Sunday, 13 March 2016

Awadhi Juma aiweka Simba kilelen leo dhid ya Prison

Wakati watani zao wa jadi Yanga wamemaliza kucheza mchezo wao wa kwanza wa raundi ya pili katika michuano ya klabu bingwa Afrika dhidi ya APR ya Rwanda kwa ushindi wa goli 2-1 March 12, Simba wao wameshuka dimbani March 13 kuendeleza harakati zao za kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania bara.

Simba wameshuka dimbani kucheza dhidi ya klabu ya wajelajela wa Mbeya Tanzania Prisons, katika mchezo wao 23 wa Ligi Kuu Tanzania bara. Simba waliingia uwanjani kuhakikisha wanapata point tatu ili waendelee kuwa katika nafasi nzuri ya kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania bara.

Rais Magufuli kateua Wakuu wapya wa mikoa… yumo na Paul Makonda,

Magufuli awateua wakuu 13 wapya wa mikoa
Rais wa Tanzania amewateua wakuu 13 wapya wa mikoa miongoni mwa orodha mpya ya wakuu 26 wa mikoa iliyotangazwa leo na ikulu ya rais.
Rais John Pombe Magufuli amewahifadhi wakuu 13 waliohudumu katika serikali ya Jakaya Kikwete.
Uteuzi huo umetangazwa na katibu mkuu kiongozi, Mussa Ibrahim Iyombe.

Saturday, 12 March 2016

Mh. Esther Bulaya kaachiwa huru

Mh Estar bulaya mbunge wa bunda akiwa kwenye office ndogo za bunge jiji daresalam baada yakuachiwa huru na mda huu anaelekea airport kwa ajiri ya safari yakwenda mwanza kwenye kikao cha kamati kuu..

Yanga yaichapa APR 2-1


YANGA SC imejiweka kwenye nafasi nzuri ya kuingia hatua ya mwisho ya mchujo ya Ligi ya Mabingwa Afrika, baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya wenyeji APR katika mchezo wa kwanza wa raundi ya Kwanza jioni ya leo Uwanja wa Amahoro, Kigali, Rwanda.
Asante kwa wafungaji wa mabao hayo, beki Juma Abdul Jaffar kipindi cha kwanza na kiungo Thabani Scara Kamusoko kipindi cha pili na Yanga sasa watahitaji hata sare mchezo wa marudiano ili kusonga mbele

Mkutano wa Donald Trump wakumbwa na ghasia

Donald Trump
Mkutano ulipangwa kufanyika katika jimbo la Chicago nchini Marekani wa mgombea wa chama cha Republican Donald Trump umehairishwa baada ya kutokea maandamano.
Mkutano huo ulifutwa pia kutokana na sababu za kiusalama baada ya bwana Trump kukutana na maafisa wanaohusika na masuala ya usalama wa eneo hilo.

Kizimbani kwa kusema Rais Mugabe ni Mzee

Rais Mugabe
Afisa mmoja wa polisi amefikishwa mahakamani nchini Zimbabwe baada ya kulaumiwa kwa kusema kuwa rais Robert Mugabe ambaye sasa ana umri wa miaka 92 ni mzee sana kuwa kiongozi.
Thomson Joseph Mloyi pia anadaiwa kumtusi mkewe rais Mugabe, Grace, kuwa kahaba kwa mujibu wa gazeti la kibinafsi nchini humo.

Friday, 11 March 2016

Ben Carson amuunga mkono Donald Trump

Carson na Trump
Aliyekuwa mgombea wa urais kupitia chama cha Republican Ben Carson amethibitisha kwamba anamuunga mkono aliyekuwa mpinzani wake Donald Trump katika kinyang'anyiro cha urais nchini Marekani.
Carson alimuidhinisha katika mkutano wa pamoja na wanahabari mjini Florida huku Trump akiwa anaongoza katika kura ya mchujo wa kumtafuta atakayewania urais kupitia chama hicho kabla ya Jumanne kuu.
Bwana Carson ,aliye kifua mbele aling'atuka wiki iliopita baada ya kushindwa kuungwa mkono.