Thursday, 12 December 2013
Wednesday, 11 December 2013
Bunge laanza kuchambua ripoti za Kamati
. Mkutano wa 14 wa Bunge, unaendelea mjini
Dodoma leo. Inatarajiwa kwamba wabunge wataendelea kutema cheche dhidi
ya utendaji usioridhisha wa baadhi ya mawaziri.
Kwa mujibu wa ratiba ya mkutano huo, leo wabunge
watachangia ripoti tatu za kamati za kudumu za Bunge zinazosimamia fedha
za umma zilizowasilishwa wiki iliyopita.
Ripoti zitakazoendelea kujadiliwa ni pamoja na ya
Kamati ya Serikali za Mitaa (Laac), ambayo inaonekana kuwagusa wabunge
wengi kutokana na kuibua ufisadi wa kutisha.
Wabunge pia wataendelea kuchangia ripoti ya Kamati
ya Bunge ya Hesabu za Serikali na Mashirika ya Umma inayoongozwa na
Zitto Kabwe (PAC) na ile ya Bajeti inayoongozwa na Andrew Chenge.
Baada ya kukamilika kwa mijadala hiyo, Serikali
inatarajiwa kujibu hoja mbalimbali za wabunge ambao wameonyesha
kutoridhishwa na utendaji wa baadhi ya mawaziri.
Kuendelea kuwapo kwa vitendo vya wizi, ubadhirifu
na ufisadi kwa baadhi ya wizara kunaonekana kuwachefua wabunge hata
baadhi yao kumshauri Rais Jakaya Kikwete kuwawajibisha.
Baadhi ya wabunge waliochangia Ijumaa na Jumamosi
iliyopita walimtaka Rais Kikwete kumfukuza kazi Waziri Mkuu, Mizengo
Pinda. Wengine walimtaka amfukuze kazi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri
Mkuu, Tamisemi, Hawa Ghasia, kwa kushindwa kukabiliana na ufisadi.
Mbunge wa Mwibara (CCM), Kangi Lugola ndiye
aliyekuwa mwiba kwa Pinda akisema amekuwa mpole na hawajibiki ipasavyo.
Alisema katika nchi nyingine, wakati Kamati za Bunge zinawasilisha
taarifa zake ndipo jicho la wananchi na Serikali linakuwa bungeni lakini
kwa Tanzania imekuwa ni tofauti.
Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David
Kafulila alisema taifa lina matatizo makubwa mawili ambayo ni ukusanyaji
kodi na matumizi mabaya ya fedha.
“Tunaposema Serikali imechoka maana mbadilishe
kikosi, mpaka dakika 90 ziishe? Wabunge wa CCM mtakubaliana nami kwamba
hii ni dalili kwamba mmechoka mbadili kikosi,” alisema na kuongeza:
“Waziri Mkuu wetu tumeshamzoea kila suala
tunalomwambia anakwambia tunaangalia, tunafuatilia, tuko mbioni
yanazungumzika… tumechoka na haya.”
Alisema mawaziri mizigo walitajwa katika ziara ya
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana wako wanne lakini Pinda ndiye
namba moja.
Simba yafuta makosa ya Cannavaro, Yondani
KOSA la kumzuia straika Amisi Tambwe
lililofanywa na mabeki wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Kelvin
Yondani hadi akapiga pasi kwa mfungaji Betram Mombeki, sasa linafanyiwa
kazi na kikosi cha Simba.
Mombeki alifunga bao hilo dakika ya 54 baada ya
kupokea pasi murua ya Tambwe ambaye aliwazidi ujanja Yondani na
Cannavaro ambao walijipanga vibaya kwa kumzuia Tambwe lakini straika
huyo aliwazidi ujanja na kumpa pasi mfungaji.
Katika pambano hilo la Ligi Kuu Bara lililochezwa Oktoba 20, mwaka huu kaika Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, Yanga ilikuwa ikiongoza kwa mabao 3-0 hadi mapumziko lakini Simba ilisawazisha mabao yote kipindi cha pili.
Katika pambano hilo la Ligi Kuu Bara lililochezwa Oktoba 20, mwaka huu kaika Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, Yanga ilikuwa ikiongoza kwa mabao 3-0 hadi mapumziko lakini Simba ilisawazisha mabao yote kipindi cha pili.
Kwa muda mrefu kwenye mazoezi ya Simba mwishoni
mwa wiki iliyopita, Kocha wa Simba, Zdravko Logarusic ameonekana
akiwahimiza mabeki wake hasa wa kati kusimama katika nafasi sahihi
wakati timu inaposhambuliwa.
Logarusic alionekana akitilia mkazo sehamu ya
kusimama mabeki wake na mara kwa mara alikuwa akiwaelekeza kwa ukali
baadhi ya mabeki waliokuwa wakirudia makosa ya kutokuwapo sehemu husika.
Kocha huyo alienda mbali zaidi kwa kuwafundisha mabeki wake namna ya
kusimama wanapokuwa wanakaba jambo lililokuwa likishangiliwa na
mashabiki wachache wa Simba waliohudhuria mazoezi hayo.
Muda mfupi baada ya mazoezi hayo, Logarusic raia
wa Croatia aliliambia Mwanaspoti; “Beki yeyote mzuri lazima awe anajua
mahala sahihi pa kusimama na usimamaji wake unapaswa kuwa madhubuti
ndiyo maana umeona nawasisitizia.”
Umoja wa Mataifa wapeleka ndege za Drone Congo.
Umoja wa Mataifa utaanza kurusha ndege zenye kamera zisizotumia
rubani-Drones - kwenye anga ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo-DRC hapo
Jumanne ili kuwasaidia walinda amani kuwasaka waasi na kufuatilia
mienendo yao.
Mkuu wa walinda amani katika Umoja wa Mataifa, Herve Ladsous yupo mjini Goma kushuhudia uzinduzi huo wa Drones. Alisema Jumatatu kwamba hali huko mashariki mwa Congo ni tofauti sana kutoka mwaka mmoja uliopita wakati kundi la waasi wa M23 walipoiteka miji kadhaa katika eneo hilo.
Mwezi uliopita kundi la M23 lilitangaza kuweka chini silaha zake baada ya jeshi la Congo kuteka ngome ya mwisho ya kundi hilo kwa msaada wa kikosi maalumu cha Umoja wa Mataifa.
Mkuu wa walinda amani katika Umoja wa Mataifa, Herve Ladsous yupo mjini Goma kushuhudia uzinduzi huo wa Drones. Alisema Jumatatu kwamba hali huko mashariki mwa Congo ni tofauti sana kutoka mwaka mmoja uliopita wakati kundi la waasi wa M23 walipoiteka miji kadhaa katika eneo hilo.
Mwezi uliopita kundi la M23 lilitangaza kuweka chini silaha zake baada ya jeshi la Congo kuteka ngome ya mwisho ya kundi hilo kwa msaada wa kikosi maalumu cha Umoja wa Mataifa.
Wanamgambo waanza kuondoka Tripoli
Wapiganaji wa jeshi la mgambo huko Libya wanaolaumiwa kwa ghasia mbaya
mjini Tripoli tangu kuanguka kwa Moammar Ghadafi walianza kuondoka
katika mji mkuu Jumatatu huku vikosi vya jeshi la Libya vikiingia
kuhakikisha usalama mitaani.
Wanamgambo kutoka pwani ya mji wa Misrata walianza kuondoka kuelekea mashariki baada ya kutokea ufyatuaji risasi kwa waandamanaji Ijumaa na kuchochea siku mbili za mapambano ambayo yaliuwa watu wasiopungua 46 na kuwajeruhi mamia wengine.
Pia Jumatatu naibu mkuu wa upelelezi nchini Libya, Mustafa Nuh aliachiwa huru na watekaji nyara wake siku moja baada ya kumkamata wakati akiondoka kwenye uwanja wa ndege wa Tripoli.
Haikufahamika ni nani alimteka Nuh ambaye familia yake inatokea Misrata.
Wanamgambo kutoka pwani ya mji wa Misrata walianza kuondoka kuelekea mashariki baada ya kutokea ufyatuaji risasi kwa waandamanaji Ijumaa na kuchochea siku mbili za mapambano ambayo yaliuwa watu wasiopungua 46 na kuwajeruhi mamia wengine.
Pia Jumatatu naibu mkuu wa upelelezi nchini Libya, Mustafa Nuh aliachiwa huru na watekaji nyara wake siku moja baada ya kumkamata wakati akiondoka kwenye uwanja wa ndege wa Tripoli.
Haikufahamika ni nani alimteka Nuh ambaye familia yake inatokea Misrata.
Makamu wa marais na mawaziri waapishwa Sudan
Rais Omar al-Bashir amehudhuria sherehe za kuapishwa kwa makamu wa
marais wawili walioteuliwa hivi karibuni pamoja na wasaidizi na mawaziri
wapya, ambao wote wanatoka Chama tawala cha National Congress CNP.
Mabadiliko ya baraza la mawaziri nchini Sudan yamekuja baada ya nchi
hiyo kuendelea kukumbwa na hali ya kukosekana kwa utulivu wa kisiasa.
Makundi ya waasi wa Sudan ambao mara kwa mara wanalalamikia hali ya
kuwekwa kando na maendeleo yasiyo na uwiano katika maeneo nje ya
Khartoum, wanaendelea na mapambano, huku hali ya kuzorota kwa uchumi
mjini Khartoum na kupanda kwa bei za bidhaa zikisababisha malalamiko na
vifo vya watu wengi katika mwezi Septemba mwaka huu.
Wanajeshi wa UN wapambana na waasi DRC
Kamanda huyo, Generali Carlos Alberto dos Santos
Cruz, anasema kwamba wanajeshi wake wanajiandaa kupambana na waasi wa
FDLR walio Katika mkoa wa Kivu Kaskazini.
Kamanda wa wanajeshi wa Umoja wa mataifa katika
Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo, anasema kuwa wanajeshi wake wameanza
kupambana na waasi wa Kihutu kutoka Rwanda pamoja na makundi mengine ya
waasi Mashariki mwa nchi.
Kundi hilo, lilianzishwa na wapiganaji wa kihutu
waliokimbilia Congo Mashariki kutoka Rwanda wakati wa mauaji ya kimbare
mwaka 1994.Mwezi jana wanajeshi wa UN kwa kutumia nguvu waliweza kuwashinda waasi wa M23 waliokuwawanaendesha harakati zao Mashariki mwa Congo.
Subscribe to:
Posts (Atom)




