Sunday, 8 May 2016

Msichana Asiye na Mikono Ashinda tuzo la Muandiko Bora

Anaya Ellick kutoka Chesapeake, Virginia hatumii viungo vya kumsaidia wakati anapoandika.

Wakati anapoandika yeye husimama huku akishikilia kalamu yake katika mikono.

Mwalimu wake mkuu Tracy Cox kutoka shule ya Greenbrier Christian amemtaja kuwa mtu wa mfano mwema.

Akata sehemu za siri za mkewe ili apate mtaji

Mwanamke mwenye umri wa miaka 60 , anadai kukatwa sehemu zake za siri (nyeti) na mumewe aliyemtaja kwa jina moja la Mashaka ili akauze Sh. milioni tano za Kitanzania akauze kwa mganga wa kienyeji ili apate mtaji.Mwanamke mwenye umri wa miaka 60 aliyekatwa sehemu zake za siri (nyeti) na mumewe anayefahamika kwa jina moja la Mashaka. Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo baya,

Mwanamke huyo anadai kujeruhiwa na mumewe usiku wakati wakiwa wamelala nyumbani kwao
Akizungumza na mwanahabari wetu kwa tabu akiwa wodini kwenye hospitali hiyo akiwa na maumivu makali, mama huyo alikuwa na haya ya kusema:
“Siku ya tukio, nakumbuka mume wangu alikwenda kutembea, aliporejea nyumbani alifuatana na mtu mmoja ambaye ni mganga wa kienyeji.“ Walipofika nyumbani aliniambia yupo na mganga wa kienyeji ambaye alikuwa akitafuta viungo vya sehemu za siri za mwanamke akiwa na fedha milioni tano

Saturday, 7 May 2016

Mchezaji mwingine wa Cameroon afia uwanjani , Angalia VIDEO HAPA

 
Kama ni mfuatiliaji mzuri wa mitandao ya soka barani Ulaya huenda utakuwa umekutana na taarifa za kusikitisha kwa taifa la Cameroon, usiku wa May 6 2016 Cameroon na Afrika  kwa ujumla ilipata taarifa za kushtusha, baada ya kupokea taarifa za kifo cha kiungo wa kimataifa wa Cameroon aliyekuwa anaicheze Dinamo Bucuresti Patrick Ekeng.

Monday, 2 May 2016

Diamond Azipangua Shutuma za Kutoka na Mrembo Lyyn..Adai Wanajaribu Lakini Zari Ndio Roho yake


Diamond Ameamua Kuwakata watu vidomo wanaosema kuwa yeye na Zari kwa sasa hakuna mawasiliano mazuri kisa mrembo aliyecheza kwenye video mpya ya Rayvan...kwa kumpost Zari kwenye page yake ya Instagram...Tetesi za Diamond kutoka na msichana huyo zimekuwa gumzo kubwa instagram ....

Roho ya SIMBA!!!.... wanajaribu ila hawatokaa Waweze... Nakupenda Mpaka Naugua! @Zarithebosslady 😙 #Mmechelewa

Trump achekwa kwa alivyotamka Tanzania

TrumpTrump alishambulia sana sera ya kigeni ya Obama
Mgombea urais wa chama cha Republican Donald Trump amekejeliwa mtandaoni baada ya kuonekana akiboronga akitamka Tanzania wakati wa kutoa hotuba.
Bw Trump alikuwa akizungumzia mashambulio ya kigaidi yaliyotekelezwa katika mabalozi ya Marekani nchini Kenya na Tanzania mwaka 1998 wakati wa kuzungumzia sera yake ya kigeni.
Badala ya kutamka vyema ‘Tanzania’ anasikika akitamka ‘Tan-zay-nia’.

Binti wa Obama, Malia kusomea Havard

Binti ya Obama, Malia kusomea Havard
Mwanaye rais wa Marekani Barack Obama,Malia,amefuzu kujiunga na chuo kikuu cha Havard.
Taarifa kutoka ikulu ya White House imesema kuwa Malia ambaye amekuwa mapumzikoni baada ya kuhitimu masomo ya chuo cha upili, atajiunga na chuo hicho cha kifahari mwakani.
Malia ataendelea na likizo yake kabla ya kujiunga na Havard mwakani.'' taarifa hiyo ya ikulu ilielezea.

Magufuli apunguza kodi ya mapato na 2% kutoka 11% hadi 9%

Magufuli apunguza kodi ya mapato na 2%

Huku wafanyikazi kote duniani wakiadhimisha sikukuu ya wafanyakazi, nchini Tanzania, wafanyikazi wanakila sababu ya kutabasamu.
Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli amewaongezea wafanyikazi wote nchini humo asilimia mia mbili 2% mishahara.
Katika hotuba ya kuadhimisha siku ya wafanyikazi, bw Magufuli alitangaza kupunguzwa kwa kodi ya mapato PAYE kutoka asilimia 11% hadi asilimia 9%.
Hii inamaanisha kuwa kila mfanyikazi atapata ongezeko la mapato yake kwa asilimia 2%.
Magufuli alitangaza kauli hiyo kufuatia ombi la wafanyikazi kupitia kwa katibu mkuu bwana Nicholus Mgaya la kutaka wanusuriwe makali ya mfumuko wa bei ya bidhaa muhimu.