Sunday 7 February 2016

Leicester City yatembeza kichapo kwa Manchester City kwenye uga wa Etihad

Leicester City yatembeza kichapo kwa Manchester City kwenye uga wa Etihad
Ligi ya soka ya EPL nchini Uingereza iliendelea leo kwa mechi kali ya kusisimua kati ya Manchester City na Leicester City.
Wenyeji Manchester City walitapatapa mbele ya mashabiki wao na kushindwa kuondoka na ushindi wala sare.
Wageni Leicester City ambao wanazidi kutia fora msimu huu, walitamba mbele ya Manchester City na kufanikiwa kuwacharaza 3-1.
Magoli ya Leicester City yalifungwa na Robert Huth katika dakika ya 3 na 60, na Riyad Mahrez katika dakika ya 60.
Sergio Aguero aliifungia Manchester City goli la kufutia machozi katika dakika ya 87.
Ushindi huo umeiwezesha Leicester City kuendelea kujikita kileleni na pointi 53 huku Manchester City ikibakia na pointi 47.

No comments: