanamichezo baada ya kusawazisha dakika ya 87.
Kwa mujibu wa BBC, hiyo ilikuwa kadi yake ya njano ya nane ya msimu, ambayo inamaanisha hatacheza mchezo wa Jumamosi dhidi ya Torino.
Balotelli alitolewa nje ya uwanja mapema msimu huu kwa kuwatukana waamuzi mwisho wa mchezo dhidi ya Napoli.
"Balotelli atajifunza," kocha wa Italia, Cesare Prandelli, alisema mapema juzi.
"Atahitaji upendo mwingi, ni mtu anayeifanyia mengi Milan na muhimu kwa timu hiyo," alisema Prandelli.

No comments: