Monday 6 January 2014

Ushindi wa vinara wa ligi kuu ya England Arsenal dhidi ya wapinzani wao wa jadi wa jiji la London,Tottenham, Jumamosi kunawapambanisha na Coventry City walio daraja la kwanza katika mzunguko wa nne wa kombe la FA.

Katika mchezo huo Arsenal iliichakaza Tottenham magoli 2-0.
Arsenal, The Gunners, ambao waliondolewa na Blackburn Rovers katika mzunguko wa tano wa mashindano kama hayo mwaka 2013, itapenda kufanya vyema ili kutwaa kombe la FA ambalo kwa mara ya mwisho ililitwaa mwaka 2005.
Taarifa zinazohusiana


Nayo Swansea, kwa kuichapa Manchester United 2-1 katika uwanja wake wa nyumbani wa Old Trafford, Jumapili ni fursa ya kupambana na moja wapo ya timu za Birmingham City, Bristol Rovers ya daraja la pili au Crawley ya

daraja la kwanza- huku mechi ya Crawley ya mzunguko wa pili iliyoahirishwa ikiwa bado kuchezwa.

Mabingwa watetezi wa kombe hilo Wigan wataikaribisha Crystal Palace iwapo wataifunga MK Dons katika mechi yao ya marudiano baada ya timu hizo kwenda sare ya 3-3 Jumamosi.
Ratiba ya Kombe la FA mzunguko wa nne:

Sunderland kupambana na Kidderminster au Peterborough

Bolton kupambana na Cardiff

Southampton itapambana na Yeovil

Huddersfield itakabiliana na Charlton au Oxford

Port Vale au Plymouth itachuana na Brighton

Nottingham Forest itamenyana na Ipswich au Preston

Southend na Hull

Rochdale dhidi ya Macclesfield au Sheffield Wednesday

Arsenal uso kwa uso na Coventry

Stevenage itaonyeshana kazi na Everton

Wigan au MK Dons itanyukana na Crystal Palace

Chelsea dhidi ya Stoke

Blackburn au Manchester City itapepetana na Bristol City au Watford

Bournemouth au Burton kivumbi dhidi ya Liverpool

Birmingham, Bristol Rovers au Crawley itacheza dhidi ya Swansea

Sheffield United itapambana na Norwich au Fulham

Mechi hizo za mzunguko wa nne zitachezwa kati ya tarehe 25 na 26 mwezi Januari, 2014.

No comments: