Thursday 26 May 2016

Mshukiwa wa ulipuaji Kampala apatikana na hatia

LuyimaMshukiwa mkuu wa mashambulio ya kigaidi yaliyotekelezwa mjini Kampala mwaka 2010 amepatikana na hatia.
Isa Ahmed Luyima amepatikana na kosa la ugaidi.
Luyima alikuwa ameshtakiwa pamoja na washukiwa wengine 12 kuhusiana na mashambulio hayo yaliyosababisha vifo vya watu 74.

Kundi la Kiislamu la al-Shabab kutoka Somalia lilidai kuhusika.
Jaji Alfonse Owinyi Dollo awali alikuwa ameamua kwamba washukiwa wote hawana hatia ya kuwa wanachama wa kundi la kigaidi kwa kuwa kundi la al-Shabab, halikuwa limeorodheshwa kuwa kundi la kigaidi mwaka 2010.
 
Washukiwa wameondolewa hatia ya kuwa wanachama wa kundi la kigaidi.
Kesi hiyo imechukua muda wa miaka sita.
Mahakama bado haijatoa uamuzi kuhusu makosa hayo mengine yanayowakabili washukiwa hao ambayo ni pamoja na mauaji na kusaidia ugaidi.

No comments: