Tuesday 28 July 2015

Tatizo la mashine kutotambua alama za vidole limejitokeza katika baadhi ya vituo jijini DSM

Tatizo la mashine kutokutambua alama za vidole limejitokeza kwa baadhi ya vituo wakati zoezi la uandikishaji likiendelea jijini Dar es Salaam na kusababisha mashine kuzima zaidi ya mara sita huku tatizo la ubovu wa mashine na waandikishaji wasiokuwa na uzoefu likiendelea kulalamikiwa.
Licha ya kuwepo kwa malalamiko tangu siku ya kwanza ya zoezi hili kuanza hapa jijini lakini mamlaka husika zimeonekana kushindwa kuyatatua kwa wakati hali inayopelekea msongamano kwa baadhi ya vituo kutokupungua na watu kulazimika kuamka usiku wa manane kuwahi namba za uandikishwaji siku moja kabla.
 
TanzaniaOne blog imetembelea vituo mbalimbali na kushuhudia wananchi wakiwa wamejipumzisha vivulini na wengine wakichapa usingizi wakisubiri kuitwa majina huku kina mama wenye watoto wakilalamikia kutokupewa kipaumbele.
 
Baadhi ya waandikishaji waliozungumza na Ukomboz Blog wamedai kuwa tatizo la vidole vya baadhi ya wananchi kutokusoma kwenye mashine limekuwa likijitokeza mara kwa mara na kulazimika kutumia muda mwingi kuhudumia mtu mmoja hali inayozua kelele kwa watu waliopo kwenye foleni.
 
Kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi Temeke akizungumzia zoezi hilo amesema changamoto ambayo wamekuwa wakikabiliana nayo mara kwa mara ni watu kupiga simu vituoni hasa wanapoona wenzao hawafuati utaratibu na kuongeza kuwa hakuna aliyeshikiliwa kutokana na vurugu zinazojitokeza katika vituo hivyo.

No comments: