Monday 23 February 2015

Kova atoa ufafanuzi juu ya kutekwa kwa Kiongozi wa JKT





KATIKA hali isiyokuwa ya Kawaida jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limesema aliamini kwamba Mwenyekiti wa Umoja wa Wa wanajeshi waliokuwa kwenye mafunzo JKT ,wanaoshinikiza Serikali iwatafutie Ajira kwamba ametekwa na watu wanadaiwa ni Usalama wa Taifa,badala yake Jeshi hilo limesema litafanya Uchunguzi ili kujilidhisha juu ya Sakata hilo.AnaripotiKAROLI VINSENT Endelea nayo.
Kauli hiyo ya Jeshi hilo la Polisi imekuja huku bado Mwenyekiti huyo Bwana GEORGE S/O GALUS MGOBA,Miaka 28 akiwa amelezwa kwenye Hospitali ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam baada ya kutekwa na watu wasiojulikana na kutupwa kwenye Msitu ulioko Pugu Mkoa wa Pwani huku mwili huo ukiwa umechoka kutokana na kipigo alichopigwa watekaji hao.
Taarifa hiyo ya Jeshi la Polisi imetolewa mda huu Jijini Dar es Salaam,na Kamishna wa kanda Maalumm ya Dar es Salaam Suleimani Kova wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari ambapo Kova huku akisema kwa kujihamini amesema jeshi hilo haliamini kama kiongozi huyo ametekwa mpaka pale watakapofanya uchunguzi na kulidhisha.
“Taarifa za kutekwa siwezi kuziaamini mpaka tuunde tume ichunguze na tufahamu nani kamteka huyo mtu,ili tujue harafu tuweze kubaini maana isije kuwa watu wanataka umahaarufu kwa kutumia mipango hiyo,na tukimaliza kuchunguza kama ni kweli ametekwa tutachukua hatu”
“Kwasababu huyo mwenyekiti anasema ametekwa na amechomwa sindano ya sumu na watekaji,kwanini sasa anakataa kupimwa na madaktari,kuna nini hapa tena anataka hadi kutoroka hospitalini na juzi tulimkamata nje ya mrango wa hospitali akitaka kukimbia sasa hapa kuna nin jamani kwahiyo lazima tufanye uchunguzi suala hili”amesema Kamishna Kova.
Mtifuano wa Kamishan Kova na Waandishi wa Habari
Katika hali ya kushangaza wakati wa mkutano huo na waandishi Wa Habari ulibadilika na kuwa sehemu ya Mabishano pale Waandishi hao walipokuwa wanataka ufafanuzi kuhusu kurudia mara kwa mara kwa matukio hayo ya utekaji kwa watu mbalimbali kwaanzia—
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini Dokta Steven Ulimboka na Mhariri Mtendaji wa Magazeti ya NewHabari nchini Bwana Kibanda na Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Mawio Saed Kubenea ambao wate walifanyiwa vitendo viovu na vya kihalamia.
Kamishna huyo akageuka mbogo na kuwataka Waandishi wa Habari waache maswali ya Uchochezi kwani matukio hayo yalishafanyiwa kazi na ufumbuzi ulishapatikana na aliwataka waandishi wakitaka kuuliza maswali ya hayo waandae siku maalum kwa ajiri ya maswali na yeye atakuwa tayari kuwajibu.
Katika hatua Nyingine Jeshi hilo Kanda maalum ya Dar es Salaam limesema limewakamata vijana wapatao watano ambao ni viongozi wa “Umoja wa Kikundi cha wahitimu wa mafunzo ya Jeshi la kujenga Taifa” kwa makosa ya uchochezi na mikusanyiko isiyo halali jijini Dar Es Salaam. Watu hao wanatabia ya kujikusanya kwenye kundi la vijana wasiopungua 300.
Kamishna Kova amesema Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa umoja huo hauna usajili kisheria na hakuna ahadi yeyote ambayo kikundi hicho kimepewa.
Ambapo Kamishna huyo amewataja Wanaohojiwa mpaka sasa ni pamoja na Mwenyekiti wa kikundi hicho aitwaye GEORGE S/O GALUS MGOBA, Miaka 28, Mkazi wa Mabibo Loyola.
Mwingine ni Katibu wa kikundi hicho aitwaye LINUS S/O EMMANUEL, Miaka 28, Mkazi wa Tabata.
Wakati huo huo Makamu Mwenyekiti wa umoja wa vijana waliohitimu JKT anayejulikana kwa jina la PARALI S/O ARUWERA KIWANGO, Miaka 25, Mkazi wa Temeke Mikoroshini, anatakiwa kujisalimisha haraka katika ofisi ya Mkuu wa Upelelezi Polisi Kanda Maalum Dar es salaam au kituo chochote cha Polisi cha karibu na mahali aliko. Mtuhumiwa huyo alitoroka baada ya kugundua katibu wake amekamatwa hivyo anatakiwa ajisalimishe kuhojiwa kwa matukio hayo.
Kamishna huyo amesema Katika suala hili la wahitimu wa JKT, kuanzia sasa Jeshi la Polisi litachukua hatua kali kudhibiti mkusanyiko au mkutano wa aina yeyote kwani haina uhalali wowote kisheria. Imegundulika kwamba mikusanyiko ya vijana hawa ni uchochezi na siyo halali kisheria hivyo haikubaliki. Yeyote atakayejaribu kushiriki katika mkusanyiko wa aina hiyo awe ni kiongozi au mjumbe atachukuliwa hatua kali haraka sana.
Historia ya kutekwa
Mnamo tarehe 22/02/2015 majira ya saa 11:45 jioni mtuhumiwa GEORGE S/O GALUS akiwa chini ya ulinzi alijaribu kutoroka kutoka wodini katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikolazwa lakini Polisi walimbaini na kumkamata kabla hajatokomea. Jalada la utoro chini ya ulinzi halali limefunguliwa na uchunguzi linaendelea.
Aidha tukio la mtuhumiwa GEORGE S/O GALUS kudai kutekwa kati ya tarehe 16/02/2015 hadi 19/02/2015 linaendelea kuchunguzwa kwa ushirikiano kati ya Mkoa wa Pwani na Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam ili kubaini ukweli wa taarifa hiyo na kuwajua wanaosemekana kumteka

No comments: