Tuesday 28 July 2015

Mbunge wa Viti maalumu Chadema atimkia ACT

Wakati vuguvugu la uchaguzi mkuu wa rais,wabunge na madiwani likiendelea kwa kasi mbunge wa viti maalum kwa tiketi ya chama cha demokrasi na mendeleo chadema Bi.Chiku Abwao amejitoa katika chama hicho na kujiunga rasmi na  chama cha ACT wazalendo.
Bi.Abwao amesema ameridhishwa na uongozi wa ACT-wazalendo, katiba na ilani ya uchaguzi wa chama hicho hadi kumpelekea kuamua kujiunga kwa vile kinalenga kumkomboa mtanzania masikini pamoja na kuweka msingi imara ya maadili ya viongozi.

Awali akizungumza kwa niaba ya katibu mkuu wa ACT-wazalendo, katibu wa mipango na mikakati  Bwana Mchanga Habibu amesema chama cha ACT-wazalendo kimepata maendeleo makubwa kwa muda mfupi kutokana na kuwa katiba bora, kufuata azimio la Tabora na ilani ya uchaguzi iliyobora hali inayochangia wanasiasa wengi kujiunga na ACT kwa kuwa ndio chama kinacholenga kuwakomboa wananch

No comments: