Polisi wanasema kuwa alikuwa na mtoto msichana anayekisiwa kuwa na miezi 3.
Aidha anasemekana kumuuliza mpita njia iwapo angependa kumnunua mtoto aliyekuwa katika kigari cha kuwakokota watoto.
Polisi waliitwa na mara moja wakamtia mbaroni kwa makosa ya kumtelekeza mtoto.
Mtoto huyo yuko chini ya ulinzi wa serikali na anasemekana kuwa yuko katika hali nzuri kiafya.
Inspekta Liam Boden anasema kuwa watamhoji kuhusiana na madai hayo huku upelelezi wa kina ukianza.
No comments:
Post a Comment