Friday, 17 November 2017

Wananchi Mikoa Yote Kupimwa UKIMWI

MIKOA yote nchini imeagizwa kuwapima wananchi wake, virusi vya ukimwi (HIV) bure kwenye wiki ya kuadhimisha Siku ya Ukimwi.


Wiki hiyo inaanza Novemba 24 na kuisha siku ya kilele cha Siku ya Ukimwi duniani Desemba Mosi. Kaulimbiu ni “Changia mfuko, okoa maisha, Tanzania bila Ukimwi inawezekana”. Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na watu Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama alisema hayo jana.
Alikuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani yanayofanyika kitaifa Dar es Salaam. Aliagiza kupatikana wataalamu wa kutosha kwa kila mkoa kwa upimaji huo na ushauri nasaha.
Alisema katika wiki hiyo, kutazinduliwa Ripoti ya utafiti wa kitaifa wa virusi vya Ukimwi, utafiti ambao hufanyika kila miaka minne. Alitaja shughuli nyingine ni uzinduzi wa mkakati wa kondom wa kitaifa, kongamano la kitaifa la wataalamu watakaojadiliana kukabili Ukimwi na huduma ya kupima kwa hiari.


Chanzo-Habarileo

Wednesday, 15 November 2017

ALiyekuwa makamu wa Rais Zimbabwe Atangazwa Kuwa rais wa Chama cha ZANU-PF



ZIMBABWE: Aliyekuwa Makamu wa Rais, Emerson Mnangagwa atangazwa kuwa Rais mpya wa Chama cha ZANU-PF
> Mapema leo atua Uwanja wa Ndege wa Jeshi wa Manyame

Jeshi la Zimbabwe la kanusha kufanya mapinduzi

Jeshi la Zimbabwe limekanusha madai kwamba mapinduzi ya kijeshi yamefanyika kuiondoa serekali, na kudai kwamba rais Robert Mugabe na familia yake wapo salama.Katika taarifa iliyotolewa na jeshi kupitia televisheni ya taifa, imeelezwa kwamba jeshi linalenga wahalifu wanaosababisha shida za kijamii na kiuchumi na kuwafikisha mbele ya sheria.

Thursday, 9 November 2017

Ndoa ya Dogo Janja na Uwoya imedhibitika ni Fake: Wema sepetu ahusika

PICHA: Dogo Janja akionekana anatia saini kwenye cheti cha ndoa
Ndoa ya Irene Uwoya na Dogo Janja yabainika kuwa reel na sio real, Uwoya ampora Wema dili la million 400 toka kituo kikubwa cha TV barani Afrika !
Nyuma ya sarakasi ya kile kinachosemekana ni ndoa kati ya staa wa wa filamu nchini Irene Pancras Uwoya na dogo wa Bongo Fleva, Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’ kuna mengi, Amani limeibuka na jipya.
Ubuyu wa motomoto uliolifikia gazeti la Amani mapema wiki hii, ulidokeza kuwa, hapana shaka kuwa kilichokuwa kikiendelea kati ya Uwoya na Dogo Janja si ndoa bali ni tamthiliya inayotarajia kuanza kurushwa na kituo kikubwa cha runinga barani Afrika.

Monday, 6 November 2017

HESLB yatoa majina ya mikopo awamu ya tatu 2017/2018


Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu imetoa orodha ya Awamu ya Tatu ya wanafunzi 7,901 wa Mwaka wa Kwanza waliofanikiwa kupata mikopo na hivyo kufanya jumla ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza waliopangiwa mikopo hadi sasa kufikia 29,578.

Friday, 20 October 2017

RASMI : MATOKEO YA DARASA LA SABA 2017/18 YATANGAZWA, SOMA HAPA

Baraza la Mitihani taifa ( NECTA) limetangaza matokeo ya darasa la saba leo tarehe 20/10/2017
kupata matokeo hayo  BOFYA HAPA 👇👇👇👇
                                   MATOKEO YA DARASA LA SABA 2017/18

Thursday, 12 October 2017

MCHEZAJI WA ZAMANI WA CHELSEA NA AC MILAN GEORGE WEAH ASHINDA URAIS LIBERIA




Aliyekuwa mchezaji wa zamani wa Chelsea akitokea Ac Milani George Weah amefanikiwa kushinda nafasi  ya urais iliyoachwa wazi na aliyekuwa rais Mstaafu Eileen nchini Liberia kwa kuwabwanga washindani wenzake 19 waliokuwa wakiwania kiti hicho cha urais.