Riyad Mahrez ameruhusiwa kuondoka
katika kambi ya kikosi cha Algeria na kurudi Ulaya ili kukamilisha
uhamisho wake hadi klabu mpya kulingana na shirikisho la soka nchini
Algeria.
Winga huyo wa Leicester aliwasilisha ombi la kutaka
kuondoka katika uwanja wa King Power na amehusishwa na vilabu vingi huku
Roma ikiwa tayari imewasilisha ombi la kumununua mchezaji huyo mara
tatu , ombi la mwisho likiwa lile la dau la £32m.Thursday, 31 August 2017
Monday, 14 August 2017
Waziri Mkuu aagiza wananchi wasizuiwe kuonyesha mabango
Waziri
Mkuu Kassim Majaliwa ametaka mabango yanayoonyeshwa na wananchi kwa
viongozi wa kitaifa wanapowatembelea yasiwe yanazuiwa kwa vile yanakuwa
yanaelezea changamoto wanazokabiliana nazo.
Majaliwa alisema hayo baada ya kuona mabango yaliyoinuliwa na wananchi kwenye mkutano wake na wananchi mwishoni mwa juma lililopita mjini Sikonge mkoani Tabora huku wananchi hao wakitakiwa kuyashusha.
“Siku nyingine msirudie na kuanzia sasa waacheni wananchi waonyeshe mabango yao kwani ndiyo njia wanayotumia kuonyesha hisia zao kwa yale wanayokumbana nayo na kuwasababishia kero,” alisema Majaliwa.
Majaliwa alisema hayo baada ya kuona mabango yaliyoinuliwa na wananchi kwenye mkutano wake na wananchi mwishoni mwa juma lililopita mjini Sikonge mkoani Tabora huku wananchi hao wakitakiwa kuyashusha.
“Siku nyingine msirudie na kuanzia sasa waacheni wananchi waonyeshe mabango yao kwani ndiyo njia wanayotumia kuonyesha hisia zao kwa yale wanayokumbana nayo na kuwasababishia kero,” alisema Majaliwa.
Friday, 21 July 2017
Mawakili Kigali walaani kukamatwa Rais wa wanasheria Tanganyika, Tundu Lissu
Baadhi ya Mawakili jijini Kigali wamekosoa kitendo cha
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar Es Salaam cha kumkamata rais wa
chama cha wanasheria Tundu Lissu ambaye alikuwa njiani kuelekea jijini
humo kuhudhuria mkutano.
Tundu Lissu ni Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema),
amekamatwa leo, Alhamisi, Julai 20 katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
wa Julius Nyerere (JNIA) akielekea Kigali, Rwanda kwenye kikao cha
Halmashauri ya EALS kinachoanza kesho.
”Huu ni mpango wa kumdhoofisha, kwanini asingekamatwa
jana?” amehoji wakili wa kujitegemea Rwebangiza Kiondo kutoka Tanzania,
ambaye yupo jijini humo kwa shughuli za kufuatilia uchaguzi wa Rwanda.
Wakili Rwebangiza ameiambia BBC, kuwa Polisi wanatumia
nguvu nyingi kupambana na Mwanasheria huyo ambaye alikuwa akitekeleza
majukumu yake.
”Unamkamata Wakili akiwa katika pilika za kutekeleza wajibu
wake, tena kwa kumshtukiza utafikiri ni jambazi anayetafuta, sikatai
kwamba huenda pana hoja lakini kwanini umshtukize, mtu ambaye ni
mbunge?”
Monday, 17 July 2017
TETESI ZA USAJILI LEO TAREHE 17/7/2017
Kulingana na gazeti la Sky Sports Klabu ya chelsea inataka kukamilisha dili la kumsajili mshambuliaji wa Borussia Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang , katika harakati hizo chelsea imeongeza dau lake kutoka paundi milion 65 hadi kufikia paundi ilion 70 kuhakikisha wanapata saini ya mchezaji huyo baada ya kumkosa Romeu Lukaku aliyetua Man U .Thursday, 13 July 2017
Ajira mpya 10,184 kuziba waliachishwa kazi kwa vyeti feki
![]() |
| Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais anayeshughulikia Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki |
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Rais, Utumishi, Florence Temba, ilieleza kuwa agizo hilo linazihusu Mamlaka za Serikali za Mitaa, Sekretarieti za Mikoa, Wakala wa Serikali, pamoja na Taasisi na Mashirika ya Umma.
Ilimnukuu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angela Kairuki akitoa agizo hilo wakati akizungumza katika kikao kazi na watumishi wa Umma wa Wilaya ya Kigamboni mkoani Dar es Salaam jana.
“Mgawanyo wa vibali vya ajira umezingatia upungufu uliojitokeza baada ya kukamilika kwa zoezi la uhakiki, vipaumbele vya Taifa kwa sasa na upatikanaji wa watumishi kutoka katika soko la ajira,” alisema Kairuki.
Wednesday, 12 July 2017
Tetesi za usajili leo tarehe 12.7.2017
Klabu ya Chelsea iliyo na maskani yake jiji la London imetuma ofa ya paund million 65 kwaajili ya kumsajili mshmbuliaji wa Borusia Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang raia wa Gaboni.
Meneja wa Chelsea Antoni Conte ametuma ofa hiyo baada ya
kukosa saini ya aliyekuwa mchezaji wa Everton Romeo Lukaku ambaye sasa
amejiunga na mahasimu wao Manchester United jumatatu ya wiki hii. Mpango wa
kumsajili mshambuliaji huyo uekuja baada ya Chelsea chini ya meneja wake Conte
kuonekana hana mpango na Diego Costa kwa msimu ujao ,Kwa Upande wa Dortmund wamefungua milango kwa mchezaji huyo
kuuzwa , ripoti kutoka gazeti la “The Sun ” zineleza kuwa Pierre-Emerick
Aubameyang anatamani sana kucheza ligi ya Uingereza. Aubemeyang aliibuka
mpachikaji bora wa magoli katika ligi ya ujerumani msimu wa 2016/17, PSG na AC MILLAN pia zinafuatilia saini ya mchezaji huo kwa
karibu zaidi
Subscribe to:
Posts (Atom)






