Mahakama ya juu zaidi nchini Uganda imefutilia mbali kesi iliyokuwa ikipinga ushindi wa rais Yoweri Museveni katika uchaguzi wa urais uliofanyika mwezi uliopita.
Mahakama hiyo ilisema kuwa licha ya kuwepo kwa dosari nyingi za uchaguzi, matokeo ya mwisho hayakuathiriwa.
Kundi la watoa misaada 10 kutoka nchi za magharibi wametangaza kusitisha ufadhili wao kwa bajeti ya serikali ya Tanzania.
Hii inafuatia uamuzi wa shirika la utoaji misaada la serikali ya marekani kuondoa msaada wa dola 472 wa kufadhili miradi ya maendeleo kutokana na jinsi uchaguzi wa kisiwa cha Zanzibar ulivyoendeshwa.
Karibu theluthi moja ya bajeti ya Tanzania ilitegemea msaada mwaka uliopita, kwa hivyo hatua hizo za hivi punde ni pigo kwa mipango ya maendeleo ya serikali mpya.
Wanariadha
waliokuwa wanakimbia mbio ndefu za marathon walijipata wamekula sabuni
baada ya kudhania kwamba zilikuwa chakula kutokana na kukosa kuelewa
lugha ya kiingereza.
Takriban wanariadha 20,000 katika mbio za
Qinyuan marathon kusini mwa mkoa wa Guangdong nchini Uchina walipata
zawadi mda mfupi baada ya kumaliza mbo hizo katika utepe kulingana na
gazeti la kila siku nchini humo la Peoples daily.
Wakidhania kwamba walikuwa wanakula chakula,wanariadha hao badala yake walikuwa sabuni zilokuwa zikinuka harufu nzuri .
Raia wa Mexico
wanaosherehea sikukuu ya pasaka wamekuwa wakichoma sanamu za mgombea wa
kiti cha urais kupitia chama cha Republicans Donald Trump.
Mojawapo
ya tukio hilo la kushangaza limefanyika katika kitongoji kimoja cha
wakaazi walio na kipato cha chini kiitwacho La Merced.
Wakaazi
wengi wa La Merced wamejitokeza kushuhudia kuchomwa kwa kikaragosi cha
Trump badala ya kile cha yule mfuasi wa Yesu Kristu aliyemsalito Judas
Iscariot.
Tanzania imehuzunishwa na hatua ya bodi ya shirika la changamoto za milenia (MCC) kusitisha msaada
wake wa awamu ya pili wa dola milioni 472.8 ambazo ni
sawa na shilingi trilioni moja pesa za Tanzania.
Waziri wa mambo
ya nje wa Tanzania Bw Augustine Mahiga ameelezea kushtushwa kwake na
hatua hiyo ya bodi ya MCC akisema "imepuuza hatua kubwa tu zilizopigwa
kidemokrasia" nchini humo.
''Inasikitisha kuwa demokrasia yetu inatathminiwa tu na matokeo ya uchaguzi wa visiwani Zanzibar,'' Waziri wa mambo ya nje bwana Augustine Mahiga
Kuhusiana na uchaguzi wa Zanzibar Bw Mahiga anasema
kuwa Tanzania, ilifanya kila kitu kuambatana na sheria na katiba ya nchi
wala hakuna tatizo ama ukiukwaji wa sheria.
Mahiga anasema kuwa huo ni uamuzi wao na kwa sababu hela hizo ni
zao wanauhuru wa kuzitumia watakavyo ila anahoji kwanini uamuzi huo
uliafikia bila ya majadiliano na serikali ya muungano ya Tanzania.
Kocha wa zamani wa Leicester Nigel Pearson amepewa kipaumbele kuja
kuchukua mikoba ya kocha wa Aston Villa Mfaransa Remi Garde
anayetegemewa kutimuliwa siku za hivi karibuni. (Chanzo Daily Mail)
Shirikisho la soka nchini Uingereza (FA) linataka kujaribu kwa mara ya
mwisho kumzuia mshambuliaji wa Arsenal Alex Iwobi, 19, kuchukua uraia wa
Nigeria. (Chanzo Daily Mirror)
Mabingwa wa nchini Italia Juventus watajaribu kumsajili mshambuliaji wa
Arsenal Oliver Giroud, 29, mwishoni mwa msimu ikiwa watamkosa chaguo lao
namba moja, Edison Cavani, 29, wa Paris St-Germain. (Chanzo Tuttosport
kupitia Daily Express)
Watu
wawili wamefariki dunia kwa maradhi ambayo dalili zake zinafanana na ugonjwa wa
ebola.
Mkuu
wa Kitengo cha Uchunguzi wa Magonjwa MNH, Dk Praxeda Ogweyo alisema wamewapokea
wagonjwa hao wawili, lakini vipimo havijaonyesha kama wana ebola.
“Ni kweli kuwa tumewapokea wagonjwa hao wawili na vipimo vya mgonjwa wa kwanza
kinaonyesha hana ebola, lakini bado wanaendelea kufanya uchunguzi wa kina kujua
ni ugonjwa gani,” alisema.