Wednesday, 20 January 2016

Serikali Yatoa Tamko Kuhusu Dawa Mpya ya Ukimwi Iliyogundulika Hivi Karibuni

SERIKALI imesema kama Shirika la Afya Duniani (WHO), litapitisha matumizi ya dawa mpya ya ugonjwa Ukimwi wataitumia, lakini kwa sasa haiwezi kuzungumzia tafiti za ugonjwa huo ambazo zipo nyingi.
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Michael John, amesema kwa sasa zipo tafiti nyingi, lakini wao kama wizara wanasubiri mwongozo kutoka WHO ambao ndiyo unathibitisha ubora wa dawa na matumizi yake.
“Zipo tafiti nyingi tunazisikia zinafanyika, lakini hili la Ukimwi ni mapema mno kulizungumzia ila kinachohitajika ni kusubiri mwongozo wa WHO ambao ndio wanatuongoza kwenye orodha ya dawa na matumizi yake katika magonjwa mbalimbali,” alisema John.

Sunday, 17 January 2016

CCM Chali Dar es Salaam, UKAWA Washinda Kiti ca Umeya Kinondoni na Ilala

Hatimaye baada ya danadana za muda mrefu, uchaguzi wa kuwachagua Mameya wa Manispaa za Kinondoni na Ilala, umefanyika na Umoja wa Vyama vinavyunda Katiba ya Wananchi (Ukawa) wamefanikiwa kuongoza Manispaa hizo.
Chaguzi hizo zilizhairishwa mara mbili kutokana na mvutano uliotokewa katika chaguzi za nyuma, ikiwa ni pamoja na kusimamishwa kwa amri za mahakama.

Tuesday, 12 January 2016

Nikipata mwanamke atakayeweza kuziba nafasi ya Shilole ndio nitafuta tattoo zake – Nuh Mziwanda

Ingawa Shilole tayari amefunika tattoo aliyochora kifuani yenye jina la ex wake Nuh, kwa kuongeza mchoro wa ua juu yake baada ya wawili hao kuachana, Nuh Mziwanda amesema yeye bado hajaamua kufuta tattoo zake.

Nuh ambaye alichora tattoo mbili, moja ikiwa na jina la Shishi Baby na nyingine ikiwa na sura ya Shishi amesema kuwa endapo atapata mwanamke wa kuziba pengo la Shishi ndio atafuta tattoo hizo.

Samatta ataka kusherehekea tuzo yake na majirani zake





Mbwana Samatta 


Mwanasoka Bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza soka ndani ya Afrika, Mbwana Samatta hapendi makuu kwani familia yake ilipomuuliza achague hoteli watakayomfanyia sherehe ya kumpongeza kwa kutwaa tuzo hiyo ya Afrika alichowajibu kiliwaacha hoi.






Mwanasoka Bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza soka ndani ya Afrika, Mbwana Samatta hapendi makuu kwani familia yake ilipomuuliza achague hoteli watakayomfanyia sherehe ya kumpongeza kwa kutwaa tuzo hiyo ya Afrika alichowajibu kiliwaacha hoi.
Baba mzazi wa nyota huyo, Pazi Ally Samatta akielezea alichojibiwa na mwanae huyo alisema, “Baada ya kumwambia Samatta kwamba familia imekuambia chagua ni wapi utafurahia tukikufanyia sherehe ya kukupongeza,  yeye alinijibu baba nifanyie sherehe hiyo nyumbani kwa sababu nataka kufurahia pamoja na majirani wote wanaotuzunguka,” alisema.

CUF: Uchaguzi unaweza kuzua vurugu Zanzibar

Chama cha CUF kimepinga hatua ya tume ya uchaguzi ya kufuta matokeo ya uchaguzi wa urais
Chama cha Wananchi (CUF) kimeonya kuwa kurudiwa kwa uchaguzi visiwani Zanzibar kunaweza kusababisha vurugu na kumtaka Rais wa Tanzania Dkt John Magufuli kuingilia kazi kutatua mzozo ulitokana na uchaguzi visiwani humo.
Katibu mkuu wa chama hicho Maalim Seif, akihutubia wanahabari, amesema chama hicho hakitaki uchaguzi urudiwe na kuendelea kusisitiza msimamo wa awali kwamba mshindi wa uchaguzi uliofanywa 25 Oktoba mwaka jana anafaa kutangazwa.
"Ni vyema tukaweka waziwazi hapa kwamba kurudiwa uchaguzi sio suluhishona hakukubaliki. Kwani, kama nilivyoonesha hakuna hoja wala msingi wa kikatiba na kisheria wa uchaguzi kurudiwa," amesema Bw Seif.
Bw Maalim Seif, aliyekuwa mgombea urais wa chama hicho, alionekana kupendekeza mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Jecha Salim Jecha ang’atuke.

Al-Shabab wako 'huru' kushiriki soka Somalia

Wapiganaji wa Alshabaab
Mkuu wa shirikisho la soka nchini Somalia amesema kuwa kundi la wapiganaji wa al-Shabab liko huru kushiriki katika ligi kuu ya soka nchini humo.
Abdiqani Said Arab amemuambiwa mwandishi wa BBC jijini Nairobi John Nene kwamba iwapo wapiganaji hao wanataka kushiriki watepewa fursa.
''Hatuwapingi na hawatupingi," alisema.
Kundi la al-Shabab linaloendesha itikadi kali, limewaagiza wanasoka kuvaa suruali ndefu na limepiga marufuku muziki katika maeneo linalodhibiti.

Messi atwaa tuzo ya Balloon D'or

Mshambuliaji wa klabu ya soka ya Barcelona, na timu ya taifa ya Argentina Lionel Messi, ametwaa tuzo ya mchezo bora wa dunia.
Messi mwenye miaka 28 alishinda kwa 41.33% kwa kura zote zilizopigwa, huku Cristiano Ronaldo akishika nafasi ya pili kwa 27.76% na Neymer akipata 7.86%.
Hii ni mara yake ya tano kutwaa tuzo hiyo.
Kwa upande wa wanawake nyota wa Marekani Carli Lloyd, ameibuka kuwa mchezaji bora kwa upande wa wanawake.
Goli bora la mwaka likifahamika kama Puskas limwendea Wendell Lira anayekipiga katika Atletico Goianiense ya Brazil.
Kocha wa Barcelona Muhispania Luis Enrique amechaguliwa kuwa kocha bora wa mwaka kwa kuiongoza barca kufanya vizuri barani Ulaya kwa kutwa mataji matano msimu uliopita.
Jill Ellis kocha wa kikosi cha taifa cha Marekani amekuwa kocha bora wa wanawake baada ya kuongoza timu ya taifa ya Marekani kufanya vyema katika michuano ya kombe la dunia.