Friday, 11 March 2016

Mwanamuziki Bob Junior Akamatwa na Polisi Kwa Tuhuma za Kushirikiana na Majambazi


Msanii wa muziki wa bongo fleva Bob Junior amekamatwa na jeshi la Polisi nyumbani kwao magomeni mapipa Jijni Dar es salaam majira ya saa sita mchana wa leo.

Kwa mujibu wa chanzo cha  habari ambaye ni rafiki wa karibu wa Bob Junior ameiambia ukomboz blog.com kuwa Polisi wamemkamata Msanii huyo kwa kile walichodai kuwa wamepata taarifa kuwa Bob Junior anashirikiana na kikundi cha majambazi.

Rafiki huyo wa karibu na Bob Junior, ameiujuza mtembezi.com kuwa Msanii huyo amekuwa akipigiwa simu tangu juzi kutoka kituo cha polisi cha magomeni usalama kwamba kuna lalamiko la mtu anaye dai kutekwa na kikundi cha majambazi ambacho msanii huyo anashirikiana nacho

Friday, 4 March 2016

BREAKING: Waziri Jenister Mhagama Kafanya Maamuzi NSSF Usiku Huu...Atengua Uteuzi wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu NSSF

Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Jenister Mhagama ametengua uteuzi wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Dkt. Carina Wangwe uliotangazwa leo Dar es salaam.

Taarifa iliyotolewa usiku huu imeeleza kuwa uteuzi huo umetenguliwa kutokana na kutokamilika kwa baadhi ya taratibu, uteuzi mpya kwa mujibu wa mamlaka na sheria utakapofanyika taarifa zitatolewa kwa wananchi

Aliyesema hakuna Mungu nchin Urusi ashitakiwa

KrasnovAkipatikana na hatia, Krasnov huenda akafungwa jela mwaka mmoja
Mwanamume aliyeandika kwamba hakuna Mungu katika majibizano mtandaoni ameshtakiwa kusini mwa Urusi.
Viktor Krasnov aliripotiwa kwa polisi na wanaume wawili waliokasirishwa na lugha aliyoitumia wakati wa majibizano katika mtandao wa kijamii wa Kirusi wa VKontakte mwaka 2014.
Mtandao huyo hufanana sana na Facebook na ni maarufu sana.
Ameshtakiwa Stavropol kwa kosa la "kutusi hisia za waumini”.
"Matusi” kama hayo yaliharamishwa kisheria mwaka 2013 baada ya kesi ya Pussy Riot.
Wakati wa majibizano hayo, Bw Krasnov anadaiwa pia kupuuzilia mbali Biblia na kusema ni “mkusanyiko wa hadithi za kubuni za Wayahudi”.

Thursday, 3 March 2016

Jipu la wanaotumia majina feki Mitandaon Kutumbuliwa

Mahakama
Watu wanaobuni majina bandia katika mitandao huenda wakakabiliwa na mashtaka kulingana na maelezo yaliopendekezwa na waendesha mashtaka nchini Uingereza na Wales.
Huduma ya waendesha mashtaka inasema watu wazima ni lazima washtakiwe iwpo watatumia majina bandia katika mitandao ya kijamii ili kuwanyanyasa wengine.
Pia watu wanaoweka machapisho yasio na heshima ya uongo na kusababisha dhiki na wasiwasi pia watashtakiwa.

Magufuli na Kenyatta wazindua barabara Arusha

EACRais Kenyatta aliwasili Tanzania jana kwa mkutano wa wakuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki
Rais wa Tanzania John Magufuli na mwenzake wa Kenya Uhuru Kenyatta wanaweka jiwe la msingi katika barabara itakayounganisha mji wa Arusha nchini Tanzania na mji wa Voi nchini Kenya.
Barabara hiyo kutoka Arusha hadi Taveta inatarajiwa kurahisisha uchukuzi na kuimarisha biashara kati ya mataifa hayo mawili.
Ina umbali wa kilomita 234 na ni sehemu ya mradi mkubwa wa barabara inayotoka Arusha na kupitia Holili na Taveta hadi Mwatate. Jiwe la msingi limewekwa na marais hao wawili eneo la Tengeru, Arusha.
Mwaka uliopita Rais Kenyatta na Rais wa Tanzania wakati huo Jakaya Kikwete walizindua mradi wa ujenzi wa barabara hiyo ya Taveta-Mwatate/Voi iliyo upande wa Kenya.

Wednesday, 2 March 2016

Tanzania na Kenya kuimarisha ushirikiano

Rais Uhuru na Magufuli katika ikulu ya rais nchini Tanzania
Kenya na Tanzania zimekubaliana kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa miundombinu na kukuza biashara.
Katika mazungumzo ya viongozi wa nchi hizo mbili, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya ameeleza kufurahishwa kuona Rais John Magufuli wa Tanzania yupo tayari kuhakikisha nchi hizo zinakuwa karibu na miradi ya maendeleo inaharakishwa.
Mradi mwingine wa maendeleo walio ujadili ni kuzalisha ajira kupitia viwanda.

Mwanawe aliyekuwa waziri mkuu wa Kenya, Raila Odinga, Rosemary, amekiri kuwa alikosea alipodai kuwa bonde la Olduvai Gorge liko Kenya ilhali liko Tanzania.

'Nilikosea, nawaomba radhi watanzania' ,Rosemary Odinga
Mwanawe aliyekuwa waziri mkuu wa Kenya, Raila Odinga, Rosemary, amekiri kuwa alikosea alipodai kuwa bonde la Olduvai Gorge liko Kenya ilhali liko Tanzania.
''Bonde la Oldupai ama Olduvai liko Tanzania, nimekubali kuwa nilikosea nilipokuwa nikihutubia mkutano wa viongozi wa vijana kutoka kote duniani nikiwa New York Marekani(International Young Leaders Assembly).
''Nahisi kama ambaye nimewakosea ndugu zangu kutoka Tanzania''.
''Nia yangu ilikuwa ni kusema kuwa nilipokuwa mdogo nikienda shuleni nilifunzwa kuwa fuvu la mtu wa kale lilipatikana Olorgesaiile eneo la Kajiado.