Wednesday 6 August 2014

Evance Aveva amrudisha Mbabe wa Yanga Kundini


Rais wa klabu ya Simba, Evans Aveva  
Jumapili Simba walifanya Mkutano Mkuu wa wanachama ambapo walifanya mabadiliko ya Katiba katika baadhi ya vipengele huku Ibara ya 25 kipengele cha 8(iii) kimeonekana kumrudisha kundini kihalali Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Zacharia Hans Poppe.
Kigogo huyo amekuwa tishio kwa Yanga haswa kutokana na ushawishi wake.
Kabla ya mabadiliko hayo, kipengele hicho ambacho kinahusu viongozi watakaochaguliwa na Mkutano Mkuu wa uchaguzi ni wajumbe watano wa Kamati ya Utendaji, pia Rais atateua wajumbe wengine watano wa Kamati ya Utendaji ambao anaweza kuwabadilisha kwa kadiri anavyoona inafaa.
Kipengele hicho kimeendelea kuelezea kuwa wajumbe hao wa kuteuliwa wanatakiwa kuwa na sifa zile zile wanazotakiwa kuwa nazo wajumbe wa kuchaguliwa na wanachama.
Hivyo katika marekebisho ya kipengele hicho ni kwamba wajumbe watano wa Kamati ya Utendaji watachaguliwa na wanachama, lakini Rais atateua wengine watano wa kamati hiyo ambao anaweza kuwabadilisha kwa kadiri anavyoona inafaa na hawatakiwi kuwa na sifa kama zile za wajumbe wa kuchaguliwa.
Hiyo inamaana kwamba wajumbe hao wa kuteuliwa wanatakiwa kuwa na sifa ya uanachama wa klabu hiyo tu. Tayari Rais wa klabu hiyo, Evans Aveva ameteuwa wajumbe watatu ambao ni Mohamed Nassoro, Salim Abdallah na Musley Saleh hivyo amebakiwa na nafasi mbili za kujaza.
Kwa mamlaka aliyona sasa, Aveva anaweza kutumia nafasi hiyo kumpachika Hans Poppe ambaye hawezi kugombea nafasi yoyote ndani ya Simba kutokana na kubanwa na Ibara ya 26 (4) kinachosema mgombea asiwe aliyewahi kutiwa hatiani kwa kosa la jinai kwa kuhukumiwa kifungo.
Tayari Hans Poppe ambaye ni mmoja wa wanachama wa Simba wenye ushawishi mkubwa alishatamka wazi kuwa hawezi kugombea tena Simba kutokana na kubanwa na kipengele hicho

No comments: