Thursday 26 May 2016

Klabu ya soka yafungwa mabao 44 Ecuador, Mchezaji afunga mabao 18 pekee

Pelileo Sporting ClubUwanja ulikuwa na mashabiki 200 wakati wa mechi hiyo
Klabu moja ya soka nchini Ecuador imepata ushindi mkubwa ambao ukiidhinishwa basi itakuwa rekodi mpya ya ufungaji mabao duniani.
Klabu hiyo ya Pelileo Sporting Club ilicharaza Indi Native mabao 44-1 katika mechi ya ligi ya daraja la tatu nchini humo mbele ya mashabiki 200.

Mshambuliaji wa Pelileo Ronny Medina alifunga mabao 18.
Rais wa Indi Native Diego Culequi amesema matokeo hayo hayakutarajiwa na wachezaji hawakuwa wamezoea joto kali ambalo anasema lilichangia kushindwa kwao.
Mwandishi wa habari Mwingereza Tim Vickery, ambaye amekuwa Brazil kwa miaka 20, amesema Bon Accord kwa sasa wamejadiliwa sana katika vyombo vya habari Ecuador.
Anasema ligi ya daraja la tatu ya Ecuador huwa na ushindani mkubwa.
Rekodi ya sasa inashikiliwa na Arbroath FC ya Scotland iliyofunga mabao 36-0 dhidi ya Bon Accord miaka 131 iliyopita.
Mwenyekiti wa Arbroath FC John Christison amesema ana wasiwasi kiasi kwamba rekodi yao waliyoiweka 1885 huenda ikavunjwa.
Amesema klabu hiyo itasubiri uamuzi wa Guinness World Records.
44-1
matokeo ya mechi kati ya Pelileo Sporting Club na Indi Native nchini Ecuador
  • Pelileo Sporting Club
    18 mabao aliyofunga mshambuliaji wa Pelileo Ronny Medina
  • 131 miaka ambayo rekodi ya sasa, Arbroath 36-0 Bon Accord, imedumu
Bw Christison ameambia BBC Scotland: "Ni rekodi ambayo tumeishikilia kwa miaka 130.
"Tutasikitika sana kama klabu iwapo tutaipoteza rekodi hii ambayo kama jiji twajivunia sana.
“Ilifahamika sana kwamba wakati huo kipa wetu hata hakugusa mpira na alisimama kwenye goli na mwavuli kwani mvua kubwa ilikuwa inanyesha.
"Lakini tutasubiri uamuzi wa maafisa wa Guinness.”
Siku hiyo ya ushindi wa Arbroath mwaka 1885, Dundee Harp walilaza Aberdeen Rovers 35-0.
Ingawa mwamuzi alisema mabao yalikuwa 37, karibu wa Dundee Harp alisema alirekodi 35 pekee, mabao ambayo mwishowe yalitambuliwa.
Mwaka 2002, mechi ya ligi kuu ya Madagascar ilitoa matokeo ya kushangaza baada ya mabingwa wateule AS Adema kulaza mahasimu wao wa jadi Stade Olympique I'Emyrne 149-0. Wachezaji wa Olympique walijifunga makusudi kwa hasira kulalamikia uamuzi wa refa.
Matokeo ya mechi hiyo hayakutambuliwa kimataifa.

No comments: