Eneo la uwanja huo utakaoitwa Mbeya City Arena upo
lipo Iwambi jijini Mbeya ambapo ni nje kidogo ya jiji hilo na una
ukubwa wa hekta mita 5.7.
Kuhusu maandalizi ya timu, Kimbe alisema kuwa
wamewasilisha majina ya wachezaji wao Shirikisho la Soka Tanzania (TFF)
ambapo wataingia kambini Agosti 15 akiwamo Saady Kipanga ambaye
inasemekana tayari yupo jijini Mbeya.
Kipanga alikuwa ni miongoni mwa wachezaji ambao
walidaiwa kusajiliwa na Simba msimu ujao, lakini dili hilo liliingia
mchanga baada ya wajumbe wa Kamati ya Usajili kutokubaliana na usajili
wake na hivyo kumsajili Elius Maguli wa Ruvu Shooting.
No comments:
Post a Comment