Simba wameshuka dimbani kucheza dhidi ya klabu ya wajelajela wa Mbeya Tanzania Prisons, katika mchezo wao 23 wa Ligi Kuu Tanzania bara. Simba waliingia uwanjani kuhakikisha wanapata point tatu ili waendelee kuwa katika nafasi nzuri ya kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania bara.
Sunday, 13 March 2016
Awadhi Juma aiweka Simba kilelen leo dhid ya Prison
Simba wameshuka dimbani kucheza dhidi ya klabu ya wajelajela wa Mbeya Tanzania Prisons, katika mchezo wao 23 wa Ligi Kuu Tanzania bara. Simba waliingia uwanjani kuhakikisha wanapata point tatu ili waendelee kuwa katika nafasi nzuri ya kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania bara.
Rais Magufuli kateua Wakuu wapya wa mikoa… yumo na Paul Makonda,
Rais wa Tanzania
amewateua wakuu 13 wapya wa mikoa miongoni mwa orodha mpya ya wakuu 26
wa mikoa iliyotangazwa leo na ikulu ya rais.
Rais John Pombe Magufuli amewahifadhi wakuu 13 waliohudumu katika serikali ya Jakaya Kikwete.Uteuzi huo umetangazwa na katibu mkuu kiongozi, Mussa Ibrahim Iyombe.
Saturday, 12 March 2016
Mh. Esther Bulaya kaachiwa huru

Mh Estar bulaya mbunge wa bunda akiwa kwenye office ndogo za bunge jiji
daresalam baada yakuachiwa huru na mda huu anaelekea airport kwa ajiri
ya safari yakwenda mwanza kwenye kikao cha kamati kuu..
Yanga yaichapa APR 2-1

YANGA SC imejiweka kwenye nafasi nzuri ya kuingia hatua ya mwisho ya mchujo ya Ligi ya Mabingwa Afrika, baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya wenyeji APR katika mchezo wa kwanza wa raundi ya Kwanza jioni ya leo Uwanja wa Amahoro, Kigali, Rwanda.
Asante kwa wafungaji wa mabao hayo, beki Juma Abdul Jaffar kipindi cha kwanza na kiungo Thabani Scara Kamusoko kipindi cha pili na Yanga sasa watahitaji hata sare mchezo wa marudiano ili kusonga mbele
Mkutano wa Donald Trump wakumbwa na ghasia
Donald Trump
Mkutano ulipangwa
kufanyika katika jimbo la Chicago nchini Marekani wa mgombea wa chama
cha
Republican Donald Trump umehairishwa baada ya kutokea maandamano.
Mkutano
huo ulifutwa pia kutokana na sababu za kiusalama baada ya bwana Trump
kukutana na maafisa wanaohusika na masuala ya usalama wa eneo hilo.Kizimbani kwa kusema Rais Mugabe ni Mzee
Afisa mmoja wa
polisi amefikishwa mahakamani nchini Zimbabwe baada ya kulaumiwa kwa
kusema kuwa rais Robert Mugabe ambaye sasa ana umri wa miaka 92 ni mzee
sana kuwa kiongozi.
Thomson Joseph Mloyi pia anadaiwa kumtusi mkewe rais Mugabe, Grace, kuwa kahaba kwa mujibu wa gazeti la kibinafsi nchini humo.Friday, 11 March 2016
Ben Carson amuunga mkono Donald Trump
Aliyekuwa mgombea
wa urais kupitia chama cha Republican Ben Carson amethibitisha kwamba
anamuunga mkono aliyekuwa mpinzani wake Donald Trump katika
kinyang'anyiro cha urais nchini Marekani.
Carson alimuidhinisha
katika mkutano wa pamoja na wanahabari mjini Florida huku Trump akiwa
anaongoza katika kura ya mchujo wa kumtafuta atakayewania urais kupitia
chama hicho kabla ya Jumanne kuu.Bwana Carson ,aliye kifua mbele aling'atuka wiki iliopita baada ya kushindwa kuungwa mkono.
Subscribe to:
Posts (Atom)