Wednesday 8 February 2017

MCHUNGAJI LUSEKELO (MZEE WA UPAKO) ALAANI UTARATIBU UNAOTUMIKA KUWATAJA WATU BILA KUWA NA UHAKIKA WA KUTOSHA.

Mzee wa upako dakika chache zilizopita alipokuwa kwenye kipindi cha 'Kikaangoni' kinachorushwa moja kwa moja na EATV, amesema kuwa kilichopaswa kufanywa ni kuwaandikia summons washukiwa hao, kuwataka kuripoti polisi kwa mahojiano, na sio kuwaita kupitia magazeti, na kuwataja majina kwenye vyombo vya habari.
Mzee wa upako alipoulizwa swali kuhusiana na mchungaji Gwajima kutajwa na Makonda, amesema kuwa kumtaja mtu juu ya tuhuma hizi ni lazima kuwe na uhakika wa kutosha, kuwe na ushahidi wa kutosha, na sio kumtaja mtu bila ushahidi wa kutosha, ni kumdhalilisha mtu, kumshushia heshima yake, na kumsononesha moyoni.

Ametolea mfano kwake, kuwa mwaka 1997 aliwahi kutajwa kuwa anauza madawa ya kulevya, lakini utaratibu uliotumika ni kwamba, walimfuata Askari wa Interpol (mambo ya ndani), wakamuandikia summon ya karatasi kuwa anahitajika polisi kwa mahojiano, alikwenda polisi wakazungumza naye, akawaambia "ninyi ni polisi, fanyeni uchunguzi, " basi polisi walipojiridhisha kuwa hahusiki, walimwacha huru, japo habari ile ilivuja kwa vyombo vya habari na ikamchafulia jina kwa muda wa takribani miaka Saba mpaka alipofanikiwa kuirejesha heshima yake.
Kwahiyo, Mzee wa upako amekazia kuwa, mtu kujijengea heshima kwenye jamii inamchukua miaka mingi, kupata heshima sio kazi ndogo, lakini inapokuja wakati unashushiwa heshima kwa sababu zisizo za msingi, inaumiza sana.

No comments: