Saturday, 14 November 2015

Ubelgiji yashauri raia wake waondoke Burundi

Burundi
Raia wa Burundi wamekuwa wakitoroka mitaa mingi ya mji wa Bujumbura
Ubelgiji imewashauri raia wake kuondoka Burundi, huku Muungano wa Ulaya nao ukipunguza maafisa wake wanaohudumu huko kutokana na kuongezeka kwa machafuko.
Balozi wa EU nchini humo Patrick Spirlet amesema hatari ya kutokea mapigano zaidi imeongezeka.
Hayo yamejiri huku idara ya Amani ya Usalama ya Muungano wa Afrika ikikutana mjini Addis Ababa kujadili mpango wa kutuma walinda amani nchini humo.

Watu 120 wameuawa katika ukumbi wa sanaa wa Bataclan, katikati mwa mji wa Paris.

ParisMashambulio kadha yametokea mjini Paris
Ufaransa imetangaza hali ya hatari na kufunga mipaka yake baada ya watu zaidi ya 120 kuuawa kwenye mashambulio kadha mjini Paris.
Watu 120 wameuawa katika ukumbi wa sanaa wa Bataclan, katikati mwa mji wa Paris.
Watu wenye silaha walishika mateka watu waliokuwa kwenye ukumbi huo kabla yao kuzidiwa nguvu na maafisa wa polisi.
Watu wengine waliuawa kwenye mlipuko uliotokea karibu na uwanja wa michezo wa taifa wa Stade de France ambako mechi ya kirafiki kati ya Ufaransa na Ujerumani ilikuwa ikiendelea.

Wednesday, 11 November 2015

Buhari atangaza baraza lake la mawaziri

AdeosunBi Adeosun ameteuliwa waziri wa fedha
Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari hatimaye ametangaza wizara na mawaziri watakaozisimamia, miezi saba baada yake kushinda uchaguzi wa urais.
Nafasi muhimu ya waziri wa fedha ameikabidhi mwanauchumi Kemi Adeosun, aliyesomea Uingereza kabla ya kurejea Nigeria na kuhudumu kama kamishna ya fedha jimbo la Ogun.
Jenerali mstaafu Mansur Dan Ali atakuwa Waziri wa Ulinzi, na kazi yake kuu itakuwa kuongoza vita dhidi ya wanamgambo wa Boko Haram.
Gavana wa zamani wa jimbo la Lagos Babatunde Fashola ameteuliwa waziri wa kawi, ujenzi na makazi na anakabiliwa na kibarua cha kutatua mzozo wa umeme Nigeria.
Mwanasiasa mkongwe ambaye pia ni mkulima Audu Ogbe ameteuliwa waziri wa kilimo.
Nigeria ina ardhi kubwa ambayo ikutumiwa vyema inaweza kubuni nafasi za kazi na kupunguza utegemezi wa mafuta, wadadisi wanasema.
Kuzinduliwa kwa baraza hilo lenye mawaziri 36 kumefanyika miezi saba baada ya uchaguzi wa urais.
Buhari
Buhari alishinda uchaguzi uliofanyika Machi
Bw Buhari aliyechaguliwa Machi alikuwa ameahidi kukabiliana na ufisadi na ukosefu wa usalama, na aliahidi kuteua watu wenye ujuzi na wasio na ila.
Mhariri wa BBC Hausa Mansur Liman anasema baraza hilo la Rais Buhari litashangaza watu na hasa uteuzi wa Bi Adeosun kuwa waziri wa fedha. Wengi walitarajia Okechukwu Enelemah, aliyeteuliwa waziri wa biashara na uwekezaji, angeteuliwa waziri wa fedha.
Rais Buhari pia ameshangaza wengi kwa kumteua mkuu wa zamani wa jeshi Jenerali Abdurrahman Dambazau kuwa waziri wa mambo ya ndani. Wengi walitarajia angeteuliwa waziri wa ulinzi.
Amina Mohammed, mshauri wa zamani wa mkuu UN Ban Ki-Moon kuhusu maendeleo endelevu, alitarajiwa kuteuliwa waziri wa mipango lakini ameteuliwa waziri wa mazingira.

Mchezaji achunguzwa kwa kutishia mbwa

OaklandKlabu ya mchezaji huyo ilishindwa kwenye mechi hiyo
Mchezaji wa Oakland Raiders Ray-Ray Armstrong anachunguzwa na maafisa wa polisi kwa tuhuma za ‘kubweka’ na kujipiga kifua mbele ya mbwa wa polisi.
Armstrong, 24, anadaiwa kuinua shati lake na kumchokoza mbwa huyo kabla ya mechi ya NFL dhidi ya Pittsburgh Steelers Jumapili.
Akipatikana na hatia, huenda akashtakiwa na kosa la kumchokoza mbwa wa polisi, ambalo ni kosa la ngazi ya tatu jimbo la Pennsylvania.

Teodore Obiang kuwania tena urais Equatorial Guinea

ObiangObiang ameongoza taifa hilo kwa miaka 36
Rais wa Equatorial Guinea Teodoro Obiang Nguema, ambaye ameongoza taifa hilo kwa miaka 36, amesema atawania tena, shirika la habari la AFP limeripoti.
Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 73 alisema kupitia kituo cha redio cha taifa kwamba ameungwa mkono na chama chake kuwania urais kwa muhula mwingine wa miaka saba mwaka ujao.
Chama cha Obiang cha Democratic Party of Equatorial Guinea kilishinda viti 99 kati ya 100 vya ubunge katika uchaguzi mkuu wa 2008.
Alishinda uchaguzi wa urais mwaka mmoja baadaye kwa kupata 95% ya kura.
Obiang ni mmoja wa viongozi waliokaa madarakani muda mrefu zaidi Afrika.

Tuesday, 18 August 2015

Wanachama wa CCM waandamana kibondo kupinga uteuzi wa mgombea ubunge

Mamia ya wanachama wa chama cha mapinduzi CCM katika wilaya ya Kibondo wameanadamana na kuvamia ofisi za chama hicho wakipinga mgombea aliyeshinda katika kura za maoni Jamal Abdalah kutoteuliwa na halmashauri kuu ya taifa ya CCM kuwania ubunge katika jimbo la Muhambwe wilayani Kibondo.

Wanachama wa CCM waandamana kibondo kupinga uteuzi wa mgombea ubunge

Mamia ya wanachama wa chama cha mapinduzi CCM katika wilaya ya Kibondo wameanadamana na kuvamia ofisi za chama hicho wakipinga mgombea aliyeshinda katika kura za maoni Jamal Abdalah kutoteuliwa na halmashauri kuu ya taifa ya CCM kuwania ubunge katika jimbo la Muhambwe wilayani Kibondo.