Saturday 6 February 2016

Mwanamume ‘aliyeota mizizi’ Bangladesh

Abdul Bajandar 
Familia ya Abdul Bajandar ilishindwa kugharimia matibabu yake
Serikali ya Bangladesh imesema itagharimia upasuaji wa kumtibu mwanamume ambaye anaugua ugonjwa unaofanya mtu kupata dutu zinazofanana na mizizi ya mti mwilini.
Waziri wa afya wa Bangladesh Mohammad Nasim alitangaza hilo baada ya kumtembelea Abul Bajandar, hospitalini Alhamisi.
Bw Bajandar anaugua ugonjwa ambao kisayansi unajulikana kama epidermodysplasia verruciformi.
Ni ugonjwa wa kinasaba ambao humfanya mtu kuota vidutu kwenye ngozi. Hujulikana sana kama “ugonjwa wa binadamu mti”.

Alianza kuota vidutu miaka 10 iliyopita.
“Awali, nilidhani hazina madhara,” Bw Bajandar ameambia AFP.
Abdul Bajandar
"Sasa zimeongezeka na nyingine zina urefu wa inchi mbili hadi tatu katika mikono yangu miwili. Kuna nyingine miguuni,” amesema.
Bw Bajandar alisafiri India kutafuta matibabu lakini familia yake haingemudu gharama.
Sampuli za damu yake na ngozi zitapelekwa kwenye maabara moja Marekani kuchunguzwa zaidi, profesa Abdul Kalam, ambaye ni mtaalamu wa upasuaji wa ngozi ameambia BBC.
Atatibiwa nchini Bangladesh baada ya matokeo ya uchunguzi kutolewa.
Bw Bajandar ni mmoja wa watu watatu wanaougua “ugonjwa wa binadamu mti” duniani, mkurugenzi wa hospitali ya chuo cha Dhaka, Samanta Lal Sen ameambia AFP.
Ni mara ya kwanza kwetu kupata kisa kama hicho hapa Bangladesh

No comments: