Sunday 15 May 2016

Tisho la bomu laripotiwa Old Trafford

Hofu ya kuwepo bomu uwanjani imesababisha mechi ya Manchester United na Bournemouth kuhairishwa.
Mechi ya mwisho katika ligi ya soka ya uingereza, EPL, kati ya Manchester united na Bournemouth imeahairishwa kufuatia wasiwasi wa bomu, uwanjani Old Trafford.
Kifurushi kinachoshukiwa kuwa na vilipuzi kilipatikana kimetegwa katika sehemu ya North West Quadrant.
Wachezaji wakiongozwa na kocha Louis Van Gaal walirudi kwenye chumba cha mabadiliko.
Tayari kikosi cha timu hiyo kilikuwa kinajiandaa kuingia uwanjani baada ya kutajwa. Maelfu ya mashabiki waliokuwa wanasubiri mchuano huo walilazimika kutoka nje.

Mashabiki walishauriwa kuondoka uwanjani
Wataalam wa kutegua mabomu wameingia uwanjani kwa uchunguzi zaidi. Mchuano huo ulitarajiwa kuamua hatma ya Manchester United huku ikisaka nafasi ya kushiriki kwenye ligi ya vilabu bingwa barani ulaya.
Manchester United inashikilia nafasi ya saba ikiwa na alama 63 baada ya mechi 37. Awali Mashabiki wa klabu walionyesha kughadhabishwa na utendakazi wa kocha Van Gaal, wakitaka aachishwe kazi.
Hii ni baada ya Westham kuzamisha matumaini ya klabu hiyo kwa kuizaba 3-2 wiki iliyopita.

No comments: